Skip to main content

UNESCO kuendelea kushirikiana na Idara ya Mambo ya Kale nchini



Baadhi ya washiriki wa warsha iliyoandaliwa na UNESCO pamoja na Idara ya Mambo ya Kale wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Mr Adelhelm Meru kufungua warsha hiyo iliyofanyika Coral Beach jijini Dar Es Salaam


Baadhi ya viongozi wa Hifadhi wakifuatilia warsha hiyo iliyoandaliwa na UNESCO pamoja na Idara ya Mambo ya Kale


Mwakilishi wa UNESCO Nchini Ms Zulmira Rodriguez (katikati) akichangia moja ya mada iliyowasilishwa na baadhi ya wakuu wa hifadhi waliohudhuria warsha hiyo. 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dr Adelhelm Meru akifungua warsha ya siku moja iliyoandaliwa na UNESCO kwa kushirikiana na Idara ya Mambo ya Kale kwaajili ya kujadili uboreshwaji wa utawala na matumizi endelevu ya hifadhi za urithi na mazingira za Tanzania, ambazo ni Magofu ya Kilwa; Michoro ya Asili Kondoa; Mji Mkongwe Zanzibar; Hifadhi ya Wanyama Selous; Hifadhi za Taifa za Serengeti, Ngorongoro, Lake Manyara na Mlima Kilimanjaro; na Hifadhi ya Mazingira ya Usambara Mashariki’.
Mkuu wa Hifadhi ya Kondoa Rock Art, Zuberi Mabie akichangia mada katika warsha hiyo iliyofanyika jana katika kujadili mafanikio na changamoto zinazoikabili hifadhi hizo.



Warsha ikiendelea juu ya utunzaji na uendelezaji wa maliasili na vivutio vya Utalii iliyofanyika katika hoteli ya Coral Beach jijini Dar Es Salaam





Na Josephat Lukaza

UNESCO kwa kushirikiana na Idara ya mambo ya kale imeendesha warsha ya siku moja kwa wakuu wa hifadhi na vivutio vya utalii hapa nchini huku wakuu hao wakishirikishana mafanikio na changamoto zinazowakabili katika hifadhi zao

Warsha hiyo iliyohudhuriwa na Wakuu wa hifadhi mbalimbali hapa nchini iliweza kuhusisha uwasilishaji wa mafanikio na changamoto wanazokutana nazo wakuu wa hifadhi hizo katika hifadhi huku matatizo makubwa yakiwa ni Ukosefu wa Pesa kwaajili ya Kujiendesha na Kwa baadhi ya hifadhi kukosa nyumba za Wafanyakazi na upungufu wa wafanyakazi kwa baadhi ya hifadhi hizo.

Mbali na Changamoto hizo pia wakuu wa hifadhi walielezea mafanikio yao katika hifadhi hizo katika vipengele tofauti tofauti kama Vitendea kazi, Ujumuikaji wa jamii katika hifadhi hizo, Utalii, Rasilimali watu, Uhifadhi Utawala na mengineyo.

Moja ya mafanikio katika nyanja tofauti Mkuu wa Hifadhi ya Usambara Mashiriki (East Usambara Reserve Management) Bi Mwanaidi Kijazi alisema kuwa hifadhi yake imetokea kuwa kituo cha Mafunzo kwa wengine na kupelekea kuanzishwa kwa Amani Nature Reserve na hifadhi hiyo kufanikiwa katika kutoa taarifa kwa wakati kwa njia ya Vipeperushi kuhusiana na Mradi huo wa Amani Nature ambao upo kusini mwa Hifadhi hiyo ya Usambara Mashariki.

Vilevile alisema katika hifadhi yake kuna wafanyakazi ambao wanaweza kuhudhuria shughuli za Hifadhi hiyo na kusema na hiyo ni moja ya Mafanikio katika Hifadhi hiyo ya Usambara Mashariki.

Kwa Upande wao UNESCO walisema wataendelea kushirikiana na idara ya Mambo ya Kale katika kutoa ushirikiano na misaada ya kitaalam katika kuhakikisha Hifadhi hizi zinaweza kujiendeleza na kujiboresha na kuvutia watalii zaidi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...