Skip to main content

Williamu lukuvi amembeza mpinzani wake katika jimbo la ismani

MGOMBEA ubunge wa jimbo la Ismani kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM) William Lukuvi

Na fredy mgunda, Ismani
 
MGOMBEA ubunge wa jimbo la Ismani kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM) William Lukuvi amembeza mgombea mwenzake anayegombea ubunge kwenye jimbo hilo kupitia chama cha demokrasia na maendeleo chadema Patrick Olle Sosopi na kusema kuwa Sosopi hata afanye hawezi kuvaa viatu vyake kwa kuwa mbunge wa jimbo hilo.

Kauli ya Lukuvi aliitoa juzi wakati akiwahutubia wananchi wa vijiji vya Igingilanyi,Kising’a,Kinywang’anga,Mkungugu,Matembo na Ilambilole vilivyopo tarafa ya Isimani katika Jimo la Ismani alisema kuwa Sosopi hawezi kuvaa viatu vyake kwa kuwa mbunge wa jimbo hilo kwa maana hana staha ya kuweza kuwashawishi wananchi kuwaletea maendeleo na badala yake anawabeza wagombea wa chama cha mapinduzi CCM pamoja na mgombea ubunge wa jimbo hilo kwa kusema kuwa kwa kipindi cha miaka 20 ya ubunge wa Lukuvi hakuna maendeleo yoyote yaliyofanywa na chama hicho.


“Mimi kiatu change navaa namba nane Sosopi anavaa namba moja hivi kweli ataweza kuwa mbunge wa jimbo hili?alihoji huku akishangiliwa sana na wananchi hao,kiukweli niwaambie kama mnataka maendeleo kichagueni CCM ndicho chama pekee kitakachowaletea maendeleo na sio chama kingine.”alisema Lukuvi


Akiwa katika kijiji cha Kinywang’anga Lukuvi aliahidi kuwatafutia wananchi hao madaktari wa kutosha kwenye zahanati zilizopo kwenye jimbo hilo pamoja na dawa za kutosha ili kuendeleza huduma nzuri ya afya kwenye jimbo lake.


Alisma kuwa akatika kuendeleza kuduma nzuri ya afya tayari ameagiza gari ya kubebea wagonjwa(Ambulance) nchini Japani yenye gharama ya Tsh.mil 120 kwa ajili ya zahanati ya kijiji cha Kinywang’anga.


Alisema kuwa kwa sasa tayari ujenziwa zahanati ya kisinga unaendelea na wanajenga wodi ya watoto,wodi ya wazazi pamoja na nyumba za kuishi watumishi ikiwa maendeleo yote yameletwa chini ya uongozi wa CCM.


Alisema kwa kipindi cha miaka miatano ijayo atahakikisha wananchi wake wanapata maji ya uhakika kutoka Jimbo la Iringa mjini ambayo yanatokana na Mto wa Ruaha.


“ Tayari fedha za kuvuta maji yam to Ruaha kutoka Iringa mjini hadi Ismani tumeshapata,wataalamu tayari wapo na wamesema muda wowote kuanzia sasa zoezi la maji Ismani litaanza”alisema Lukuvi


Aliongeza kuwa uongozi wa serikali ya magufuli hata kabla ya kuamua kugombea Urais tayari alishaweka mpango wa kutengeneza barabara ya Kising’a,Ilambilole,Mikongwi,Ngano hadi Ismani tarafani kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Km.35 kwa gharama ya zaidi ya Uro milioni tano ambapo tayari ujenzi huo umeshaanza.


Wakati akihutubia wananchiwa kijiji cha mkungugu alisema kuwa atahakikisha atapandisha kiwango cha elimu kwenye jimbo hilo pamoja na kuweka haki sawa kwa wanawake na wanaume katika kumiliki ardhi.


Hata hivyo alisema kuwa suala la umeme kwenye jimbo hilo kwa baadhi ya maeneo ni la muhimu kwa sababu kuna maeneo yaliyopo ndani ndani hayana umeme hivyo atahakikisha ataleta nguzo kwa haraka ili wananchi hao waweze kuwa umeme.
 
“Nitawapigania kuhakikisha umeme unaingia kwenye vijiji vilivyojificha sana ndani ndani na nawaambia lazima nitawaletea nguzo kwa maana mimi mwenyewe jambo la nguzo sitoshindwa,”alisema Lukuvi.
 
Hata hivyo aliwataka wananchi hao kumchagua mgombea urais wa CCM John Magufuli,mgombea ubunge Williamu Lukuvi pamoja na mgombea udiwani wa kata ya kising’a Ritta Malagala ili waweze kuwaletea maendeleo ya jimbo hilo na sio mtu mwingine.
 
Alisema kuwa kwa uongozi wa Magufuli yeye hataki mchezo huu ni wakati wa kazi na sio lelemama na kama kutakuwa na kiongozi ambaye ataonesha amekaa legelege lazima atanyooka kwa maana magufuli hapendi mtu ambae sio mchapa kazi.




Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...