Skip to main content

MKOA WA IRINGA UNA KIWANGO KIKUBWA CHA MATUKIO YA UKATILI WA KIJINSIA


 Msanii kutoka Kikundi cha Sanaa cha Mundu Cultural Groups maarufu kwa jina la Mussa Manyoka akionyesha umaili wake wa kucheza na nyoka wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia uliyofanyika katika viwanja vya Mwembetogwa, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa jana.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu (wa tatu kushoto) akipitia hotuba yake kabla ya kuisoma huku wageni wengine wakifuatilia burudani iliyokuwa ikitolewa na Kikundi cha Sanaa cha Mundu Cultural Groups wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia uliyofanyika katika viwanja vya Mwembetogwa, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa jana. (Picha zote na Friday Simbaya)

Mkoa wa Iringa ni mojawapo ya mikoa ambayo ina kiwango kikubwa cha matukio ya ukatili wa kijinsia, kutokana na utafiti uliyofanywa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Shirika la Taifa la Takwimu (NBS) mwaka 2012.

Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa (RAS), Wamoja Ayubu wakati wa uzinduzi siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia uliyofanyika katika viwanja vya Mwembetogwa, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa jana.

Alisema kuwa utatifi unaonyesha kuwa kiwango cha ukatili wa kijinsia katika Mkoa wa Iringa ni asilimia 54, na kuongeza kuwa kiwango hiki ni kikubwa ukilinganisha na wastani wa kitaifa wa asilimia 44.

RAS alisema kuwa utafiti huo unaonyesha kuwa kuwa kuna uhusiano mkubwa kati ya uwepo wa vitendo vya ukatili wa kijinsia na ongezeko la Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi.

“Mkoa wetu wa Iringa ni mojawapo ya mikoa ambayo ina kiwango kikubwa cha maambukizi ya VVU na Ukimwi kwa kuwa na asilimia 9.1 (wanawake 10.9 na wanaume 6.9); na kufanya kuufanya kuwa mkoa wa pili Tanzania kwa kuwa na maambukizi ya VVU na Ukimwi baada ya Mkoa wa Njombe wenye asilimia 14.9 ya maambukizi,” alisema Ayubu.

Alisema kuwa uhusiano wa vitendo vya ukatili wa kijinsia na kuongezeka kwa VVU na Ukmwi ni kutokana na ukweli kwamba vitendo vingi vya ukatili hasa wa kingono vinafanyika bila kutumia kinga, hivyo kuongeza kasi ya maambukizi VVU na Ukimwi.

Kadhalika mila na desturi hatarishi kama kurithi wajane, kuwa na wapenzi wengi, umasikini na ulevi uliopindukia huchangia kwa kiasi kikubwa kutokea kwa ukatili wa kimwili na ukatili wa kingono, hivyo kupelekea kuongezeka kwa VVU na UKIMWI.

Ukatili wa kijinsia ni tatizo linalohitaji kuunganisha nguvu za pamoja kati ya serikali na Asasi zisizo ya kiserikali, madhehebu ya dini, vyama vya siasa na mtu binafsi kwa kuwajibika ipasavyo ili kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia katika Mkoa wa Iringa.

Uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia hufanyika kila mwaka tarehe 25 Novemba, siku 16 za kupinga utakili wa kijinsia hujumuisha Siku ya Ukimwi duniani tarehe 01/12, Siku ya watu wenye ulemavu duniani tarehe 03/12 na Siku ya haki ya haki za binadamu tarehe 10/12 kwa kufanya shughuli mbalimbali yenye lengo la kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Aidha mashirika kama vile USAID, Engender Health, JHPIEGO-SAUTI, AFRICARE, WCS na UNICEF pamoja na maafisa kutoka Idara ya Maendeleo ya Jamii, Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Jeshi la Polisi na mahakama walishiriki katik kuandaa uzinduzi huo dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia mkoani Iringa jana.

Uzinduzi huo wa pamoja pia ulikwenda sambamba na kauli mbiu ya mwaka 2015 ya “FUNGUKA: Chukua hatua mlinde mtoto apate elimu” ilikuweza kuwafikia wananchi walio wengi zaidi.

Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...