Skip to main content

'Matumizi ya choo na unawaji wa mikono kwa sabuni bado vikiwa bado vipo chini'

IRINGA: JUMLA ya kaya 201,120 ambayo ni sawa na asilimia 89 mkoani Iringa zina vyoo na kati ya Kaya hizo asilimia 17 tu ndiyo zenye vyoo bora. 

Kauli hiyo imetolewa jana na katibu tawala wa mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mafunzo ya kuhamamisisha wanahabari juu ya usafi wa mazingira.

Ayubu alisema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwa kuwajengea uwezo wanahabari kujua mambo muhimu yanayohusiana usafi wa mazingira na matumizi ya choo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya usafi wa mazingira hapa nchini.

Alisema kuwa hali ya unawaji mikono kwa sabuni ni sawa na asilimia tisa huku hali ya matumizi ya choo na unawaji wa mikono kwa sabuni bado vikiwa bado vipo chini.

Naye ofisa afya wa mkoa wa Iringa Khadija Haroun alisema mafunzo hayo yanaenda sambamba na wiki ya usafi wa mazingira hapa nchini.

Haroun alisema kuwa watu takriban milioni 1.8 wanakufa kila mwaka duniani kote kutokana na magonjwa ya kuhara.

Alisema kuwa watoto chini ya miaka mitano 760,000 hufa kila mwaka kutokana na magonjwa ya kuhara kila mwaka.

Pia alisema kuwa tanzania watu 30,000 hufa kila mwaka kutokana na magonjwa ya kuhara.

“Asilimia 60 hadi 80 ya wagonjwa wote wa nje wana magonjwa yanayosababishwa na ukosefu wa maji na mazingira machafu.”alisema Haroun

Aliwataka wananchi kuonya matunda kabla ya kula ,kunawa mikono kwa maji safi na sabuni mara baada ya kutoka chooni ili kuepukana na magonjwa hayo ya kuhara.

Naye Ofisa habari wa mkoa wa Iringa Dennis Gondwe aliwataka wanahabari mkoani hapa kutoa elimu kwa jamii kuhusu mafunzo waliyoyapata katika mafunzo hayo ambapo alisema kwa kupitia waandishi wa habari jamii itapata elimu itakayowasaidia kuweza kuepukana na ugonjwa wa kuhara pamoja na ugonjwa wa kipindupindu.

MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...