Skip to main content

ALGERIA YAIFUNGASHIA STARS FURUSHI LA MAGOLI

Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars'Kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ 


Timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ imeondoshwa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania kupangwa kwenye hatua ya makundi kwa ajili ya kutafuta nafasi ya kucheza fainali za kombe la dunia mwaka 2018 ambazo zitafanyika nchini Urusi baada ya kufungwa kwa magoli 7-0 kwenye mchezo wa marudiano uliochezwa kwenye uwanja wa Mustapher Tchaker mjini Blida, Algeria

Stars imeondoshwa kwa jumla ya mabao 9-2 baada ya kucheza michezo miwili, mchezo wa kwanza Stars ililazimishwa sare ya kufungana kwa goli 2-2 na Algeria jijini Dar es Salaam huku mchezo wa pili uliopigwa Blida, Algeria ukimalizika kwa Stars kulala kwa goli 7-0.

Algeria walianza kupata bao la kwanza sekunde ya 40 kupitia kwa Yacine Brahimi huku Ghoulam Faouzi akipachika goli la pili dakika ya 23 kabla ya Ryad Mahrez kutupia la tatu dakika ya 43 na kuufanya mchezo kwenda mapumziko Algeria wakiwa mbele kwa magoli 3-0 dhidi ya Stars.

Kipindi cha pili kilianza kwa Stars kufanya mabadiliko kwa kuwatoa Farid Musa na nafasi yake kuchukuliwa na Salum Telela wakati Aishi Manula aliingia kuchukua nafasi ya Ali Mustafa.

Dakika ya 49 Algeria waliendeleza mvua ya magoli kwa Stars baada ya Slimani Islam kuipatia Algeria bao la nne kwa mkwaju wa penati wakati Ghoulam Faouzi akiifungia Algeria tano pia kwa mkwaju wa penati ikiwa ni dakika ya 59.

Carl Medjani akafunga goli la sita dakika ya 72 huku Slimani Islam akipachika bao la saba dakika ya 75.

Farid Musa, Himid Mao Mkami, Kelvin Yondani, Haji Mwinyi Nadir Haroub na Aishi Manula walioneshwa kadi ya njano huku Mudathir Yahya akioneshwa kadi mbili za njano zilizopelekea kupata kadi nyekundu dakika ya 41 kipindi cha kwanza na kuiacha Stars ikicheza pungufu kwa muda wote uliosaliaPublished By: Shaffih Dauda 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...