Skip to main content

CWT MKOA WA DAR ES SALAAM KINAIDAI SERIKALI SH.BILIONI 1.1




Posted by Ngabwe Mlulu on 08:31




Amina Kisenge





Na Dotto Mwaibale

WALIMU wa Mkoa wa Dar es Salaam wanaidai Serikali jumla ya sh. Bilioni 1.1 za madai yao mbalimbali kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi 2015.

Hayo yalielezwa na Mwenyekiti wa Chama cha Walimu (CWT) Mkoa wa Dar es Salaam, Mwalimu Amina Kisenge (pichani kushoto), katika kikao cha baraza la dharura la chama hicho lililoketi hivi karibuni.

Awali CWT ilikua ikidai jumla ya Sh.Bilioni 3.9 kabla ya kupunguza kiasi cha Sh.Bilioni 1.9 mapema mwaka huu.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti, madeni hayo ni pamoja na malimbikizo ya nauri za likizo kuanzia mwezi wa Juni na Desemba, 2013; na Juni na Desemba mwaka jana.

Malimbikizo mengine ni pamoja na pesa ya kuwasafirisha wastaafu kwenda majumbani kwao, alisema Kisenge.

"Uhamisho wa walimu kutoa kituo kimoja kwenda kingine ikiwa ni posho ya usumbufu na ya kujikimu; pamoja na pesa za gharama za masomo baada ya walimu kujigharamia kujisomesha, imekuwa pia ni tatizo kwa serikali kutoa," alisema Mwenyekiti.

Kisenge aliongeza kwamba chamgamoto nyingine inayowakabili walimu ni mfuko wa PSPF kutowalipa walimu wastaafu kwa wakati ambapo walimu waliostaafu Januari hadi Septemba mwaka huu hawajalipwa mafao yao.

Kero nyingine kwa mujibu wa CWT ni walimu kutopandishwa madaraja kwa wakati na kwa wale wanaobahatika kupanda madaraja, mishahara yao hairekeshwi.

Wakati huohuo, CWT iliitaka serikali ya awamu ya tano kuharakisha matumizi ya chombo cha ajira kwa walimu kilichopitishwa na serikali ya awamu ya nne;kwamba chombo hicho ndicho mkombozi wao. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...