Skip to main content

UCHAGUZI KURUDIWA KATIKA KITUO CHA IPOGORO 'C' MJINI IRINGA








Mgombea Ubunge kupitia tiketi ya Chadema katika Jimbo la Iringa Mjini Mch. Peter Msigwa (juu ya gari) akiwatumiza mzuka wafuasi wake ili tume ya taifa ya uchaguzi (NEC) iendelee na mchakato wa kutangaza matokeo ambayo hata hivyo bado hajatangazwa.


CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Iringa Mjini kimeyapinga matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Madiwani, Ubunge na Rais jimbo la Iringa Mjini yanayoelekea kukipa ushindi mkubwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Matokeo hayo yameshindwa kutangazwa leo kama ilivyotarajiwa na wafuasi wengi wa chama hicho na wakazi wengine wa jimbo hilo baada ya kutokea wizi wa maboski mawili yaa kura katika kituo cha kupigia kura cha Ipogolo ‘C’, majira ya saa nne usiku, Oktoba 25.

Wakisubiri matokeo hayo leo, mamia ya wafuasi wa Chadema walikuwa wamejazana nje ya ofisi ya msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo Ahmed Sawa toka saa 12.00 asubuhi hadi 11.00 jioni walipotangaziwa kwamba matokeo hayo hayatatangazwa mpaka kesho wapiga kura wa kituo hicho watakaporudia uchaguzi huo.

Akitangaza uamuzi huo katika tukio lililokuwa na ulinzi mkali wa jeshi la Polisi pamoja na magari yake ya washawasha, Sawa alisema uchaguzi katika kituo hicho unarudiwa baada ya kutokea wizi huo na kwamba matokeo ya jumla yatatanngazwa baada ya marudio hayo kukamilika.

Awali Katibu wa CCM Iringa Mjini, Elisha Mwampashi alifanya mkutano na wanahabari na kuwaleza kwamba hawayatambui matokeo ya uchaguzi huo kwasababu ulikuwa na dosari ikiwemo ya wizi wa maboksi hayo ya kura.

Dosari nyingine kwa mujibu wa Mwampashi ni ushabiki wa wazi kwa wagombea wa Chadema uliooneshwa na baadhi ya wasimamizi wasaidizi katika vituo mbalimbali vya kupigia kura. 

Akizungumzia wizi wa maboksi ya kura katika kituo hicho, Mwampashi alisema majira ya saa nne usiku, baada ya zoezi la upigaji kura kukamilika, kituo hicho kilivamiwa na vijana waliokuwa wamevaa nguo zenye nembo ya Chadema, wakawatisha wasimamizi na mawakala wa kituo hicho na kutokomea na maboksi hayo.

“Kwa hiyo tumemuandikia barua msimamizi tukitaka uchaguzi huo jimbo zima urudiwe ili haki iweze kutendeka. Na wakati wa marudio hayo tunamtaka msimamizi kubadilisha wasimamizi wasaidizi wote kwa sababu waliotumiwa katika uchaguzi huo walionesha dalili ya kutokuwa waaminifu baada ya kuonekana wakishabikia wagombea wa Ukawa,” alisema.

Akizungumzia madai ya CCM, Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Iringa Mjini, Frank Nyalusi alisema; “madai ya CCM tumeyasikia baada ya kuwasilishwa katika kikao cha pamoja na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo.”

Akikubaliana na uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi wa kurudia uchaguzi katika kituo hicho, Nyalusi alisema madai ya uchaguzi mzima wa jimbo kurudiwa hayakubaliki kwa sababu hayaendani na sheria za uchaguzi na yanakiuka misingi ya demokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa.

“Kwanza nikanushe kwamba walioiba maboksi hayo ya kura ni wafuasi wa Chadema kama inavyodaiwa na CCM kwani kuvaa vazi lenye nembo ya Chadema hakuhalalishi kwamba kila anayevaa vazi hilo ni mfuasi au mwanachama wetu maana katika siasa wapinzani wetu wanaweza kuwatumia watu wao waliowavalisha mavazi yenye nembo yetu ili kufanya jambo litakalohalalisha jambo wanalotaka kulifanya,” alisema.

Nyalusi alisema wakati uchaguzi huo ukitarajiwa kurudiwa katika kituo hicho taarifa walizokusanya toka kwa mawakala wao zinaonesha mgombea wao, Mchungaji Peter Msigwa zinaonesha amepata ushindi dhidi ya mgombea wa CCM, Fredericck Mwakalebela na wagombea wengine wanne walioshiriki kinyang’anyiro hicho.

Pamoja na Mchungaji Msigwa kudaiwa kupata ushindi huo, chama hicho pia kinaongoza udiwani katika kata 14 kati ya kata 18 za jimbo hilo, matokeo ambayo kwa mujibu wa Mwampashi yamekishtua chama chake, CCM.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...