Skip to main content

UNESCO YAWAKUTANISHA WADAU KUJADILI AMANI UCHAGUZI MKUU



Katibu Mkuu wa Baraza la Mahedhebu kwaajili ya Amani,Mchungaji,Canon Thomas Godda akizungumza katika kongamano la Amani lililoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,Sayansi na Utamaduni (UNESCO)kwa kushirikiana na madhehebu ya Dini na Viongozi wa Mila ili kuhamasisha amani katika kipindi cha uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Na Mwandishi wetu, Simanjro

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia na Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) limekutanisha wadau mbalimbali katika kongamano la kujadili na kuhamasisha amani katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 4,2015

Kongamano hilo lilifanyika katika Kituo cha Redio Orkonerei (ORS)Terrat wilaya ya Simanjiro mkoa wa Manyara na kuwaleta pamoja viongozi wa dini,mila na wawakili wa muungano wa Redio za Jamii nchini(Comneta)ambao kwa pamoja walisisitiza umuhimu wa amani.

Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph alisema mchango wa unaotolewa na Redio za kijamii nchini ni mkubwa kwani unawawezesha wananchi kuzitumia kujiletea maendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya kuhamasisha amani na utulivu katika kipindi hiki na baada ya uchaguzi mkuu.

Ameongeza kuwa Muungano wenye nguvu wa Redio za Jamii ndio ukombozi wa wananchi kwani wanahitaji kuelimishwa maswala mbalimbali ya afya, kilimo na programu zinazoandaliwa na serikali kwajili ya wananchi.

Mmoja wa viongozi wa mila ,Laigwanani Lesira Samburi alisema viongozi wa mila licha ya mchango wao kwenye jamii bado hawajashirikishwa ipasavyo pamoja kuwa huwa hawajishughulishi na siasa moja kwa moja.

"Naomba serikali itambue mchango wetu katika kutatua migogoro na kuhamasisha amani kwenye jamii zetu,tunaweza kufanya mambo makubwa kama serikali ikitushirikisha ipasavyo sio katika kipindi hiki cha uchaguzi tu bali hata baada ya uchaguzi,"alisema Samburi


Mwenyekiti wa Radio za Jamii kutoka UNESCO na Mhadhiri Mwandamizi wa Mawasiliano katika Chuo Kikuu cha Hyderabad, Profesa Vinod Pavarala akizungumza katika kongamano la amani, lililofanyika katika Kituo cha Redio ya Jamii ya ORS (OPA)iliyopo wilaya ya Simanjiro mkoa wa Manyara. Pichani wanaofatilia kwa karibu ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Dini kwa ajili ya Amani, Mchungaji Thomas Godda na Afisa Miradi wa UNESCO, Al-Amin Yusuph.

Nae Katibu Mtendaji wa Baraza la Dini kwaajili ya amani, Mchungaji Thomas Godda alisema viongozi wa mila wana michango muhimu kwani wako karibu sana na jamii inayowazunguka hivyo wakishirikiana na viongozi wa madhehebu ya dini na asasi za kiraia kuna mambo ya msingi yatakayoipa jamii heshima .

Alisema Tume ya uchaguzi imewashirikisha katika hatua muhimu wadau wake kuhakikisha kila mwananchi aliyejiandikisha anapata haki ya kupiga kura na hakuna udanganyifu utakaotokea hivyo kuwataka wananchi washiriki kwa amani tukio hilo muhimu katika kukuza demokrasia nchini.

Mjumbe wa bodi ya Muungano wa Redio za Jamii nchini (COMNETA), Balozi Christopher Liundi alisema iwapo wananchi watazitumia ipasavyo redio za jamii zitaleta mabadiliko chanya.


Mjumbe wa Bodi ya Muungano wa Redio za Jamii nchini (COMNETA), Balozi Christopher Liundi akichangia mada ya umuhimu wa matumizi ya Redio za Jamii.


Kiongozi wa Mila ya jamii ya wafugaji katika Kijiji cha Terrat wilaya Simanjiro mkoa wa Manyara, Lesira Samburi akizungumza kwenye kongamano la kuhamasisha amani kuelekea Uchaguzi Mkuu.


Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Redio ya Jamii 94.9 Mkoani,Pemba,Hamdu Hasan Bakari (kushoto)akiteta jambo na Katibu Mtendaji wa Baraza la Dini kwa ajili ya Amani, Mchungaji Thomas Godda.


Meneja wa Orkonerei Radio Service Simanjiro Manyara (ORS FM), Bw. Baraka Ole Maika akivishwa Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph mavazi ya jamii ya wafugaji wa kimaasai ikiwa ni ishara ya kumpongeza na kumuaga baada kuhamishwa kikazi nchini India, kushoto ni Mwenyekiti wa Muungano wa Redio za Jamii nchini (COMNETA), Joseph Sekiku.


Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph (kulia) akifurahia zawadi ya mavazi na Rungu la jamii ya wafugaji wa kimaasai na kusimikwa rasmi kuwa 'Laigwanan' kwa kutambua mchango wake katika kuendeleza jamii hiyo kupitia Redio za jamii nchini, Al Amin amepewa uhamisho kwenda India, kushoto ni Kiongozi wa Mila, Laigwanan Lesira Samburi na Mwenyekiti wa Muungano wa Redio za Jamii (COMNETA) Sekiku Joseph.


Viongozi wa Mila wakionesha ujumbe wa kuhamasisha amani.


Katibu Mtendaji wa Baraza la Dini kwaajili ya Amani, Mchungaji Thomas Godda (kushoto) akiteta jambo na maafisa wa UNESCO, Nancy Kaizirege na Al -Amin Yusuph.


Ujumbe wa Muungano wa Redio za Jamii,Wazee wa Mila na Viongozi wa dini wakiwasili kwenye kiwanda cha kuzalisha nishati kwa njia ya Mibono katika Kijiji cha Terrat ambacho kimekua msaada kwa wananchi wengi.







Mkurugenzi wa Kituo cha Redio ya Jamii ya ORS (OPA)iliyopo wilaya ya Simanjiro mkoa wa Manyara,Martin Kariongi (kushoto) akizungumza na ujumbe ulioshiriki kongamano la amani lililoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshighulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) waliotembelea mtambo wa kuzalisha umeme kwa kutumia teknolojia ya Mafuta ya Mibono.





Mbegu zinazotumika kuzalisha mafuta kwa ajili ya nishati.





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...