Skip to main content

UN NA SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUDUMISHA AMANI ILIYOPO NCHINI



Mgeni rasmi Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues (wa pili kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari (UTPC), Abubakar Karsan mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Nyanza jijini Mwanza kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Amani ambapo kitaifa yamefanyika jijini humo na kuandaliwa na Baraza la Dini mbalimbali la Amani Tanzania (IRCPT) kwa ushirikiano wa UNESCO ambapo yaliwashirikisha Viongozi wa Serikali, Asasi za Kiraia, Waandishi wa habari, Viongozi wa madhehebu ya dini, Jeshi la Polisi, Walemavu, Wananchi pamoja na Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa. Kushoto ni Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi na wa pili kulia ni Afisa Mfawidhi Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa kanda ya ziwa Mwanza, Bw. Ludovick Ringia.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).


Na Mwandishi Wetu, Mwanza

Umoja wa Mataifa (UN) umesema utaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kulinda na kudumisha amani ya pamoja kwa makundi yote ili amani iliyopo itumike kuleta maendeleo endelevu nchini.

Hayo yamebainishwa na Mgeni rasmi Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues, wakati akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya Amani Duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Mwanza (Septemba 21.2015).

Bi.Rodgrigues amesema amani ya pamoja inatoa nafasi kwa kila mmoja kuwa mshirika wa kudumisha na kuendeleza amani bila kujali itikadi, imani au matabaka mbalimbali yaliyipo ndani ya jamii.

Amefafanua kuwa Tanzania ni mfano wa kuigwa katika kulinda amani, hivyo nguvu ya pamoja ni muhimu katika kufikia malengo na maendeleo yanayotakiwa kutokana na kuwepo kwa utulivu, mshikamano, umoja, na amani.

Kwa upande wake, Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amewataka watanzania kuachana na propaganda za kisiasa zinazoleta chuki na hasa katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Jaji Mutungi ameeleza kuwa amani haina tabaka na kusisitiza umuhimu wa wananchi kupiga kura kwa kutumia falsafa ya kulipenda taifa na kuwaonya viongozi wa vyama vya siasa kuacha kuwadharau watanzania ambao wameilinda amani kwa muda mrefu.

Nalo Jeshi la Polisi mkoani humo, limelaani kitendo kilichofanywa na watu wanaoaminika kuwa ni wafuasi wa vyama vya siasa kwa kushambulia polisi na kuvunja vioo vya gari la polisi kwa kusingizio cha kampeni za uchaguzi.

Katika tukio hilo imeelezwa kuwa, baada ya watu waliokuwa wakitokea katika mkutano wa kampeni wa umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) kushambulia Polisi, kuvunja vioo vya gari la polisi na kujeruhi askari.


Mkuu wa wilaya ya Nyamagana, Baraka Konisaga akisoma hotuba kwa niaba ya Kaimu Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo kwenye maadhimsho ya siku ya kimataifa ya Amani Duniani ambapo kitaifa imefanyika jijini Mwanza.

Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Charles Mkumbo ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika kilele hicho cha siku ya Amani jijini hapa.

Kamanda Mkumbo ameeleza kuwa kitendo hicho ni uhalifu kama uhalifu mwingine na polisi haiwezi kuvumilia vitendo vya aina hiyo na hasa wakati huu ambapo kampeni za uchaguzi zinaendelea.

Maadhimisho ya siku ya amani duniani yanafanyika septemba 21, kila mwaka ili kukumbuka na kulinda amani na kauli mbiu ya mwaka huu ni “Amani Kwanza – Utamaduni wetu wa amani ni nguvu yetu”. Ambapo siku hiyo pia viongozi mbalimbali waliweza kuhudhuria siku hiyo wakiwemo viongozi wa siasa, dini, jeshi la Polisi, viongozi wa serikali na binafsi pamoja na wananchi mbalimbali.


Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues akitoa ujumbe maalum kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Unesco, Irina Bokova kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Amani Duniani ambayo kitaifa imefanyika jijini Mwanza.


Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Charles Mkumbo akizungumza kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Amani Duniani ambayo kitaifa imefanyika jijini Mwanza.


Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi akitoa nasaha zake kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Amani Duniani ambapo kitaifa yamefanyika jijini Mwanza.


Jukwaa kuu la viongozi mbalimbali waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Amani ambapo kitaifa imefanyika jijini Mwanza.


Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Charles Mkumbo akiteta jambo na Mgeni rasmi Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Amani, ambapo kitaifa imefanyika jijini Mwanza.


Kikundi cha kwaya ya Patimo-Mabatini jijini Mwanza kikitoa burudani kwenye maadhimisho hayo.


Burudani ya Qaswida maalum iliyobeba ujumbe wa kutunza 'Amani' ikitolewa.


Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Baraka Konisaga akiweka saini kwenye Azimio maalum la kuenzi Amani lililoandaliwa kwenye maadhimisho hayo huku Mgeni rasmi Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Dini mbalimbali la Amani Tanzania (IRCPT), Rev. Canon Godda (wa pili kulia) wakishuhudia tukio hilo.


Kamanda wa Polisi Mkoani Mwanza, Kamishina Msaidizi wa Polisi, Charles Mkumbo (kushoto) na viongozi mbalimbali wa dini wakiendelea kusaini Azimio hilo.


Mgeni rasmi Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues akiweka sahihi kama shuhuda katika kupitisha Azimio hilo.


Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi naye akiweka saini kama shuhuda wa kupitisha Azimio hilo. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Baraka Konisaga.


Pichani juu na chini ni makundi ya Viongozi mbalimbali wa madhehebu ya dini, Viongozi wa Serikali, Asasi za Kiraia, Waandishi wa habari, Jeshi la Polisi na Walemavu waliodhuruia siku ya Kimataifa ya Amani Duniani ambapo kitaifa imefanyika jijini Mwanza katika viwanja vya Shule ya msingi Nyanza.





Wawakilishi wa vikundi vya vijana walioshiriki maadhimisho ya siku ya Amani Duniani ambayo kitaifa yamefanyika jijini Mwanza.


Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya msingi Nyanza walikuwa ni miongoni mwa washiriki wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya Amani duniani.


Meza kuu katika picha ya pamoja.


Washiriki katika picha ya pamoja na meza kuu.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...