Skip to main content

WAHUKUMIWA JELA MMOJA KILA MOJA KWA KWA KUJIANDISHA MARA MBILI BVR



WAKATI wananchi wanajiandaa kushiriki Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 25 mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imewahukumu Majuto Kisumbe (22)na Zawadi Mdegela (33) kulipa faini ya laki moja au kwenda jela mwaka mmoja baada ya kukiri kosa la kujiandikisha zaidi ya mara moja kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura .

Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi Andrew Peter Scout alisema Kisumbe na Mdegela wamehukumiwa kulipa faini au kenda jela mwaka moja kwa kosa la kujiandisha mara mbili kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura (BVR) kinyume na Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 2010.

Alisema kuwa katika nyakati tofauti Kisumbe, mkazi wa Mahenga wilayani Kilolo, Mkoa wa Iringa na Zawadi Mdegela wa Ifunda wilayani Iringa walijiandikisha mara mbili katika BVR katika vituo viwili tofauti. 

Hakimu Mkazi Andrew Peter Scout alisema Kisumbe alitenda kosa hilo tarehe 04 Aprili mwaka huu katika Kijiji cha Mahenge, Wilaya ya Kilolo.

Alisema kuwa mtuhumiwa Kisumbe alikutwa na kadi mbili za kupigia kura zenye namba T-1000-7557-236-8 na T- 1000-1387-385-4 alizojiandikisha katika sehemu tofauti eneo la Mahenge.

Naye Mdegela alikutwa na kadi mbili zenye namba T-1001-3631-728-2 na T-1001-2848-874-4.

Hata hivyo hakimu mkazi huyo alisema kuwa Majuto Kisumbe na zawadi Mdegela wamepoteza sifa ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu mwaka huu kutokana kujiandikisha mara mbili kwenye daftari

Kesi hizo ziliendeshwa katika mahakama isiyo wazi na washitakiwa waliomba wapunguziwe adhabu na hakimu alizingatia hilo kwa vile washitakiwa walitenda kosa hilo kwa kutojua na ni mara yake ya kwanza alisema kuwa walipa faini y laki mmoja au jela mwaka moja. 

Wananchi wengi waliofikisha miaka kumi na nane (18) na kuendelea tayari wameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. 

Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ni hitaji la Kikatiba. 

Tume ya Taifa ya Uchaguzi, imepewa jukumu la kisheria la kuandikisha wapiga kura katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura pamoja na kuliboresha kwa ajili ya Uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani. 

Hata hivyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Iringa aliongeza kuwa mfumo mpya wa BVR utasaidia kupunguza au kuondoa matatizo yaliyomo kwenye daftari lililopo ikiwamo kuzuia mtu kujiandikisha zaidi ya mara moja.

Hivi karibuni Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilibaini kuwa jumla ya wananchi 231,955 nchini walijiandikisha zaidi ya mara moja katika daftari la kudumu la wapiga kura.



Baada ya kuchakata daftari, mchakato wa mwisho wa kuhakiki daftari, hatimaye idadi halisi ya wapiga kura ni 23,154,485 ambapo 22,651,292 waliandikishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na 503,193 waliandikishwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...