Skip to main content

Mshauri:Jukwaa la wafugaji na wakulima lapunguza migogoro...


Afisa Tarafa ya Pawaga, Nasson Mwaulesi  (Picha na Friday Simbaya)


OFISA Ardhi na Maliasli wa Wilaya ya Iringa, Donald Mshauri amepongeza Jumuiko la Maliasili Tanzania (TNRF) kwa kuanzisha Jukwaa la wakulima na wafugaji wa tarafa la Pawaga linaloshughulikia migogoro baina ya makundi hayo.


Mshauri alisema hayo jana wakati wa mkutano wa wadau wa masuala ya ardhi katika Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa uliyoandaliwa na Jumuiko la Maliasili Tanzania.


Alisema kuwa kuanzishwa kwa jukwaa hilo kumepunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji katika Tarafa ya Pawaga tatizo ambalo limekuwepo muda sasa.


Alisema kuwa zipo sababu zilizopelekea migogoro ya ardhi katika wilaya yake, zikiwemo ongezeko la mifugo na ongezeko la wahamiaji kutoka wilaya zingine kuja Pawaga.


“Wafugaji wamekuwa wakiishi nyanda kame zisizo na maji na malisho ya kutosha wakati wakulima wakiishi mabondeni ambako kuna maji na shughuli za kilimo kufanyika…,” alielezea ofisa ardhi na maliasili huyo.


Mshauri alisema kuwa mambo hayo huchochewa na kukosekana kwa taratibu na mazingira rafiki yanayowezesha wafugaji kunufaika na rasilimamali zinazopatikana mabodeni.


Naye, Mratibu wa Mradi wa Ardhi Jumuiko la Maliasili Tanzania (TNRF), Godfrey Massey alisema kuwa TNRF imeunda Jukwaa la wakulima na wafugaji wa tarafa ya Pawaga kwa lengo la kuwaleta pamoja ili wajadili chanagmoto zinazowakumba na kutafuta namna yakukabilianazo kwa pamoja.


Alisema kuwa mradi huo umetoa mafunzo ya haki za ardhi na utwala vijijini kwa wanavijiji na viongozi wa vijiji vinne katika tarafa ya Pawaga ambapo wanavijiji 200 na viongozi 200 wamepatiwa mafunzo.


Massey alisema kuwa vijiji hivyo ni Itunudu, Mbolimboli, Kisanga na Isele pamoja na kutoa mafunzo kwa waangalizi nane, wawili kila kijiji kwa kuzingatia jinsia walipatiwa mafunzo zaidi ili waendelea kuwa walimu na washauri wa masuala ya ardhi katika vijiji vyao.


Hata hivyo, hivi karibuni TNRF ilifanya mafunzo ya hadhara juu ya haki za ardhi na utawala vijijini na kutoa msaada wa sheria kwa wanajiji katika vijiji vitatu katika tarafa ya Pawaga.


Vijiji hivyo ni Mkumbwanyi, Magombwe na Mkombilenga ambapo jumla ya wanavijiji 334 kati yao wanaume 215 na wanawake 119 walinufaika na mafunzo hayo.


Wakati huohuo, Afisa Tarafa ya Pawaga, Nasson Mwaulesi aiitisha kikao na watumishi wote wa serikali wanaofanya kazi ndani ya tarafa hiyo kwa kuwakumbusha kuhusu uwajibikaji kazini kila mmoja kwa nafasi yake.


Afisa tarafa huyo pamoja na mambo mengine aliwatabulisha watumishi wapya ili wafahamiane na kuwaasa watumishi kuwa na maadili mema katika kuishi na jamii.


Mwaulesi alisema kuwa watumishi wanatakiwa kuwa na kikao na afisa tarafa kila baada ya miezi mitatu na kuwaonya watumishi hao kutojihusisha na masuala ya siasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.


Alisema kuwa watumishi hao wanatakiwa kuzingatia maadili mema katika kuishi na jamii, kujipenda pamoja na unadhifu. 


Kikao hicho kulihudhuriwa na watendaji wa kata, walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari, waratibu elimu kata, maofisa ugani, maofisa maendeleo ya jamii na ofisa umwagiliaji wa tarafa.


Wengine waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na polisi tarafa ya Pawaga, mkuu wa gereza la Pawaga, mkuu wa kituo cha afya Kimende-Pawaga na hakimu wa mahakama ya mwanzo Pawaga.


Mwisho.





















Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...