Skip to main content

UNESCO YAENDELEA KUZIJENGEA UWEZO REDIO ZA JAMII NCHINI



Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph, akizungumza katika kongamano lililowakutanisha watendaji kutoka Redio za jamii nchini katika mji wa Terat, wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara jana.


Mwenyekiti wa Muungano wa Redio za Kijamii nchini (COMNETA), Sekiku Joseph akizungumza katika Kongamano hilo ambalo amesisitiza umuhimu wa viongozi wa Radio za kijamii kuthamini michango inayotolewa na wafadhili ili iweze kuwa endelevu.


Mshauri na Mkufunzi wa masuala ya vyombo vya habari jamii kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu akisistiza jambo katika mafunzo hayo.


Afisa Miradi mpya wa Unesco, Nancy Kaizirege akisisitiza jambo.


Mkurugenzi wa Redio ya Jamii Uvinza FM, Ayub Kalufya akichangia mada na kuomba Unesco kuendelea kutoa usaidizi kwao kutokana na mchango wanaoutoa kwa jamii.


Afisa Miradi mpya wa Unesco, Nancy Kaizirege akisisitiza jambo wakati mafunzo hayo yakiendelea. kulia ni Meneja wa Orkonerei Radio Service Simanjiro Manyara (ORS FM), Bw.Baraka Ole Maika.


Mwenyekiti wa Bodi ya Redio ya Jamii 94.9 FM , Mkoani Pemba, Hamidu Hassan Bakari akizungumza namna Redio yake itakavyonufaika kupitia mafunzo ya kuwajengea uwezo na vifaa ya matangazo.


Meneja wa Redio Kahama FM, Marco Mipawa, akizungumza jambo.

Mwandishi Wetu,Simanjiro

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu,Sayansi na Utamaduni(UNESCO) limeendelea kuimarisha Redio za Jamii nchini kwa kuwapa mafunzo ya mara kwa mara watendaji wa ngazi mbalimbali kwa lengo la kuzifanya Redio hizo kuwahudumia vema wananchi wanaoishi maeneo ya vijijini.

Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph amesema kumekuwa na mafanikio tangu mradi huo kuanza miaka mitatu iliyopita chini ya ufadhili wa UNESCO, Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA) na Serikali ya Uswizi ambapo licha ya kuwajengea uwezo vifaa vya kieletroniki vilitolewa kwa Redio hizo.

Kongamano hilo la mwaka la siku tatu(3) linafanyika katika Kituo cha Orkonerei Radio Service Simanjiro Manyara (ORS), Terat wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara na limewaleta pamoja watendaji wa Redio za Jamii 20 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Zanzibar .

“Tunalenga kuwajengea uwezo ili hizi Redio za Jamii zifanye kazi kwa weredi ya kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi waweze kushiriki mijadala inayohusu sekta za afya, elimu na kilimo,”amesema Yusuph

UNESCO inafanya kazi kwa karibu na Muungano wa Radio za Kijamii Tanzania(COMNETA)unaongozwa na Mwenyekiti wake Sekiku Joseph.





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...