Skip to main content

KIGWANGWALLA ATEMBELEA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA KANDA YA KUSINI



Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ligula ya mkoa wa Mtwara, Dkt. Shaibu Maarifa (katikati) akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla (kushoto) alipotembelea eneo la Mikindani inapojengwa hospitali ya mpya ya kanda ya kusini, mkoani Mtwara.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akimuuliza swali Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ligula ya mkoa wa Mtwara Dkt. Shaibu Maarifa (katikati) wakiwa eneo la Mikindani inapojengwa hospitali ya mpya ya kanda ya kusini, mkoani Mtwara.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Kigwangalla (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ligula ya mkoa wa Mtwara, Dkt. Shaibu Maarifa (kushoto) inapojengwa hospitali ya mpya ya kanda ya kusini inayojengwa eneo la Mikindani mkoani Mtwara. 



Muonekano wa moja ya majengo ya Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini itakayohudumia mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma inayojengwa eneo la Mikindani mkoani Mtwara.(Picha na Eleuteri Mangi- MAELEZO).

Na Mwandishi wetu, Mtwara

UJENZI wa hospitali ya rufaa Kanda ya Kusini, unaofanyika mkoani Mtwara sasa upo katika majengo ya wagonjwa wa nje (OPD).

Ujenzi huo ulioanza mwaka 2009 kwa kusafishwa kwa eneo na kujengwa kwa uzio wa kilomita 2.7 mwaka 2011 kwa gharama ya shilingi milioni 840 na kuanza kujengwa kwa majengo ya OPD mwaka 2013 umelenga kuwezesha mikoa ya Kusini kuwa na hospitali kubwa yenye hadhi ya kisasa.

Akisoma taarifa ya maendeleo ya ujenzi kwa Naibu Waziri katika wWizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dkt. Hamisi Kigwangalla, Mganga Mkuu wa mkoa wa Mtwara alisema kwamba ujenzi wa mapokezi umetarajiwa kutumia shbilioni 4.8 na hadi sasa wametumia bilioni 1.8

Mganga huyo alisema mradi mzima unatarajiwa kujengwa kwa bilioni 78.

Alisema kuchelewa kuendelea japo sasa wana ghorofa 2 zilizoezekwa na wanapiga ripu kunatokana na upatikanaji wa fedha kutoka serikali kuu.

Alisema hospitali hiyo ni muhimu sana kukamilika kutokana na kukua kwa uchumi wa Mtwara na mikoa jirani na pia kuwapo kwa uhitaji kwa mikoa ya kaskazini mwa nchi jirani.

Naye Naibu Waziri Kigwangwalla alisema kwamba ni matumaini yake kuwa hospitali hiyo itakamilika mapema na kubakiza changamoto za matumizi ya wananchi kutoka nchi jirani ambao kwa sasa wanafaidika sana na hospitali ya Ligula.

Alisema wataalamu wanatakiwa kuangalia hali hiyo ili kuwepo na matumizi sahihi ya miundombinu hiyo iliyolenga kufaidisha wananchi wa Tanzania.

Aidha akiwa Mtwara Naibu Waziri huyo aliendelea kusisitiza watumishi wote kuwajibika na kuwahi maeneo yao ya kazi.

Alisema watumishi wa umma wanaofikia laki nne wamepata nafasi adimu ya kuutumikia umma wa watu takribani milioni 50 na hivyo ni lazima waheshimu watanzania kwa kuwatumikia ipasavyo.

Alisema wao waliomba nafasi ya kuhudumia watanzania kwa hiyo ni lazima wawahudumie watanzania na kila mmoja katika kitengo chake ni lazima kuhakikisha watumishi wanafanya kile walichoahidi katika mikataba yao.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...