Skip to main content

MAHAKAMA YAFUTA KESI YA KUPINGA UBUNGE WA KUBENEA



MAHAKAMA Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam, imefuta kesi ya madai ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Ubungo.

Kesi hiyo ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Didas Masaburi dhidi ya mbunge wa jimbo hilo, Saed Kubenea (CHADEMA).

Uamuzi wa maombi ya kufuta kesi hiyo uliwasilishwa mahakamani hapo juzi na wakili wa Dk. Masaburi, Clement Kihoko mbele ya Jaji Lugano Mwandambo.
Wakili Kihoko alisema kuwa mteja wake hana nia ya kuendelea na usikilizwaji wa kesi hiyo ya kupinga matokeo.
Baada ya kuwasilisha maombi hayo, Jaji Mwandambo alisema mahakama imepokea maombi hayo ya kuifuta kesi hiyo.

GHARAMA

Baada ya jaji kukubali ombi hilo, Wakili Kihoko aliiomba mahakama kuwapunguzia gharama za uendeshwaji wa kesi ya msingi pamoja na fidia ya usumbufu.
Hata hivyo, Wakili wa Kubenea, Nyaronyo Kicheere, alisema licha ya upande wa utetezi kuomba punguzo hilo, lakini wanapaswa kulipa gharama hizo.

Kutokana na hali hiyo, kuliibuka mvutano wa sheria, jambo lililomlazimu Jaji Mwandambo kuahirisha kesi hiyo kwa muda mfupi, aweze kupitia hoja hizo kabla ya kurudi mahakamani.
Baada ya kurudi, Jaji Mwandambo alisema katika kesi ya msingi mdai anatakiwa kulipa asilimia 50 ya gharama zote za uendeshaji wa kesi hiyo.
Alisema katika maombi ya punguzo la uendeshaji wa kesi hiyo, kila upande utalipia gharama zake.

KUBENEA ANENA
Akizungumza baada ya kutoka mahakamani, Kubenea aliwashukuru wanachama wa Chadema kumsindikiza mahakamani wakati kesi hiyo ikiendelea.
Hata hivyo, alisema kitendo cha Dk. Masaburi kufuta kesi hiyo kinaonyesha wazi kuwa yeye ni mshindi na ataliongoza jimbo hilo katika miaka mitano.
“Wagombea wengine waliofungua kesi kama ya Dk. Masaburi wakati hawana uhakika wa kushinda wanapaswa kuzifuta ili waendelee na kazi nyingine,” alisema Kubenea.

Dk. Masaburi alifungua kesi hiyo namba 8 /2015 kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu kwa mbunge wa Ubungo, Kubenea akidai kuwa yeye na mawakala wake hawakuruhusiwa kuona vifaa vya kupigia kura kama ilivyofanyika kwa Kubenea na mawakala wake.
Vilevile alidai Kubenea alitoa rushwa ya jenereta katika Hospitali ya Mavurunza iliyopo Kimara, zawadi ya meza ya mchezo wa pool kwa vijana wa Makuburi na kujenga barabara ya Matete huko Kimara akiwashawishi kumchagua.

Dk. Masaburi pia alimlalamikia msimamizi kukataa kuhakiki kwa mara ya pili matokeo yake ikiwamo na watu kadhaa wa maeneo ya Mizizini, Mianzini, Kilimahewa, Mizambarauni, Shule ya Mugabe na Kanuni, kutokupiga kura.
Pamoja na Kubenea, washtakiwa wengine katika kesi hiyo walikuwa ni Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Ubungo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Mawakili wengine kwa upande wa Kubenea walikuwa Tundu Lissu, Mabere Marando, Peter Kibatala, Method Kimomogolo na Frederick Kihwelo. Chanzo: MTANZANIA

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...