Skip to main content

UNESCO, TCRA YATAKA WADAU WA HABARI KATIKA MATUMIZI YA INTANETI KUZINGATIA USIRI NA MAADILI



Mwenyekiti wa National Governance Internet Forum ambaye pia ni Rais wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akiwakaribisha wadau wa mitandao na watumiaji wa intaneti kwenye jukwaa hilo kabla ya kumkaribisha mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA kufungua rasmi jukwaa hilo.. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Tanzania Education and Research Network (TERNET), Amos Nungu na Kushoto ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph akifuatiwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Sunday Richard. (Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Na Mwandishi Mwetu

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO), limewaomba wadau wa habari hasa wa matumizi ya intaneti kuzingatia maadili na usiri katika kazi zao ili kutovunja sheria zilizowekwa na mamlaka husika likiwemo suala la sheria ya mtandao iliyopitishwa hivi karibuni nchini Tanzania.

Hayo yameelezwa na Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyekuwa akimwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues katika Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF), lililofanyika mwishoni mwa wiki na kuandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).

UNESCO inaamini masuala ya usiri katika mitandao ni njia bora zaidi za kuepukana na suala la mmomonyoko wa maadili na usio zingatia taaluma.

Ambapo amebainisha kuwa, takribani Asilimia 84 ya Mataifa duniani wamegundua hawana sheria madhubuti ya kulinda uhuru wa usiri kwa wananchi kupitia mitandao hivyo ni muhimu kuzingatia taaluma na maadili kwenye matumizi ya intaneti hasa kwa kipindi hichi.

“UNESCO inaamini mambo muhimu ya kuzingatia juu ya matumizi ya mitandao ikiwemo kuwa na Uwazi, Upatikanaji na Ushirikishi. Kwa hayo machache, mjadala huu wa matumizi ya mtandao unaweza kufanikiwa na sie tunapenda kuungana na nyinyi katika kushirikiana katika suala hili” alieleza Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.


Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Sunday Richard akifungua rasmi Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF) lililoandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) na kufanyika mwishoni mwa juma katika ukumbi wa mikutano COSTECH jijini Dar. Kushoto ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyemwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO na kulia Mwenyekiti wa National Governance Internet Forum, Kenneth Simbaya.

Aidha, katika mkutano huo, imeelezwa kuwa, matumizi makubwa ya mtandao wa kompyuta (intaneti) yatasaidia ongezeko la pato la taifa (GDP).

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya jukwaa la mtandao wa intaneti (IGF) Kenneth Simbaya wakati wa jukwaa hilo ambapo amebainisha kuwa, katika matumizi yake ni muhimu sana kujadili kutengeneza kesho wanayoitaka watanzania katika matumizi ya mtandao.

Ameeleza chombo cha IGF kimelenga kuangalia maendeleo ya mtandao nchini usalama wake na matumizi ya mtandao yanayoelenga kubadilisha maisha ya watanzania kwani chombo hicho nchini Tanzania kimeundwa kutokana na mkutano wa kimataifa wa jamii ya wanahabari (WSIS) waliotaka kuwepo na jukwaa kuangalia matumizi ya matandao kutokana na kuongeza kwa haja ya matumizi.

Simbaya amesema Majukwaa hayo yanatakiwa kuzungumza kuhusu sera kwa lengo la kuangalia uendelevu wake , usalama, ukuaji wa mtandao wenyewe na menejimenti yake.

Kwa upande wake Mtaalamu kutoka TCRA Dk. Emmanuel Manasseh akithibitisha umuhimu wa mtandao katika maisha ya sasa na yajayo, alielza kwamba kama kutakuwepo na ongezeko la watumiaji angalau kwa asilimia 10 pato la taifa litaongezeka kwa asilimia 1.4. zaidi.

Ambapo anaendelea kubainisha kuwa, kwa sasa idadi ya watumiaji wa mtandao wameongezeka kufikia asilimia 11 na kwamba lugha ya mtandao kwa sasa inaathiri watu mbalimbali kwa namna njema na namna mbaya.

Jukwaa hilo pamoja na kuzungumza kuhusu uendelevu wake pia ulizungumzia sheria , kanuni na taratibu zinazotakiwa kuzingatiwa katika matumizi na utawala wa intaneti ili kuzifanya zitumike kwa makusudio mema zaidi.

Naye mtaalamu wa masuala ya mtandao wa intaneti, Maxence Melo kutoka Jamii Forum amesema kwamba mpaka sasa anaona kwamba matumizi ya mtandao Tanzania bado salama ingawa juhudi lazima ziendelee kufanyika kuhakikisha kwamba hali ya usalama inaendelea kuwapo.


Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyemwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO akitoa salamu za shirika la UNESCO wakati wa mkutano wa Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF) ulioandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).


Katibu Mtendaji wa Tanzania Education and Research Network (TERNET), Amos Nungu akitoa salamu za TERNET kwa wadau waliohudhuria jukwaa hilo.


Mtaalamu kutoka TCRA Dk. Emmanuel Manasseh akiwasilisha mada iliyoelezea umuhimu wa mtandao katika maisha ya sasa na yajayo wakati wa jukwaa hilo.


Pichani juu na chini ni sehemu ya washiriki waliohudhuria jukwaa hilo wakifuatilia "presentation" iliyokuwa ikitolewa na Mtaalamu kutoka TCRA Dk. Emmanuel Manasseh (hayupo pichani).





Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph kwa mtaalamu kutoka TCRA (hayupo pichani) kama wana mipango gani kuhakikisha kuwa kutakuwepo na masafa ya kutosha kwa miaka mingi ijayo kwaajili ya wananchi wa vijijini na wale wasio na uwezo.


Picha ya pamoja.


Maxence Melo kutoka Jamii Forum akizungumza na waandishi wa habari wakati wa jukwaa lililowakutanisha kwa pamoja wadau wa masuala ya mitandao ya intaneti.


Maxence Melo kutoka Jamii Forum (katikati) akipata picha ya pamoja na wajumbe wa Tanzania Bloggers Network (TBN), Fredy Njeje wa Blog za Mikoa (kulia) na Mr. Verbs.




Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...