Skip to main content

RIPOTI MAALUM: MABADILIKO YA TABIANCHI YAATHIRI VISIWA VYA MAFIA NCHINI TANZANIA



Moja ya eneo lililoaribika kutokana na hali ya mabadiliko ya tabianchi (Climate Change) katika fukwe ya Kilindoni, katika Kisiwa cha Mafia, Mkoani Pwani, nchini Tanzania. (Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog).


Na Andrew Chale

[MAFIA-ISLAND] Kisiwa cha Mafia kijografia kipo karibu na mlango wa Mto Rufiji kusini mwa Tanzania.

Hata hivyo, Kisiwa hichi ambacho ni Wilaya moja wapo ya Mkoa wa Pwani inakabiriwa kwa kiwango kikubwa na changamoto za Mabadiliko ya tabianchi hasa baada ya wananchi wake wengi kutopata elimu hiyo sahihi.

Imeelezwa kuwa, elimu juu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi katika Kisiwa cha Mafia ambacho pia kinaunda visiwa vidogovidogo zaidi ya vitano, wananchi walio wengi katika kisiwa hicho bado hawajapata elimu sahihi ya kukabiliana na mabadiliko ya kimazingira (Climate Change).

Mtandao huu ambao ulipiga hodi katika kisiwa hicho cha Mafia ili kupata habari za mabadiliko ya tabianchi na namna ya Mabadiliko ya tabianchi yanavyo athiri Kisiwa hicho (How Climate Change effects Mafia Island in Tanzania) ambapo iliweza kuzungumza na maafisa Ardhi, Mazingira na wananchi wa Wilaya hiyo, na kueleza haya:

Kwa upande wa Afisa Mazingira wa Wilaya hiyo, Gideon Zakayo (pichani juu) amebainisha kuwa, Kisiwa cha Mafia kinakabiliwa na changamoto mbalimbali za Kimazingira ikiwemo hali ya Mabadiliko ya tabianchi huku suala la elimu kwa wananchi likiwa dogo kutokana na kutokuwa na fungu la kutosha.

“Kwa sasa bado hatuna fungu la kutosha kuwafikia wananchi na kutoa elimu ya Mabadiliko ya tabianchi. Ila bado milango ipo wazi kwa mashirika na taasisi binafsi kufika na kutoa elimu hiyo kwa sasa” anasema Zakayo.

Zakayo ameongeza kuwa, Suala la Mazingira ni pana kwani limejumuisha Afya, Maji, Kilimo, Misitu, ardhi na mazingira yote kwa ujumla hivyo wadau wanahitajika kujitokeza kusaidiana na Serikali katika kutoa elimu, kuelimisha sera na taratibu zinazotakiwa kufuatwa na wananchi katika maeneo husika.

Aidha, ameongeza kuwa, katika miongoni mwa visiwa vidogo vidogo ndani ya Mafia, kuna baadhi ya visiwa vimeanza kuharibiwa kutokana na Mabadiliko ya tabianchi.

“Vipo visiwa baadhi tayari vimeanza kuathirika na mabadiliko hayo kwani maji yamekula ardhi. Pia baadhi ya maeneo maji yameweza kuingia katika ardhi na kubadilisha maeneo hayo tofauti na awali.” amebainisha Zakayo, Afisa Ardhi Wilaya ya Mafia.



Mahojiano na wananchi kisiwa cha Jibondo:

Modewjiblog imeweza kufanya mahojiano kadhaa na wananchi wa kisiwa cha Jibondo ambapo wameweza kueleza kuwa kisiwa hicho kimeanza kulika katika baadhi ya maeneo kwani kwa sasa maji yameweza kuingia katika ardhi.

Kwa mujibu wa wakazi wa Jibondo ambapo maana ya jina hilo ni jiwe kubwa na ndivyo kilivyo kisiwa hicho, kwani kipo juu ya mwamba mkubwa kwa sasa baadhi ya maeneo maji ya bahari yameingia baharini.

Zahoro Swed mkazi wa Jibondo amemweleza mwandishi wa habari hizi kuwa, awali katika eneo wanaposhushia vyombo vya usafiri lilikuwa mbali na majini, lakini sasa eneo hilo limemezwa na maji yamesogea zaidi.

“Wasiwasi wetu ni ujaaji wa maji. Zamani vyombo vyetu tulikuwa tunapaki eneo la nyuma kabisa, lakini sasa tunasogea hadi huku mbele haya ni mabadiliko na hali ikizidi hivi basi tutakuja kushuhudia maji yakiingia katika makazi ya watu” alibainisha Swed alipozungumza na Modewjiblog katika kisiwa hicho cha Jibondo.

Aidha, kwa upande wao baadhi ya wananchi wa eneo hilo la jibondo wamebainisha kuwa, kutokana na suala la uvuvi kushamiri wapo wavuvi wasio waaminifu wanaotumia mabomu kiasi cha kuharibu mazingira ya bahari hata kupelekea kisiwa hicho kupata matatizo ya maji kuingia kwenye ardhi.

Wakazi hao wameeleza kuwa, elimu ndogo ndio chanzo cha wavuvi hao kuendelea kutumia mabomu kufanya shughuli zao za uvuvi haramu ambapo mabomu hayo yanapelekea kisiwa hicho ambacho ni cha miamba ama jiwe (Mafiwe) kuathirika zaidi huku Mabadiliko ya tabianchi yakipata nafasi ya kuongeza uharibifu huo.



Kisiwa cha Chole:

Kwa upande wa wananchi wa kisiwa cha Chole ambacho ni kisiwa kidogo na ndio kisiwa chenye utalii na urithi wa kale ikiwemo magofu na majumba ya zamani, wananchi wengi wa kisiwa hicho wamelalamikia juu ya elimu ndogo ya Mazingira kutolewa licha ya kuihitaji mara kwa mara.

Wakazi hao wa kisiwa hicho walipaza sauti kwa kueleza kuwa, wengi wao wanajishughulisha na shughuli za baharini ikiwemo uvuvi na suala la kilimo cha mwani ambapo wamekuwa wakishuhudia matatizo ya kimazingira yanayotokea baharini mara kwa mara.

Swaumu Mohammed ambaye ni mkazi wa kisiwa hicho cha Chole anayefanya shughuli za kilimo cha zao la mwani anaeleza kuwa wamekuwa wakishuhudia mabadiliko kadhaa ndani ya bahari hiyo ikiwemo baadhi ya maeneo kuwa tofauti na awali.

“Maji yamekuwa yakiongezeka mara mbili zaidi. Wakati mwingine tunapofika kuvua mwani hapa kipindi cha nyuma maji yalikuwa ni ya kiasi, lakini kuna wakati hali hiyo inakuwa haipo kabisa na maji yanakuwa ni mengi zaidi na hata kutupa hofu.

Hivyo elimu zaidi inahitajika katika kujua mabadiliko ya tabianchi ni yapi na namna ya kujikinga nayo hasa sisi tunaoshinda baharini muda mrefu” alieleza Bi. Swaumu alipoulizwa kama anafahamu juu ya hali ya mabadiliko ya tabianchi ama .

Mbali na wananchi wa visiwa hivyo, kwa upande wa wananchi wa Kisiwa cha Bwejuu kwa upande wao wameonyesha wasiwasi wao kuwa baadhi ya maeneo yanayozunguka kisiwa hicho yamekuwa yakiliwa na maji kwa muda mrefu huku kukiwa hakuna juhudi za haraka kunusuru hali hiyo.

Wananchi hao wameonyeshwa kusikitishwa na kasi ya hali hiyo kwani imekuwa ikiongezeka mara kwa mara na hakuna hatua ya haraka iliyochukuliwa.

“Kwa kawaida ukiwa unatoka sehemu moja ama nyingine hali hii hutoiona kwa harakaharaka. Ila kwa sie tuliozoea ndio tunajua kama ardhi imeliwa na bahari” anaeleza mmoja wa wavuvi anayefanya shughuli zake katika eneo la kisiwa hicho aliyefahamika kwa jina la Salum Mwinyikame.

Aidha, Mwinyikame ameongeza kuwa, kisiwa hicho ambacho ni asili ya mchanga. Kimekuwa kikipata changomoto nyingi ya kimazingira huku akiomba mamlaka husika kufika na kutoa elimu hiyo ya mazingira.

Hata hivyo, Modewjiblog ilipowasiliana na viongozi wa Serikali wa Kisiwa hicho cha Mafia, wamebainisha kuwa, karibu visiwa vyote vinavyokaliwa na watu wamekuwa wakijitahidi kufikisha elimu mbalimbali huku akisisitiza wito wa wadau binafsi kujitokeza kusaidia na serikali katika swala hilo la utoaji wa elimu ya Mazingira na mabadiliko ya tabianchi hasa katika kukabiliana na majanga yatokanayo na masuala hayo.


Moja ya vyombo vya uvuvi na usafirishaji abiria vikiwa vimepaki katika fukwe za Kisiwa cha Chole huku vikisubiria maji kurejea katika eneo hilo kama vilivyokutwa na mwandishi wa makala haya. (Andrew Chale).



Pichani ni katika eneo la Fukwe za Wavuvi kama linavyoonekana lilivyoharibika kulikosababishwa na mabadiliko ya tabianchi. Kwa mujibu wa wakazi wa eneo hilo la Kilindoni wameeleza kuwa, miaka ya nyuma hapo palikuwa na minazi huku maji ya bahari yakiwa mbali, lakini kwa kadri mabadiliko yalivyotokea, eneo hilo limeweza kuliwa na kufanya minazi kupotea hali iliyosababisha kuweka mfereji/mto mdogo ambao unapitisha maji kutoka baharini na kuchanganyika na yale ya mvua ya kwenye makazi ya watu. (Picha na Andrew Chale)


Taswira ya kisiwa cha Chole kinavyoonekana..


Baadhi ya fukwe za kupendeza za kisiwani Mafia zinavyookena kwa picha hii iliyopigwa juu

eneo la Mafia.. 


Moja ya sehemu za eneo la Kisiwa cha Jibondo kama inavyoonekana pichani ambapo kisiwa hicho kipo juu ya mwamba ama jiwe kama inavyofahamika Jibondo ama jiwe kubwa. (Picha ya kwa hisani ya Mafia Island page ya fb).


Pichani Mwandishi wa Makala haya akiwa katika boto maalum kwa safari za visiwa vilivyo ndani ya Mafia ambavyo Kisiwa hicho kinakadiliwa kuwa na Visiwa vidogovidogo zaidi ya vitano. Picha ya chini Mwandishi akiwa katika Kibao cha Shule ya Kijiji cha Chole katika Kisiwa cha Chole ambacho ni kisiwa pekee chenye magofu ya Kale na vitu vya thamani vya enzi za zamani vikiwa vimehifadhiwa huko.


Kisiwa cha Chole


Moja ya visiwa vidogo na vya kuvutia ndani ya Kisiwa cha Mafia.






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...