Skip to main content

KINGUNGE NGOMBALE MWIRU ATANGAZA KUACHANA NA CCM RASMI





Anasema kamati kuu haiwezi kusema watu watano au sita ni hawa bila kuwasikiliza, kilichotokea mwaka huu ni tofauti kabisa kilichotokea mwaka 1995, safari mwenyekiti ni Jakaya Kikwete, kilichotokea ni jambo kubwa katika historia yetu na mimi katika historia yangu pale ambapo naona kwamba katiba inavunjwa nimekuwa na tabia ya kusema waziwazi na kuwaambia wenzangu si sawa.

Mwaka 1972 nikiwa mkuu wa mkoa Simiyu, kulikuwa na Bunge Dar es Salaam, nikakuta kuna mswada wa kurekebisha katika kuhusiana na swala la wakuu wa mikoa. Mchango wangu uliibua hisia kali na kumwambia mwenyekiti muswada aurudishe maana hatuukubali, kwa upande wa watu walipo serikalini walisema ndio na wabunge wa kuchaguliwa walisema hapana.

Ilipofika zamu yangu nikasema sina upande, wabunge walifurahi sana. Kura zilipohesabiwa serikali ilishindwa kwa mara ya kwanza katika mfumo wa serikali ya chama kimoja. Mzee Kawawa aliniita akasema wewe ni mwenzetu lakini umetuacha, Rais atakubadilisha kazi.

Nilipoitwa na mwalimu nilimueleza kwa nini nilikataa na akasema ningekuwa katika nafasi yako ningepinga lakini mimi ndio naongoza nchi lakini usiwe na wasiwasi. Tukakubaliana na siku ya pili nikatangazwa nimeachishwa uwaziri. Nilifanya uamuzi ule nikijua kabisa naweza kupoteza kazi lakini kwenye masula ya kimsingi huwa sitetereki.

Mimi sikubaliani na mambo yaliyotokea tarehe kumi na kumi na moja Dodoma, kilichotokea ni kuwadhalilisha wagombea wenye haki, kamati kuu ingeweza kuwahoji na kuamua. Hili halikfanyika. wadhalilishwa, wamezungushwa mikoa 15 kwa gharama zao na kuishia mlangoni mwa kamati kuu.

CCM inaamini binadamu wote ni sawa na kila mtu anastahili heshma ya kutambuliwa utu wake, kuwazungusha alafu nyinyi mmefunga mlango, si kuwadhalilisha? Katika nchi yetu hao waliodhalilishwa wamenyamaza moja kwa moja isipokuwa Mwandosya, aliinuka na kusema kwamba kweli wamedhalilishwa na kadhalika.

Nawapongeza Kimbisa, Sophia na Nchimbi kwa kueleza yaliyotokea kamati kuu, tuliingia chama hiki si kwa ajili ya kutafuta cheo na wengine tuliacha kazi kwa mkoloni. Tulitafuta chombo cha ukombozi kwa watanzania na waafrika.

Kwa kuwa uongozi wa sasa wa chama cha mapinduzi kufanya yale wanayotaka wao kwa maslahi ambayo sina hakika ni ya nani, vijana wanatumiwa kudhalilisha watu wazima, watu wanaajiriwa kutukana tu watu, mimi nasema sikubaliani na hiko sio chama tulichoshirikiana kukijenga.

Mimi kuanzia leo naachana na chama cha mapinduzi kwa sababu siwezi kuhimili chama kinachoendeshwa bila kuheshimu katiba kwa sababu katiba ndio inayotuunganisha sisi sote. Sasa nasema kuanzia sasa najitoa chama cha mapinduzi, najua uamuzi wangu utasumbua baadhi ya rafiki zangu, makada wenzangu na wazee wenzangu hata vijana lakini ni uamuzi ambao lazima niufanye kwa sababu vinginevyo mimi nitajisaliti mwenyewe.

Nimehusika kuweka misingi ya chama chetu, ndani ya chama chetu kumekuwa na demokrasia halafu wakuu wanakwenda kutangaza kwenye majukwaa hakukuwa na tatizo lolote, mambo yote yalikuwa sawasawa.

Sikusudii kujiunga na chama kingine chochote na nina sababu, mimi nimekuwa mwanaharakati wa TANU na CCM kwa muda wa miaka 61, nadhani miaka 61 inatosha mimi kuwa mwanaharakati.

Tatu mimi ni raia tena raia huru wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, nna haki zangu za kisisasa na kijamii hivyo nitaendelea misimamo yangu.

Katika hali ya sasa ina makundi mawili, moja linasema kidumu chama tawala maana yake hakuna mabadiliko. Kundi jingine linasema linataka mabadiliko katika nchi yetu, sitaki kusema kundi lipi kubwa lakini nasema hali iko hivyo, kwa jinsi nnavyotazama vijana wanataka mabadiliko ukiondoa vijana wangu wa UVCCM, kina mama walio wengi wanataka mabadiliko, wafanyakazi wakulima, wafugaji, wavuvi, wachimba migodi wadogowadogo najua wengi wao wanataka mabadiliko, wanafunzi hasa wa sekondari ya juu, wa vyuo na vyo vikuu na wasomi wa nchii walio wengi wanataka mabadiliko.

Nilisema siku moja nilipoulizwa nani unamuona anafaa kugombea Urais, niliwaambia kwamba mimi nitamuunga mkono yule ambae ziko dalili zote wananchi wanasema ndie anaefaa. Pia nilisema nilipokuwa na ndugu Lowassa Arusha, Mwalimu alisema ulizeni wananchi wanasema nini?

Katika hili swala la mabadiliko mimi niko upande wa mabadiliko tena mimi nasema wamechelewa, walio wengi wanataka mabadiliko. Mimi nasema niko upande wa mabadiliko kwa sababu ya wale. Katika historia yetu katika TANU na Afro shirazi sisi tulikuwa upande wa mabadiliko.

Tuliungana na hio ilikuwa mabadiliko, mwaka 77 tuliua Afro Shirazi, tuliua TANU na kufanya mabadiliko. 
Baada ya kukaa madaraki miaka mingi hatuwezi kuleta jipya pamoja na ahadi za Magufuli, nusu karne ni muda mrefu sana, pumzi, kuongoza nchi na kama kupanda mlima, unafika mahala pumzi zinakwisha, huwezi kuendelea mbele na ukitaka kuendelea wananchi wanabaki palepale walipo.

Tatizo la wananchi ni uchumi, ajira, sasa umasikini unaondolewa na uchumi imara.

Mkapa alitufanyia kazi nzuri kwa kututoa kwenye ukuaji wa asilimia 3 mpaka 4, wakati anakabidhi madaraka ulikuwa unakuwa kwa 7%. Kikwete amepokea madaraka unakuwa kwa 7%, sasa miaka kumi baadae uchumi unakuwa kwa 7%. Maana yake miaka kumi hii tumepiga maktaimu, tumebaki palepale maana yake ni kurudi nyuma.

Idadi ya watu imeongezeka, midomo imeongeza, miguu imeongezeka lakini ukuaji uko palepale, bei ya sukari kwa mfano ni ya kuruka, bei ya sukari Mkapa aliacha 600 sasa inaenda 2000. Nini! Pumzi. Kwenda kwenye maisha bora kunataka pumzi.

Tulianza na maisha bora kwa kila mtanzania lakini sasa hatusemi tena habari hizo, mabadiliko ni muhimu kwelikweli, tupate pumzi mpya. Mnataka mbaki nyinyi tu, nyinyi pumzi imekwisha. Chama kifutike? Hapana lakini kiwekwe benchi kidogo kijitafakari.

Kama hamjadili mambo mtapata wapi mawazo ya kwenda mbele, lazima ukuaji wa uchumi wa nchi angalau ufike 10%. 7% mpaka 10% si mbali lakini miaka kumi tuko palepale. Wachina wamekuwa wakikuza uchumi wao mpaka asilimia 15 na zaidi, na sisi hapa baadhi yetu kama watu watakuwa wanyenyekevu kupata mawazo ya wenzao tutapiga hatua.

Mimi nimekuwa mwenyekiti wa ilani zote za uchaguzi kasoro moja tangu mwaka 90, tatizo la ajiri kwa vijana linaonekana kana kwamba halitatuliki wakati linatatulika, kujiajiri na kutoa mitaji. Wanaotaka kujidanganya kwamba wataleta mabadiliko haya! 

Lakini tunaotaka kwenda mbele, kung'ang'ania kwamba lazima wao wawe madarakani mtakuja kujilaumu wenyewe siku moja. Asanteni sana kwa kunisikiliza.

SWALI(Mayage): Kama CCM mngemteua Lowassa, ungayasema hayo ya kusema unataka mabadiliko?

Jibu: Mimi wakati wote nimekuwa nina matumaini kwamba ndani ya CCM tunaweza kupata watu wanaoweza kubadili hali ndio maana niliamua kupambana ndani ya chama changu tukaenda mbio kuliko hivi ili hali ya wananchi ibadilike. Mimi nikamuona Edward Lowassa kwa jinsi ninavyomjua, si mtu mgeni katika nchi hii, nikasema tukimpata nchi itakwenda mbio zaidi.

Niliwahi kuzungumza kwanini nilisimama sambamba na Edward Lowassa kule Arusha, nikasema Edward ana sifa kuliko wengi niliowaona, kiongozi lazima akubalike na watu na hii ni principle ya watu tangu TANU, Lowassa anakubalika pamoja kupakaziwa mambo ya ajabu.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...