Skip to main content

ASKARI WA KIKOSI CHA UPELELEZI AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI SHINGONI

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?view=att&th=150bdff8c446975b&attid=0.1&disp=inline&realattid=file0&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ_joySY0ohOhzwcnrrpp7U7iluESV3i8d4MV5-jIC5JtSYWT0605cQkDqR9T0FcZRtt4ycxzHRS27j4XtDq8XwxlO65rJpgWbSay6_iHnNEg8oy8WaZDsTe9Q-z3RZ7tYUCuWK2gJrqYVCZRzifcn15kGyOxWFe0jig8YkW9TJEvuqTHP7nfFyLC4GHRWWV499nP7pfS4mXZDWbcGbF1TjUixB3wXxOVY38Zag6iVurwHG8Mq__7ZwdpTXm-lAEnMzzcF9FEStXPYfLeaoj_RXht-_EroaBGCJZQhzDIfAPPQEf6OaLhzlmilhgZdWKZ68e4WFdmG3ZkXhM1AxIDkJmnEltc1cxnMY4YXvuCYEg1MPtj8ZyjJHkETDVmU7uQqVJQsB0NQ3VLGHLYuay2_t50R0QNlq5upoZ_DGvuOuz7wSpG5UAdttt5lQ_7dMtrcFN_quIiZFjwf3eJKGRTXsJrgwQimR5iID6Ko1OR4RRfaAg0hAPZkN8rrmbUDiIhSC9deguKOEqQ6TJNsp1gXdiKoCI0hIJAtRp79E62vv6DuO4qx014graBOpJVyP1Y_BUDV3VaOWm5zaWum6aEvV5omACCBWcunslLySQTqexpZUzTUYiZLZBcf4

 
Askari wa kikosi maalumu cha kupambana na ujambazi mkoa wa Iringa Pascal Shila (30) pichani amejiua kwa kujipiga risasi kichwani kutokana na msongo wa mawazo.

Askari mwenye namba G.343D/C Pashal James Shila wa Ofisi ya RCO-Kikosi cha Anti Robbery amejiua kwa kujipiga risasi na mwili wake kukutwa kwenye jengo bovu la ghorofa la mjerumani lilipo nyuma ya kituo cha polisi.

Akizungumza na SIMBAYABLOG wakati wa kuaga mwili wa marehemu kwenye kituo kikuu cha polisi Manispaa ya Iringa, Kamanda wa polisi mkoa wa Iringa Ramadhani Mungi alisema tukio hilo lilitokea jana kati ya saa tisa na kumi jioni.

Kamanda Mungi alisema askari huyo kutoka ofisi ya upelelezi mkoa wa Iringa (RCO) alichukua silaha aina ya ya SMG saa sita mchana kutoka kwenye ghala ya kuhifadhia silaha kwa madai kuwa yeye na wenzake wanakwenda kufanya kazi ya dharura huko Ifunda.

Alisema baada ya hapo hakuonekana na saa saba mkewe alikwenda kwenye ofisi ya RCO kupeleka ujumbe alioandikiwa na mumewe kuwa amtunzie watoto kwa kuwa anawapenda sana.

Kamanda Mungi alisema kufuatia ujumbe huo askari wenzake walianza kumtafuta na baadaye kukuta mwili wake ukiwa kwenye jengo lililopo nyumba ya kituo kikuu cha polisi akiwa amejipiga risasi shingoni karibu na kidevuni na kabla hap alimtumia mkwewe meseji aliomba amtunzie watoto wake kwani ana wapenda sana.

Alisema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi ili kuweza kubaini
chanzo cha tukio hilo na kuwa huenda limesababishwa na msongo wa mawazo aliokuwa nao marehemu.

Alisema tukio hilo limewaumiza askari sote kwa kuwa alikuwa anachukia uhalifu kwa dhati na kuwa mwili wake utasafirishwa kesho kwenda nyumbani kwao wilayani Kyela katika kijiji cha Ilolo kwa ajili ya mazishi.

Aidha alisema matukio kama hayo yanawakuta askari kwa kuwa nao ni sehemu ya jamii na kuwa jeshi la polisi hutoa mafunzo ya jinsi ya kupambana na msongo wa mawazo kwa askari wao.

Hata hivyo habari ambazo hazijathibitishwa na kamanda wa jeshi la
polisi mkoa wa Iringa zinaeleza kuwa chanzo cha msongo wa mawazo.

Uchunguzi awali unaonyesha kuwa kulikuwepo na ugomvi baina yake na mkewe usiku jana.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...