Skip to main content

COSATO CHUMI AKERWA PROGANDA CHAFU ZINAZOFANYWA NA MPINZANI WAKE!

Mgombea ubunge Jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi (CCM) (katikati) akielezea masikitiko yake kuhusu kutoridhishwa na kampeni na propaganda chafu zinazofanywa na mgombea mwenzangu wa Chadema kwa waandsihi wa habari jana. Kushoto ni Meneja wa Kampeni -Jimbo la Mafinga mjini Albert Chalamira na Katibu Msaidizi wa CCM Wilaya ya Mufindi, Nuru Ngeleja (kulia)


Baadhi ya wanahabari wakifuatilia mkutano huo wa mgombea na waandishi wa habari katika ofisi za chama mjini Mafinga jana

Meneja wa Kampeni -Jimbo la Mafinga mjini Albert Chalamira (katikati) akielezea hali kampeni katika jimbo hilo kwa wanahabari ambapo alisema kuwa CCM inauhakika wa kushinda uchaguzi kwa asilimia 80.

Mgombea ubunge Jimbo la Mafinga Mjini Cosato Chumi (CCM) akionesha waraka wa kampeni chafu zinazodaiwa kumuzoofisha iliyopewa jina MKAKATI WA USHINDI JIMBO LA MAFINGA MIJINI kwa wanahabari. (PICHA ZOTE NA FRIDAY SIMBAYA)

Mgombea ubunge Jimbo la Mafinga Mjini, Cosato Chumi (CCM) amesema ni jambo la aibu, kusikitisha na hata kusononesha kuona kuwa katika wakati huu ambao taifa linaendea kukua na kukomaa katika siasa za vyama vingi na demokrasia ya uwazi na uwajibikaji kuna wanasiasa ndani ya jimbo wanashindwa kufanya siasa za kistaarabu.

Alisema kuwa wapo wanasiasa wanaofanya siasa za maji taka badala ya kuelezea sera, mipango na vipaumbele vya namna gani watakavyolinyanyua Jimbo la Mafinga mjini na badala yake wanaendeleza mbinu chafu za kupakana matope.

Mgombea huyu alisema kuwa hivi karibuni, timu ya kampeni imegundua na kubaini kuwa mgombea mwenzake William Mungai (Chadema) ameadaa waraka wa kurasa nne uliojaa tuhuma na uzushi dhidi ya wagombea wa CCM, kuanzia mbunge, madiwani na mgombea urais.

Kwa mfano, wamekubaliana kupitia waraka huo kuwaaminisha vijana wa bodaboda na bajaji kuwa akichaguliwa atafuta bodaboda, bajaji, atafuta mnada na atawatimua akina mama wauza matunda na mbogamboga.

Pia atawatimua vijana wauza mahindi kandokakdo ya barabara kuu. 

Hata hivyo, alisema kuwa huo ni uzushi mkubwa sasa na kumalizia kwa kutumia msemo wa kiswahili 'kuwa mfa maji hakosi kutapatapa' Usikose kusoma Nipashe kesho!





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...