Skip to main content

MWAKALEBELA AFUNGUA KESI YA KUPINGA MATOKEO


Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa , Elisha Mwampashi akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo (Picha na Friday Simbaya)


ALIYEKUWA mgombea ubunge Jimbo la Iringa Mjini, Frederick Mwakalebela, kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), amefungua kesi mahakamani ya kupinga matokeo yaliompa ushindi, Mchungaji Peter Msigwa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Kesi hiyo ya uchaguzi iliyofunguliwa kwa No. 5 ya mwaka 2015 imefunguliwa katika mahakama kuu kanda ya Iringa inatarajia kuanza kusikilizwa ndani ya siku 14 tangu kufunguliwa shauri hilo.

Mwakalebela alisema kuwa matokeo yaliyompa ushindi Mch. Msigwa yalikuwa ni ya kutengenezwa ili kumbeba mgombea huyo wa chadema kabla ya kufanyika kwa uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana (leo), Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa , Elisha Mwampashi kwa niaba ya mgombea alisema kuwa mgombea huyu atatumia haki ya kikatiba kupinga matokeo hayo mahakamani ili maoni ya wananchi kuheshimiwa na kupata haki zao za msingi.

Alisema kuwa chama hicho kimewashitaki watu wawili ambao ni msimamizi wa uchaguzi jimbo la iringa mjini pamoja na mshindi katika uchaguzi huo Mch. Peter Msigwa ambapo kila mmoja amewkewa bondi ya shilingi milioni tano.

Hata hivyo katika matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi huo, Ahmed Sawa alimtangaza Mchungaji Peter Msigwa aliyewania ubunge wa jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa mshindi baada ya kuzoa kura 43,154 dhidi ya kura 32,406 alizopata mgombea wa CCM, Frederick Mwakalebela. 

Wagombea wengine na kura zao kwenye mabano ni Chiku Abwao wa ACT Wazalendo (411), Daudi Masasi wa ADC (123), Paulina Mgimwa wa Chausta (66) na Robert Kisinini wa DP (56). 

Hivi karibuni Chama cha Mapinduzi CCM kilitangaza kwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi ya majimbo manne ya Ndanda, Iringa Mjini,Kawe na Mikumi, kutokana na kile ilichodai kuwepo kwa ukiukaji mkubwa wa utaratibu wa uchaguzi, hususan katika kujumlisha matokeo, hali iliyosababisha wabunge wa upinzani kutangazwa washindi.

Chama hicho katika madai yake, kimewatuhumu wasimamizi wa uchaguzi katika majimbo hayo kuvuruga uchaguzi huo kutokana na ilichosema utata uliokuwa umejitokeza wakati wa zoezi la kujumlisha kura na kwamba licha ya chama hicho kuomba kuhesabiwa upya ilinyimwa haki hiyo, ambayo kimsingi iko kisheria.

Hayo yalisemwa na Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM, January Makamba alipozungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam hivi karibuni.

Akizungumzia hilo, January alisema chama hicho hakijaridhishwa na utaratibu wa kukusanya na kujumlisha matokeo kwenye baadhi ya majimbo ya Kawe, Ndanda, Mikumi na Iringa Mjini kutokana na kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa utaratibu wa uchaguzi, hasa katika kujumlisha matokeo uliowezesha wabunge wa upinzani kutangazwa washindi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...