Skip to main content

UNODC YAKABIDHI VIFAA VYA MAABARA JESHI LA MAGEREZA




Afisa Mipango wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC), Immaculata Nyoni akizungumza jambo kabla ya kukabidhi vifaa vya maabara kwa Jeshi la Magereza nchini.





Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akizungumza jambo wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa vifaa vya maabara kwa Magereza Tanzania.

Afisa Mipango wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC), Immaculata Nyoni pamoja na Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa wakikata utepe kuashiria kukabidhiwa vifaa vya maabara vilivyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC).





Afisa Mipango wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC), Immaculata Nyoni akitolea ufafanuzi vifaa vya maabara alivyokabodhi kwa Jeshi la Magereza ili kusaidia kuwapima wafungwa walioko magerezani.





Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa akitoa shukrani baada ya kupokea msaada kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) lililowakilishwa na Immaculata Nyoni.




Hivi ndivyo vifaa vya maabara vilivyokabidhiwa kwa Jeshi la Magereza.




Picha ya pamoja.




Na Mwandishi wetu

Jeshi la Magereza Ukonga limepokea vifaa vya maabala kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) ambavyo vitasaidia kutoa vipimo kwa wafungwa waliofungwa magerezani hii ikiwa ni jitihada za kupunguza matumizi ya dawa za kulevya katika magereza hapa nchini.
 
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Bi. Immaculata Nyoni ambaye ni Afisa Mipango wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) alisema wametoa msaada huo baada ya kufanyika kwa tafiti hasa kwenye magereza hapa nchini na utafiti huo Magereza ilishirikiana na UNODC na kubaini changamoto wanazozipata wafungwa wakati wa kupimwa afya zao. 
Hivyo kama shirika limeamua kutoa msaada wa vifaa vya maabala ambavyo ni Hematology mbili(2), Urine Analyzer tatu (3) pamoja na Hemoglobin Mashine mbili(2) na vifaa hivi vimegharimu takribani shilingi milioni 10 za kitanzania.
 
Akitoa shukrani Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza nchini, Dkt. Juma Malewa kwa niaba ya Mkuu wa Magereza hapa nchini amesema anawashukuru UNODC kwa kuona matatizo yanayowakabili hasa kwenye hospitali za Magereza zinazohudumia wafungwa na kuamua kutoa msaada huo kwa jeshi hilo.
 
Pia alisisitizaushirikiano kati ya Jeshi la Magereza pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na Dawa za Kulevya na Uhalifu (UNODC) kuimarishwa ili kuweka ukaribu kwa kila jambo linalohusu afya ya wafungwa hasa kwa wale waliokuwa wanatumia madawa ya kulevya na wenye virusi vya UKIMWI.
 
Baada ya wauguzi kupokea msaada huo walisema sasa ni muda wa kazi tu kwani wamepata vifaa ambavyo vitaweza kuwahudumia wagonjwa kwa wakati kwani hapo mwanzo kulikuwa na uhaba wa vifaa vya maabara na kupelekea matibabu kutokuwa ya uhakika katika hospitali za Magereza zinazohudumia wafungwa.










Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...