Skip to main content

Jesca: Siwezi kujiuzulu kwa shinikizo la majungu, fitina na vikundi vya uasi...

Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu akizungumza na waandishi wa habari jana. 



Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu amesema hawezi kujiuzulu nafasi yake hiyo kwa shinikizo linalotokana na majungu, fitina na vikundi vya uasi vinavyoanzishwa ndani ya chama kwa lengo la kulinda maslai ya watu fulani.

“Hizi ni hoja zisizo na mashiko, hivi inawezekaneje mimi na hao wengine wanaowataja katika kipindi chote cha kampeni tufanye kazi ya kukihujumu chama, tuvumiliwe tuendelee na kazi hiyo, halafu tuhuma hizo zije zitolewe sasa baada ya kushindwa uchaguzi?” alisema.

Kwa kutumia vikao na taratibu zingine za katiba yake, CCM inapaswa kukaa chini na kufanya tathmini ya kina ili kujua sababu zilizopelekea wakapoteza jimbo na kata hizo.

Wanachama hao wanawatuhumu viongozi hao kuwahujumu katika Uchaguzi Mkuu wa mbunge, madiwani na rais hali iliyosababisha kipoteze jimbo hilo na halmashauri baada ya kupoteza kata 14 kati ya 18. 

Hivi karibuni, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Iringa Mjini, Ahamed Sawa alimtangaza Mchungaji Peter Msigwa aliyewania ubunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa mshindi baada ya kuzoa kura 43,154 dhidi ya kura 32,406 alizopata mgombea wa CCM Frederick Mwakalebela. 

Wagombea wengine na kura zao kwenye mabano ni Chiku Abwao wa ACT Wazalendo (411), Daudi Masasi wa ADC (123), Paulina Mgimwa wa Chausta (66) na Robert Kisinini wa DP (56). 

Wakiongea kwa kupokezana na bila kutaja majina yao wanachama hao waliokuwa wamebeba mabango yaliyowataka viongozi hao kuachia ngazi, walisema wanao ushahidi unaodhihirisha jinsi viongozi hao walivyofanya kazi iliyosababisha wapoteze jimbo, kata 14 na mgombea wao urais, Dk John Pombe Magufuli kupata kura 36,584 dhidi ya kura 38,860 alizopata mgombea urais wa UKAWA, Edward Lowassa. 

Katibu wa CCM Iringa Mjini, Elisha Mwampashi aliwataka wanachama hao kutumia vikao vyao vya kikatiba kuwasilisha malalamiko yao dhidi ya viongozi hao. 

“Tumieni vikao vya tawi na kata kuwasilisha ushahidi wenu na pale mtakahisi kuwepo kwa dalili za kuhujumiwa, leteni ushahidi wenu moja kwa moja kwangu ili tuuwasilishe kunakohusika haraka iwezekanavyo,” alisema.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...