Skip to main content

KUJISAIDIA PORINI KWA WASAFIRI SASA BASI...!

Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali akikagua ujenzi wa mradi.

Dkt Mohamed Gharib Bilali (Picha na Friday Simbaya)

Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali amesema tabia ya kujisaidia porini kwa wasafiri kama wanyama kwa lugha maarufu ya “kuchimba dawa,” sasa basi, baada ya kuweka jiwe la msingi mradi wa vituo vya mapumziko na vyoo kwa wasafiri katika barabara kuu nchini.

Alisema kuwa kwa muda mrefu abiria wanaosafiri katika barabara kuu, wamekuwa wakipata taabu pindi wanapohitaji sehemu za faragha.

Dkt Bilali alisema hayo katika hafla fupi ya kuweka jiwe la msingi mradi wa vituo vya mapumziko na vyoo kwa wasafiri katika barabara kuu nchini iliyofanyika katika Kijiji cha Idetero wilayani Mufindi, mkoani Iringa jana.

Mradi wa vituo vya mapumziko na vyoo kwa wasafiri katika barabara kuu nchini unakusudia kujenga vituo vya mapumziko kwa wasafiri 44 nchi nzima katika barabara kuu zote nchini.

“Jambo hili limefikia katika hatua mbaya hata kukiuka ustaarabu wa binadamu kwa kujisaidia porini kama wanayama. Tabia hii si ya ustaarabu inadhalilisha utu wetu…,” alielezia Dkt Bilali.

Alisema kuwa katika karne ya leo si ya kuendelea “kuchimba dawa” na kuipongeza taassi ya Mufindi Environmental Trust (MUET) kwa kushirikiana JKT kubuni mradi wa kujenga vituo vya mapunziko na vyoo kwa wasafiri katika barabara kuu nchini.

Aliongeza kuwa hatua ya MUET kubuni jambo hili inastahili pongezi na kuungwa mkono na wadau wote ili kuhakikisha malengo yake yantimia kwa kujenga vituo hivyo.

Shirika la MUET tangu kuanzishwa kwake, limefanya mambo mengi, ikiwa ni pamoja na; kuhamasisha upandaji miti kwa watu binafsi, kampuni, taasis za dini na serikali, kuboresha vyanzo vya maji, kutoa elimu ya kuzuia uchomaji misitu na kutoa elimu juu ya ugonjwa wa UKIMWI.

Aidha, Dkt. Bilali alisema kuwa ili kujenga nchi yetu,tunahitaji watu wenye afya bora. Moja ya mambo muhimu katika kuboresha afya za watu ni suala zima la usafi pamoja na kutunza mazingira kwa ujumla.

Alisema kuwa hatuwezi kuzungumzia usafi katika mazingira tunayoishi bila kutaja suala la vyoo.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya nne na zilizotangulia, imefanya jitihada kubwa kuimarisha sekta ya miundombinu ya barabara nchini ambapo karibu mikoa yote nchini imeunganishwa kwa barabara ya lami.

“Natoa rai kwa wadau na mashirika mbalimbali nchini kuiga jambo jili jema na kusaidia shughuli hii muhimu. Barabara za nchi yetu ni nyingi na maeneo ni mapana, hivyo kwa taasis moja peke yake kufanya jambo hili ni kazi ngumu,” alisema Dkt. Bilali.

Aidha, aliwashukuru pia wadau mbalimbali waliojitokeza kuunga mkono jitihada hizo za ujenzi wa vituo vya mapumziko na vyoo. 

Wadau hao ni pamoja na serikali ya china, jeshi la wananchi wa Tanzania, kumpuni ya simu za mikononi ya Airtel, Mustafa Sabodo, Mufindi Tea Companya, MUCOBA Bank, PSPF na TANESCO.

Wakati huohuo, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali aliwakumbusha watanzania wote kwamba oktoba 25 mwaka huu ni siku muhimu katika historia ya taifa.

Alisema kuwa ni siku ambayo tunaenda kupiga kura ya kuchgua viongozi katika ngazi mbalimbali.

Alitoa wito kwa watanzania wote kujitikeza kwa wengi na kutumia haki yao ya kidemeokrasia kwa kuchagua viongozi wanaowapenda.

“Tukumbe kwamba viongozi tutakaowachagua ndio watakuwa dira ya nchi yetu katika kipindi cha miaka mitano ijayo,” alisema Dkt Bilali.



mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...