Skip to main content

KASSIM MAJALIWA ATEULIWA KUWA WAZIRI MKUU SERIKALI YA AWAMU YA TANO




Na Khalfan Said
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli hatimaye ametungua kitendawili cha nani atakayekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kumteua Mbunge wa Ruangwa mkoani Lindi,  Kassim Majaliwa.

Spika wa Bunge Job Ndugai, alipokea bahasha yenye jina la mteule huyo wa Rais, kutoka kwa Mpambe wa Rais, ambaye akiwa ndani ya sare zake za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, JWTZ, aliongozwa na wapambe wa Bunge hadi kwenye meza ya Spika Ndugai na kumkabidhi bahasha hiyo mapema  Novemba 19, 2015.

Baada ya Mh. Ndugai kupokea bahasha hiyo aliwaonyesha wabunge na kusema bahasha hii imewekewa seal, hivyo akamwita Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashilila na kumtaka aifungue ili kujua jina la Waziri Mkuu ni nani.

Dkt. Kashilila aliifungua bahasha hiyo na kukumbana na bahasha ya pili, hata alipoifungua bahasha hiyo ya pili akakumbana na bahasha ya tatu na ilipofungunliwa akakutana na kadi maalum yenye ujumbe ulioandikwa kwa mkono na Mh. Rais mwenyewe kuonyesha kuwa haikupitia kwenye mkono wa mtu mwingine na hivyo kusoma jina la mteule huyo ambaye sasa anasubiri kuthibitishwa na wabunge baadaye Alhamisi Novemba 19, 2015 kwenye kipindi cha bunge majira ya jioni

Kassim Majaliwa alikuwa Naibu Waziri wa ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), kwenye serikali ya awamu ya nne akishughulika sana na masuala ya elimu.

Kassim Majaliwa alizaliwa Desemba 22, 1960 huko mkoani Lindi, na amekuwa mbunge wa jimbo ;la Ruangwa moani Lindi tangu mwaka 2010.

Chini ni matukio mbalimbali ya kiutendaji ambayo Kassim Majaliwa alikuwa akiyatekeleza kwenye nafasi yake ya Ubunge na Unaibu Waziri wa TAMISEMI






Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...