Skip to main content

Wananchi wa kijiji cha Lyamko wamepatiwa hati miliki za kimila 350







WANANCHI wa kijiji cha Lyamko kilichopo katika Kata ya Bomalang’ombe Wilayani Kilolo wamepatiwa hati miliki za kimila 350 baada ya kupimiwa mashamba yao na shirika linalojishughulisha na masuala ya ardhi nchini (HakiArdhi) kwa kushirikiana na halmashauri hiyo.

Akizungumza kijijini hapo juzi mara baada ya wananchi hao kupatiwa hati miliki zao, Ofisa Ardhi Mteule Elinaza Kiswaga alisema kuwa kijiji hicho kimekuwa kijiji cha nane ndani ya wilaya hiyo kupatiwa hati miliki za kimila tangu zoezi la upamaji mashamba kuanza mwaka 2013. 

Kiswaga alisema kuwa taasis ya haki ardhi ilianza kufanya kazi za utafiti wa awali mwaka 2012, na mwanzoni mwa mwaka 2013 taasisi hiyo kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya hiyo ilianza rasmi kutoa mafunzo ya sheria ya ardhi, utawala vijijini na mabadiliko ya tabianchi.

Kiswaga alisema kuwa lengo la mradi ulikuwa ni kutoa uelewa mpana kwa jamii juu ya sheria ya ardhi, utawala vijijini na mabadiliko ya tabianchi hususani kwa wazalishaji wadogo.

Naye Ofisa ardhi mteule wa wilaya hiyo alisema kuwa taasisi hiyo ya hakiardhi ilitoa mafunzo ya sheria ya ardhi na utawala vijijini pamoja na mabadiliko ya tabianchi katika vijiji 55, kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi kwa vijiji 11 ambavyo ni Kihesamgagao, Kidabaga, Kiwalamo, Kitelewasi, Kipaduka, Uhambingeto, Lugalo, Lyamko, Ibofwe, Itonya na Ilamba.

Kwa upande wake Mejuzi Mgeveke ambaye ni makamu mwenyekiti wa halmashauri ya kilolo aliishukuru taasisi hiyo kwa kuendesha shughuli hizo katika wilaya ambazo zimeleta mafanikio makubwa.

“Ni dhahiri kuwa mafunzo hayo yamesaidia kuleta chachu ya mabadiliko kwa jamii ya watu wa kilolo katika ngazi zote hasa juu ya uelewa wa masuala ya ardhi, utawala bora na mabadiliko ya tabia nchi.”alisema Mgeveke

Hata hivyo mkurugenzi mtendaji wa haki ardhi Yefred Myenzi, amesema katika utekelezaji wa shughuli hizo kumekuwepo na mafanikio makubwa ambayo ameshuhudia vijiji 11 kuandaliwa mipango ya matumizi bora ya ardhi, kiasi ambacho kimesadia kupunguza migogoro mingi ya ardhi.

Myenzi alisema kuwa migogoro hiyo ni ile inayotokana na mwingiliano wa matumizi baina ya uhifadhi wa misitu asili.

Alisema kuwa taasisi ya hakiardhi imefanyika na kufika vijiji 55 kati ya zaidi ya vijiji 106 vya wilaya hiyo na bado mwamko ni mkubwa kwa wananchi wa wilaya hiyo kutakifiwa na zoezi la upimaji mashamba.

“Hivi Kwa mfano, katika kijiji cha Lyamko kililengwa kupima mashamba 350 lakini wananchi waliojitokeza kwa wingi kiasi cha kufikia wananchi 351 na wengine ilishindikana kupimiwa na tutajitahidi hadi kuwafikia wote na kuwapimia.”alisema Myenzi

Maria Nzala alisema kuwa mume wake alikuwa hataki yeye kumiliki ardhi lakini ameweza kutafuta haki yake na kuipata kisawasawa,hivyo haki ya kumiliki ardhi kwa wanawake imetambuliwa na imeanza kutekelezwa kwa vitendo,pia itasaidia kuondoa migogoro baina ya wanaumeambao hawataki wanawake kutumia ardhi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...