Skip to main content

DIWANI WA CHADEMA AUNGA MKONO JITIHADA ZA JPM ZA KUBANA MATUMIZI




IRINGA: Diwani wa Kata ya Gangilonga Jimbo la Iringa Mjini, Dady Igogo (Chadema) pichani ameunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais Dk. John Pombe Magufuli katika kubana matumizi yasiyokuwa ya lazima katika kuhakikisha kuwa fedha zinaelekezwa katika miradi ya kimaendeleo.

Diwani huyo alisema kuwa posho za vikao ni ugonjwa wa ufisadi unalolitafuna taifa hili hususan kwa watendaji wa mashirika ya umma, watendaji wa serikali kuu, wabunge na madiwani.

Akizungumza na SIMBAYABLOG mjini Iringa leo diwani huyo alisema kuwa anayo dhamira ya dhati yakuazimia kutopokea posho za vikao kwa kipindi cha miaka mitano ya utumishi wake, na badala yake posho hizo zielekekezwe kwenye eneo la kusaidia vituo vya watoto yatima.

Alisema kuwa katika kuunga mkono Rais Magufuli wa awamu ya tano ameamua kutopekea posho za vikao kwa kipindi cha miaka mitano ya utumishi wake, na badala yake pesa hiyo zisaidie watoto yatima kwenye Kata ya Gangilonga.

Alisema kuwa suala hilo tayari amewasilisha kwenye kamati ya maendeleo ya kata ya Gangilonga ambapo lilipokelewa, na hatimaye iliundwa kamati itakayokuwa ikiratibu posho hizo ambao ni; mwenyekiti wa mtaa wa kichangani, mwenyekiti wa mtaa kinondoni na mtendaji mmoja wa mtaa.

“Naamini kuwa udiwani siyo kazi ya ajira, bali ni kazi ya utumishi kwa wananchi waliokuamini na pia kuwa miongoni mwa majukumu ya udiwani ni pamoja na kukaa vikao,” alisisiza.

Alisema kuwa halmashauri ya manispaa ya iringa asilimia 34 ya mapato yake inategemea serikali kuu pamoja na wahisani kwa vilie uwezo wake ni shilingi bilioni nne (4bn/-)tu makusanyo ya ndani (own source), sawa ni asilimia 16.

Alisema kuwa ili halmashauri iweze kujitegemea kimapato ni lazima itafute vyanzo vya mapato mbadala ili ni pamoja na kupunguza matumizi ya siyo ya lazima.

Alisema kuwa wastani wa posho za madiwani na watendaji kwa mwaka mmoja katika manispaa ya iringa ina uwezo wa kusomesha wanafunzi zaidi ya 4000 wa shule za sekondari.

“Nikiwa sehemu ya historia hii muhimu ya kuwa diwani wa kwanza Tanzania kukataa posho, naomba ni kuchukuwa fursa hii kuwaomba madiwani wenzangu pamoja mbunge wa iringa mjini, na mbunge viti maamlumu wa iringa kuwa sehemu ya kupinga uendelezaji wa posho zisizokuwa za msingi, ” alisema diwani huyo.

Alisema pia ni msimamo wa chama chake katika ilani yake ya uchaguzi kwa mwaka 2010 na ilani ya mwkan2015 ya kutaka posho ya kitako au vikao iweze kuftwa.

Kata ya Gangilonga ina idadi ya kaya 2,490, idadi ya watu 9,599 na ina vituo viwili vya watoto yatima ambavyo ni Upendo na Matumaini. (NA FRIDAY SIMBAYA)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...