Skip to main content

WAWILI WAFARIKI KATIKA AJALI YA GARI ILIYOBEBA MAGAZETI YA MWANANCHI





GARI iliyokuwa imebeba magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti ikitokea Dar es Salaam kuelekea Iringa na Mbeya, imepata ajali katika mlima wa Kitonga, wilayani Kilolo mkoani Iringa leo alfajiri.

Watu wawili wamekufa papo hapo na wengine sita kujeruhiwa, mmoja vibaya baada ya gari lililokuwa likisafirisha magazeti ya mwananchi kutoka Dar es Salaam kwenda Iringa na Mbeya kupata ajali eneo la mlima kitonga barabara kuu ya Dar-es-Salaam-Iringa.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa polisi Mkoa wa Iringa Ramadhan Mungi alisema ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 11 alfajiri gari hilo la magazeti kuingia nyuma ya roli likiwa katika mwendo kasi.

“Leo imetoka ajali mbaya sana hapa Iringa, ajali hiyo ilihusisha gari aina ya Haice iliyokuwa imebeba magazeti ya Kampuni ya Mwananchi Communication LTD; gari hilo lilipata ajali baada ya kuganga lori lenye tela kwa nyuma:

“Dereva wa gari hilo lililopata ajali alitaka kulipita roli ambalo nalo lilikuwa linaelekea Mbeya; alipokuwa akitaka kulipita aliona gari likija mbele yake na wakati akifanya maamuzi ya kurudi upande wake aligonga roli hilo kwa nyuma,”alisema.


Mungi aliwataja waliopoteza maisha katika ajali hiyo kuwa ni Eliud Ogwasa (40) na Godfrey Owino (34) wote wakazi wa mkazi Dar es Salaam.

Aliwataka majeruhi kuwa ni Baraka Shitindi (32) ambaye hali yake ni mbaya na Kevin Shitindi (30) wakazi wa Mbozi Mkoani Mbeya na Herold Shitindi (25) mkazi wa Morogoro.

Wengine ni Zabroin Izote (29) mkazi wa mbeya na Joseph Kayani (37) mkazi wa Mafinga mkoani Iringa.

“Kamanda Mungi aliwaasa madereva kuwa makini na kuendesha gari kwa kuzingatian sheria za barabarani ili kuepuka ajali zinazoweza kuwapotezea maisha wao na abria wao,” alisema.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Iringa, Alfred Mwakalebela alisema wamepokea maiti mbili ambazo wamehifadhi kwenye chumba cha kuhifadhia maiti hospitalini hapo.

Dkt. Mwakalebela alisema pia wamepokea majeruhi wanne ambao wameumia maeneo mbalimbali mwilini ikiwemo kuvunjika mguu huku mmoja kati yao akiwa na hali mbaya zaidi kiasi cha kushindwa kuzungumza.

Majeruhi Kevin Shitindi ambaye ameumia mkono na kifuani alisema walitoka Dar es Salaam saa sita usiku wakiwa 10 kwenye gari hiyo na walipofika Morogoro saa nane watu wawili walishuka.

Majeruhi Kayani na Lisote walisema hiace hiyo ilikuwa inakwenda kasi na wakati ajali inatokea wao walikuwa wamelala walichosikia ni kishindo na baadaye kuona madereva wamekufa papo hapo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...