Skip to main content

WANAWAKE WA MKOA WA IRINGA WAPATIWA MAFUNZO JUU YA SHERIA YA UMILIKI WA ARDHI NA UONGOZI


Darasa likiendelea

Wanawake wa wilaya za Iringa, Mufindi na Kilolo mkoani Iringa wapatiwa mafunzo juu ya ushawishi na utetezi wa haki za wanawake na sheria ya umiliki wa ardhi ya mwaka 1999.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Shirika la Land O'Lakes chini ya ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID). 

Mratibu Msaidizi wa Programu wa Shirika la Land O’Lakes Tanzania, Mary Kafanabo alisema kuwa mafunzo hayo yametolewa kufuatia uelewa mdogo wa sheria za umiliki wa ardhi na sheria ya ardhi kwa ujumla.

Alisema kuwa wanawake wengi nchini wana uelewa mdogo wa sheria za umiliki wa ardhi na sheria ya ardhi, ndio maana shirika hilo likaona umuhimu wakuwapatia mafunzo wanawake ambao ni wazalishaji wakubwa katika kilimo na masuala mengine ya kijamii.

Katika warsha hiyo wawezeshaji kutoka chama cha wanasheria wanawake (TAWLA) ambao ni Latifa Ayubu na Francisca Gasper walitoa mada kuhusu haki za wanawake katika kumiliki ardhi Tanzania.

Walisema kuwa serikali kupitia wizara ya maendeleo ya jamii na watoto ilitunga sera ya maendeleo ya wanawake na jinsia ya mwaka 1992.

Walisema kuwa serikali katika jitihada za kuwapa wananchi mwelekeo wa maendeleo ya wanawake na jinsia ili kuhakikisha kuwa sera, mipango na shughuli mbalimbali za maendeleo zinazingatia usawa wa jinsia.

Awali, Afisa Kilimo Msaidizi wa Wilaya ya Mufindi, Tinara Nyato wakati akifungua warsha hiyo kuhusu haki za wanawake katika kumiliki ardhi, aliwasihi wanawake kutumia elimu waliopata vizuri pamoja na kupeleka elimu walioipata kwa wanawake wenzao vijijini walikutoka.

Naye mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Jesca Chibwana kutoka Kijiji cha Igomaa, Kata ya Sadani waliyani Mufindi alisema kuwa baada ya kupata uelewa juu ya sheria ya umiliki wa ardhi atakuwa balozi mzuri wakuwaelimisha wanawake wenzake kijijini. 

Naye Mratibu wa Programu wa Shirika la Land O’Lakes Tanzania, Mary Kabelele alisema kuwa wanawake wengi wana uelewa mdogo kuhusu suala la umiliki wa ardhi ambapo wanadhani mwenye jukumu hilo ni mwanaume pekee.

Alisema kuwa wanawake walikuwa na dhana potofu kwamba kwa kuwa mwanaume ndio msimamizi wa familia, basi umiliki wa ardhi ni haki yake.

“Tunajivunia kwa sasa kuona walengwa wa mradi huu ambao ni wanawake na jamii kwa ujumla wameanza kupata muamko kupitia mafunzo haya na wataanza kudai haki zao, aliongeza Kabelele.

Wakati huohuo, Shirika la Land O'Lakes limewapatia wanawake 25 mafunzo kuhusu uongozi kwa wanawake na wasichana yaliyofanyika Ifunda wilayani Iringa, Mkoa wa Iringa.

Mafunzo hayo yalilenga kubainisha na kutambua mchango wa wananwake katika sekta mbalimbali, ili kuondoa fikra hasi juu na uwezo na mchango wa wananwake katika maendeleo.

Mratibu wa Programu wa Shirika la Land O’Lakes Tanzania, Mary Kabelele alisema kuwa kipimo cha uongozi ni kuona kiongozi anavyoweza kuhamasisha na kuleta ushawishi kwa watu na kufikia maendeleo yaliyotarajiwa.

“Wanawake wana nafasi na jukumu kubwa katika kuongoza mabadiliko kwa vile wanatumia muda mwingi na kuchangia kiasi kikubwa cha nguvu kazi katika kilimo na masuala mengine ya kijamii,” alisema.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...