Skip to main content

SHULE YA KIMATAIFA IRINGA YASHAURI MABORESHO KATIKA SEKTA YA ELIMU

















SHULE ya Kimataifa ya Iringa imetoa wito kwa serikali ya Dk John Magufuli kuanzisha mpango maalumu wa uingizaji na utumiaji wa teknolojia mbalimbali mpya kwa maendeleo ya nchi kwa kutoa ufadhili wa elimu kwa makundi mbalimbali ya wanafunzi watakaoplekwa katika nchi zenye teknolojia hizo.

Pamoja na mpango huo, shule hiyo imeiomba serikali hiyo kutumia utajiri wa gesi ya Mtwara kuendelea kuboresha mazingira na mifumo ya utoaji wa elimu nchini ili iwiane na nchi zilizopiga hatua kubwa katika sekta hiyo.

Hayo yalisemwa na mjumbe wa bodi ya shule hiyo, Edwin Port kwenye maadhimisho ya siku ya kimataifa ya shule hiyo yenye wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari zaidi ya 100, yaliyofanyika shuleni hapo juzi.

Mkuu wa Utawala wa shule hiyo, Jean Milliken alisema; “Kwasababu shule yetu ni ya kimataifa, tumekuwa na kawaida kila mwaka kuwa na siku hii, tunasheherekea utaifa wetu kwasababu tunatoka mataifa mbalimbali.”

Milliken alisema kwa kupitia siku hiyo; wafanyakazi, wanafunzi na wazazi na walezi wao hufanya sherehe kwa kuonesha tamaduni za nchi wanazotoka vikiwemo vyakula vinavyoliwa na mataifa hayo na kufanya maonesho mbalimbali yenye maudhui ya kukuza sekta ya elimu nchini.

Akizungumzia sekta ya elimu na matumizi ya teknolojia kwa maendeleo ya Taifa, Port alisema; “nchi inahitaji shule nyingi za vipaji maalumu sambamba na zile za kimataiafa ili zitoe wataalamu wengi kwa faida ya nchi .”

Alisema mazingira ya Tanzania yanaruhusu kufanyika kwa mapinduzi makubwa ya kiuchumi kama uwekezaji wa kutosha utafanywa katika sekta ya elimu.

“Tanzania inaweza kuwa kama Japan ambayo leo imepiga hatua kubwa ya maendeleo duniani baada ya kuwapeleka watu wake katika nchi mbalimbali duniani ambako walijifunza na kurudisha kwao tekenolojia zilizoliofanya taifa hilo liwe moja kati ya nchi zilizoendelea kiviwanda,” alisema.

Alisema wakati Japan ikipeleka watu wake katika nchi zingine zilizoendelea kujifunza tekenolojia za huko haikuwa mzalishaji mkubwa wa magari lakini hivi sasa; magari yake yanauzwa kila nchi duniani.

Alisema Tanzania inaweza kuwa nchi ya viwanda vinavyotokana na matumizi ya tekenolojia zake kama itathubutu kufanya kile kilichofanywa na Japan.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini, Salim Asas alisifia uwepo wa shule hiyo ya kimataiafa mjini Iringa akisema unasaidia kuupaishia mkoa wa Iringa katika utoaji wa elimu ya kimataifa.

Alisema serikali ina kila sababu ya kuzisaidia shule za kimataifa ili zichukue wanafunzi wengi zaidi wa kitanzania lakini pia zivutie wageni toka nje ya nchi.


Asas alisema elimu inayotolewa katika shule za kimataifa ni elimu bora inayowaandaa wanafunzi kushindana kimataifa katika nchi yoyote ile duniani jambo ni sifa na ni maendeleo kwa nchi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...