Skip to main content

Masenza: Orodha ya vituo imepungua toka 1,641 hadi 1,601


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza amesema orodha ya vituo imepungua kutoka 1,641 hadi kufikia 1,601, sawa sawa na vituo 40 vilivyopungua, Nipashe imedhibitisha.

Alisema kuwa awali Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitoa orodha ya vituo 1,641 vitakavyotumika katika zoezi la upigaji kura kwa Mkoa wa Iringa kwa Halmashauri zote tano (5). 

Masenza alisema hayo wiki iliyopita wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu mwenendo wa maandalizi ya uchaguzi mkuu wa rais, wabunge na madiwani. 

Alisema kuwa idadi hiyo imepungua kufikia vituo 1,601 baada ya uhakiki wa wapiga kura kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura unaoendelea kufanywa na Wasimamizi wa Uchaguzi.

Alisema kuwa halmashauri zote zimepokea vifaa kama masanduku, mifuniko, Tshirts, kofia, Vituturi, na fomu mbalimbali kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu. 

Aidha, alisema kuwa wasimamizi wanaendelea kufanya tathmini ili kujiridhisha endapo vifaa vilivyopokelewa vinakidhi mahitaji.

“Tayari Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetoa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa Halmashauri zote. Kazi inayoendelea hivi sasa ni uhakiki wa idadi ya wapiga kura kwa kila kituo,” alisema Masenza.

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema kuwa mkoa wake umejipanga vizuri kuhakikisha amani na usalama kwa kipindi chote cha kampeni za Uchaguzi na wakati wa zoezi la kupiga kura vyote vinafanyika vizuri kwa mujibu wa ratiba na kwa kuzingatia sheria za nchi ili Wananchi waendelee kuwa salama na kutekeleza majukumu yao. 

Alisema kuwa katika kuhakikisha mkoa unakuwa na utulivu kwa kipindi chote, amekutana na makundi mbalimbali kujadili suala la amani kuelekea Uchaguzi Mkuu. 

Makundi hayo ni viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa madhehebu ya dini, wazee na watu wenye ushawishi katika jamii na waandishi wa habari. 

Lengo ni kupata maoni na ushauri wa jinsi ya kufanikisha Uchaguzi Mkuu kwa amani na utulivu.

“Napenda kuchukua nafasi hii kuwathibitishia Wananchi wa Mkoa wa Irirnga kuwa, ulinzi utakuwepo wa kutosha katika kipindi chote cha kampeni na siku ya kupiga kura tarehe 25/10/2015,” alisema. 

Alisema kuwa Jeshi la Polisi limejipanga vizuri kuwalinda wananchi wote, hivyo, rai yake kwa wananchi ni kuwa jitokezeni kwa wingi siku ya kupiga kura mapema na baada ya kupiga kura rudini kwenye maeneo yenu kuendelea na shughuli nyingine. 

“Wananchi wasibaki kwenye vituo vya kupigia kura baada ya kupiga kura”.

Napenda kutoa rai kwa wananchi wote wa Mkoa wa Iringa kufahamu na kukubaliana kuwa yapo maisha na yataendelea kuwepo hata baada ya Uchaguzi Mkuu hapo tarehe 25 Oktoba, 2015. 

Hivyo, kila mmoja wetu lazima atimize wajibu wake katika kuhakikisha amani na utulivu vinaendelea kuwepo katika kipindi hiki chote ili tumalize zoezi hili tukiwa wamoja na wenye mshikamano mkubwa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...