Skip to main content

SALIM ASAS ALIA NA UTITIRI WA KODI


Mkurugenzi wa makampuni ya Asas, Salim Abri akisoma risala fupi kwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na  Uvuvi Dkt Titus Kamani hivi karibuni. (Picha na Friday Simbaya)


IRINGA: Mkurugenzi wa makampuni ya Asas, Salim Abri ameiomba serikali kuondoa kodi ya ongezeko la thamani (VAT) kwenye mazao ya maziwa ambayo ni siagi, jibini, samli, cream na maziwa yenye ladha za matunda.

Salim alitoa kilio hicho mbele ya Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Titus Kamani alipotembea kiwanda cha kusindika maziwa cha ASAS DAIRIES LTD mjini Iringa, mkoani Iringa kupitia mradi wa Uendelezaji Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki (EADD II).

Alisema kuwa kuondoa kodi hizo hakutaathiri sana pato la serikali kwa sababu sekta ya usindikaji wa maziwa nchini bado ni changa.

Alisema kuwa viwango vya kodi ni vikubwa na vingi kulinganisha na uwezo wa uzalishaji wa viwanda vya kusindika maziwa.

“Kwa ujumla mfumo mzima wa kodi unakwamisha mafanikio ya viwanda vya maziwa nchini,” alisema Salim.

Alisema bidhaa za maziwa toka nje ya nchi, zinauzwa kwa bei ndogo ukilinganisha na bidhaa za maziwa zinazosindikwa nchini.

Hii inatokana na ukweli kwamba wigo wa kodi hapa nchini ni mkubwa mno ukilinganisha na nchi nyingine,” aliongeza mkurugenzi.

Alisema kuwa kiwanda hakijafikia kiwango cha uzalishaji na kwa sasa kinazalisha lita 12,000 kwa siku na sababu kubwa wananchi wengi kutokuwa na tabia ya kunywa maziwa pamoja na kuwa viwango vikubwa vya kodi kama vile VAT.

Mradi wa Uendelezaji Sekta ya Maziwa Afrika Mashariki (East Africa Dairy Development) in mradi wa miaka mitano (2013-2018) unaotekelezwa kwa awamu ya pili katika nchi za Kenya, Uganda na Tanzania kwa kutumia mfumo wa kitovu cha maziwa (Dairy Hub). 

Nchini Tanzania mradi huu unatekelezwa katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe.

Mwisho









Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...