Skip to main content

WANAFUNZI 15,312 MKOANI IRINGA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWA KWANZA 2016

PICHA NA MAKTABA



IRINGA: Ufaulu wa wanafunzi waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi (PSLE) mwaka 2015 mkoani Iringa umeongezeka ukilinganisha na mwaka jana, ambapo ufaulu kwa mwaka huu ni asilimia 73.25, wakati mwaka jana ulikuwa ni asilimia 68.58, sawa na ongezeko la asimilia 4.67.

Hayo yalisemwa na Afisa Elimu Taaluma wa Mkoa wa Iringa, Euzebio Mtavangu hivi karibuni wakati akitoa taarifa ya mwelekeo wa matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi 2015 kwa wajumbe wa kamati ya uchaguzi wa mkoa wa kuchagua wanafunzi wataojiunga kidato cha kwanza mwaka 2016.

Alisema kuwa kuongezeka kwa ufaulu mwaka huu mkoani Iringa ni kutokana na utekelezaji mzuri wa mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN) ulioanzisha na serikali hivi karibuni.

Alisema kuwa wanafunzi waliofaulu mwaka 2015 ni 15,311 (7,163 wavulana na 8,148 wasichana) ambapo wanafunzi wote waliofaulu mwaka huu wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2016.

Katika mwaka 2014 matokeo ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kumaliza elimu ya msingi walikuwa ni wanafunzi 14,650 (6,835 wavulana na 7,815 wasichana).

Mtavangu aliongeza kuwa kwa mwaka 2015 wanafunzi 413 (258 wavulana na 155 wasichana) ambao ni asilimia mbili hawakufanya mtihani wakilinganishwa na 177 (109 wavulana na 68 wasichana) ikiwa ni asilimia moja kwa mwaka 2014.

“Sababu za wasiofanya mtihani ni utoro, vifo, ugonjwa, mimba na kuhama. Idadi ya utoro kwa wanafunzi mwaka huu ni kubwa ukilinganisha na mwaka jana, ambapo mwaka 2015 utoro ulikuwa ni wanafunzi 399 wakati mwaka 2014 utoro kwa wanafunzi ulikuwa ni 158,” alisema.

Mtihani wa kumaliza elimu ya msingi ulifanyika tarehe 09-10 Septemba 2015 nchini kote.

Aidha, alisema kuwa shule za msingi 467 kati ya shule 491 ndio zilizokuwa na watahiniwa wa mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kwa mwaka 2015 mkoani Iringa.

Mtavangu alisema kuwa watahiniwa waliofanya mtihani na kumaliza elimu ya msingi 2015 wanaendelea kujibu maswali ya mitihani kwa kutumia fomu za ‘Optical Mark Reader’ (OMR).

Alisema kuwa matumizi ya fomu za OMR yalianza mwaka 2012 na lengo la kutumia OMR ni kusoma moja kwa moja kwa kompyuta majibu ya mtahiniwa kutoka katika karatasi yake ya majibu na kuokoa muda wa usahihishaji.

Takwimu za watahiniwa waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2015 ni wanafunzi 20,905 (9,612 wavulana na 11,293 wasichana) na waliofaulu ni jumla ya wanafunzi 15,311 (7163 wavulana na 8148 wasichana), sawa na asilimia 73.25.

Hata hivyo, kiwango cha kumaliza elimu ya msingi (completion rate) mkoani Iringa kimeongezeka kutoka asilimia 77.2 (2014) hadi kufikia asilimia 81.1 (2015).

Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa Mkoa ya kuchagua wanafunzi wataojiunga kidato cha kwanza mwaka 2016 alikuwa ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa (RAS), Ayubu Wamoja.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...