Skip to main content

CHAVITA wamuomba Rais Magufuli awakumbuke

Rais John Magufuli


CHAMA Cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) Tawi la Mkoa wa Iringa kimemuomba Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuhakiksha kuwa makundi yote maalumu yanapata haki sawa na mengine ili kuondoa dhana ya ubaguzi.

Akiongea na SIMBAYABLOG Katibu wa CHAVITA Mkoa wa Iringa Shaibu Juma ambapo alisema kuwa wanamshukuru Rais John Magufuli kwa kutoa kibali cha kufanya sherehe za siku ya Walemavu kitaifa Mkoani Mwanza.

Alisema kuwa kuna makundi mengine, yamekuwa yakiwezeshwa mara kwa mara aidha kupitia kwa mashirika yasiyo ya Kiserikali na hivyo kuweza kupata maendeleo kwa haraka na kumudu maisha yao ya kila siku.

Juma alisema kuwa katika Kampeni zake za kutafuta Urais Dkt. Magufuli alisema katika utawala wake hatabagua makundi maalum hasa wenye ulemavu katika uongozi wake hali ambayo imeonyesha dhahiri kuwa amedhamiria kuwasaidia.

“Tunampongeza Rais John Magufuli kwa kuchaguliwa kuongoza Taifa la Tanzania na sisi kama makundi ya watu wenye Ulemavu tumeahidi kumpa ushirikiano wa hali ya juu kutokana na utendaji wake wa kazi hali ambayo itasaidia katika kuleta mabadiliko kwa wananchi wake ikiwa ni pamoja na kutekeleza kauli mbio ya “hapa kazi tuu,” alisema katibu hiyo wa CHAVITA.

Aidhi, katibu huyo alielezea masikitiko yake kwa Chama cha Walemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Mkoa wa Iringa kwa kushindwa kuviunganisha vyama vya watu kwenye walemavu mbalimbali mkoani hapa na kumemuomba Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuhakiksha kuwa makundi yote maalumu yanapata haki sawa na mengine ili kuondoa dhana ya ubaguzi.

Alisema tangu kuanzisha kwa tawi hilo la Chavita mkoa wa iringa mwaka 1994 hakijawahi kupata msaada wote kutoka kwa idara ya ustawi wa jamii mkoa, manispaa ya iringa pamoja na SHIVIWATA.

Kwa upande wake mjumbe wa CHAVITA Mkoa wa Iringa Alfred Emmanuel Chengula alisema kuwa ni vema kwa Serikali akangalia makundi kama hayo kwa sasa ili na wao pia wawe na uwezo wa kumudu changamoto nyingi zinazowakumba watu wa makundi ya Wenye ulemavu.

“Ni vema sasa kwa Serikali ya awamu ya tano Chini ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk,John Magufuli kuliangalia kwa jicho la kipekee kundi hilo na kuangalia changamoto mbalimbali zinazolikumba ili kuweza kuwawezesha kiuchumi na kuweza kumudu maisha yao ya kila siku,” alisema Mjumbe huyo.

Mjumbe mwingine aliyeambatana na katibu huyo wa Chavita ni pamoja na Zawadi Boniface aliyehoji kuwa ile asilimia kumi inayotenga na serikali kila mwaka kwa ajili ya watu wenye ulemavu inaenda wapi.

Tarehe 3, Desemba ya kila mwaka ni siku ya Watu wenye Ulemavu duniani. Siku hii inatokana na uamuzi wa Umoja wa Mataifa kui tangaza siku hii kuwa ni siku ya Watu wenye Ulemavu duniani kufuatia Azimio Na. 47/3 la mwaka 1992.

Tanzania kama nchi mwanachama imeridhia na kusaini mkataba huu, na imekuwa ikiadhimisha siku hii kitaifa katika mikoa toufati na mwaka jana maadhisho huyo walifanyika mkoani Iringa.

maadhimisho haya ni kwa lengo la serikali na wadau mbalimbali utambua uwezo wa Watu wenye U lemavu na kujenga mazingira yanayotoa fursa na ushiriki wao katika shughuli mbalimbali za maendeleo hapa nchini.

Kutangazwa kwa siku hii kumelenga kuinua u fahamu wa jamii kuhusu masuala ya Haki za Witu Wenye Ulemavu pamoja na kutoa fursa kwa Serikali za kila nchi duniani kutafakari juu ya utoaji wa huduma endelevu kwa nia ya kuinua hali za maisha ya Watu Wenye Ulemavu. 



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...