Skip to main content

JUHUDI BINAFSI ZINATAKIWA KUMALIZA UKEKETAJI, UNYANYASAJI KIJINSIA – ROSE HAJI MWALIMU



Afisa Maendeleo ya Jamii (W) Ngorongoro, Teresia Irafay (wa pili kushoto) akiitambulisha meza kuu kabla ya kumkaribisha Katibu Tawala wa Wilaya ya Ngorongoro, Lemuel Kileo, (wa tatu kulia) kufungua kongamano la viongozi wa mila wa kabila la wamasai (Laigwanan/Ngaigwanani) na wanawake Mashuhuri yenye lengo la kushawishi uondoaji wa mila potofu zinazorudisha nyuma maendeleo katika jamii za wafugaji. Kushoto ni Mtaalamu wa masuala ya vyombo vya habari vya kijamii na Mkufunzi kutoka (UNESCO), Bi. Rose Haji Mwalimu, Kiongozi wa Malaiboni wilaya ya Ngorongoro Bw. Sangau Naimodu (wa pili kulia) pamoja na Katibu wa Baraza Mila (W) Ngorongoro, Laanoi Munge, (kulia), Mwenyekiti wa Baraza la Malaigwanan wilaya ya Ngorongoro, Joseph Oletiripai (wa tatu kushoto). (Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).

Na Modewjiblog team

JAMII ya wafugaji imetakiwa kutumia juhudi zao binafsi kubadilisha mawazo na imani ya jamii kwamba mila na desturi hazibadiliki ili kutengeneza mfumo bora mpya unaothamini maisha ya wanawake.

Wito huo umetolewa na Mtaalamu wa masuala ya vyombo vya habari vya kijamii na Mkufunzi, Bi. Rose Haji Mwalimu wakati akiwasilisha mada kwenye kongamano la viongozi wa mila wa kabila la wamasai (Laigwanan/Ngaigwanan), Laiboni na wanawake Mashuhuri yenye lengo la kushawishi uondoaji wa mila potofu zinazorudisha nyuma maendeleo katika jamii za wafugaji.

Aliwataka washiriki wa warsha kusimama kidete na kutumia elimu waliyoipata katika kushawishi jamii kubadilika na kuachana na mila za ukekeketaji,ndoa za utotoni na pia unyanyasaji mwingine wa kijinsia unaoonesha ubabe wa wanaume na mfumo dume.

Aliwataka wanajamii hao kutumia njia mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari, rediojamii, vikao mbalimbali vya kata na vijiji pamoja na nyumba za ibada kuhimiza watu kubadilika na kuacha mila hizo za ukeketaji na kuozesha watoto katika umri mdogo.

Aidha Bi. Rose Haji Mwalimu katika kongamano hilo lililoandaliwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa, (UNESCO) amewataka wanawake kuvunja ukimya na kuacha uoga na kuibua vitu vinavyowanyima haki zao za msingi.


KatibuTawala wa Wilaya ya Ngorongoro, Lemuel Kileo akifungua kongamano la viongozi wa mila (Laigwanan/Ngaigwanan na Laibon) pamoja wanawake mashuhuri lenye lengo la kuondoa mila potofu zinazokwamisha maendeleo katika jamii za wafugaji ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro.

Aliwataka wanawake kujitambua ili kutumia sheria zinazowalinda kuondokana na unyanyasaji pamoja na ukatili wa kijinsia unaoendelea katika jamii za kifugaji na kuwaomba viongozi wa mila washiriki katika kuondoa mfumo dume.

Naye Ofisa Ustawi wa Jamii wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro, Benezeth Bwikizo, amesema kama watuw atajitokeza na kueleza ukweli serikali itachukua hatua hasa ya kulinda wanawake na watoto kupitia mamlaka iliyokabidhiwa na Katiba ya nchi.

Alisema kwa mujibu wa sheria Serikali ina mamlaka ya kuhakikisha kwamba haki za watoto zinalindwa kupitia sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwamba mtoto lazima alindwe na apate haki zake zote za msingi.

Alisema pamoja na katika na sheria zilizotungwa, mtoto pia analindwa na mkataba wa kimataifa wa haki za mtoto wa Novemba 20, 1989 inayotoa ufafanuzi wa kulinda na kuhakikisha kwamba haki za mtoto zinalindwa na kuheshimiwa.

Aliongeza kuwa pia ulindaji huo wa haki za mtoto unakwenda sanjari na mkataba wa Umoja wa nchi za Afrika ya mwaka 1990 unaotoa ufafanuzi juu ya haki za msingi za mtoto na namna inavyotakiwa kuheshimiwa na kulindwa bila kuathiri haki zao.


Ofisa Elimu ya Uzazi na UKIMWI kutoka UNESCO, Mathias Herman akizungumzia malengo ya kongamano hilo kwa washiriki.

Bw.Bwikizo, alitaja haki za muhimu kwa mtoto zinazotakiwa kulindwa na kuheshimiwa ili kuhakikisha mtoto anakua katika malezi bora ni huduma za afya, chanjo, matibabu, Lishe na malezi bora kupata haki ya kuishi, haki ya kuendelezwa na haki ya kulindwa.

Akizungumza katika ufunguzi wa kongamano hilo, KatibuTawala wa Wilaya ya Ngorongoro, Lemuel Kileo, amelishukuru Shirika la UNESCO kwa kuendesha mafunzo hayo ya kutoa elimu na kujenga uwezo kwa viongozi wa mila na wanawake mashuhuri ili kuondoa mila potofu katika jamii ikiwemo Ukeketaji, mimba za Utotoni na ndoa za umri mdogo.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya, Bw. Kileo aliwataka viongozi na washiriki wa warsha hiyo watumie nafasi hiyo waliyoipata kwenda kufikisha ujumbe kwa jamii ili kupeleka maendeleo mbele kwa kupunguza vifo vya akinamama na wasichana wenye umri mdogo, kuondokana na ukeketaji pamoja na mimba za umri mdogo.


Mtaalamu wa masuala ya vyombo vya habari vya kijamii na Mkufunzi kutoka UNESCO, Bi. Rose Haji Mwalimu akisisitiza jambo kwa washiriki wa kongamano.

Kwa upande wa mmoja wa wakufunzi wa warsha hiyo kutoka UNESCO akizungumzia malengo ya warsha hiyo, Ofisa Elimu ya Uzazi na Ukimwi wa shirika hilo, Mathias Herman, amesema warsha hiyo ni mwendelezo wa warsha zinazotolewa na UNESCO kwa ajili ya kutoa elimu ya kuwajengea uwezo na kugawa majukumu kwa viongozi wa kimila (Laigwanan), wa mama mashuhuri, viongozi wadini, wakunga wa jadi pamoja na waandishi wa habari kufanya ufuatiliaji wa afya ya uzazi na malezi bora kwa watoto.

Aliongeza kuwa UNESCO inatarajia mafunzo hayo kutaleta mabadiliko kupitia nafasi ya viongozi hao mashuhuri katika jamii kwa kuwa wanaaminika ili kushirikiana na wadau wengine wa maendeleo wanaotoa mafunzo kuhakikisha kwamba suala la mimba za utotoni, ndoa za utotoni pamoja na ukeketaji linafika mwisho katika jamiii ya kifugaji.



Mwenyekiti wa Baraza la Malaigwanan wilaya ya Ngorongoro, Joseph Oletiripai akisisitiza jambo kwa Malaigwanan pamoja na wakina mama mashuhuri ambapo aliwataka watumie nafasi waliyopewa na jamii na fursa ya elimu waliyopata kutoka kwa wadau wa maendeleo UNESCO kuwa italeta mabadiliko na mpango chanya katika jamii ya Kimasai.


Ofisa Ustawi wa Jamii wa wilaya ya Ngorongoro, Benezeth Bwikizo (kuhoto) akizungumzia haki za watoto. Kulia ni Mkalimani wa lugha ya Kimasaai Mchungaji Mark Murenga.


Mama Mashuhuri kutoka kijiji cha Olopiri, Nolarir Pashuku, akitoa maoni yake kwenye kongamano.


Mmoja wa washiriki katika warsha hiyo ambaye ni Laigwanan , John Olekulinja kutoka kata ya Malambo akizungumzia mafunzo hayo.


Kiongozi wa Malaiboni wilaya ya Ngorongoro Bw. Sangau Naimodu (katikati) akieleza namna inavyofaa kueneza elimu ya mabadiliko.


Mratibu wa Afya ya Uzazi na Mtoto, tarafa ya Loliondo (W) Ngorongoro, Bi. Nailejileji Joseph akitoa elimu ya uzazi wa mpango kwa washiriki wa kongamano hilo.


Pichani juu na chini ni viongozi wa mila wa kabila la wamasai (Laigwanan/Ngaigwanan), Laiboni na wanawake Mashuhuri walioshiriki kwenye kongamano hilo yenye lengo la kushawishi uondoaji wa mila potofu zinazorudisha nyuma maendeleo katika jamii za wafugaji lilioandaliwa na Shirika la UNESCO.








Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...