Skip to main content

SERIKALI KUTOA BURE MBEGU ZA MTAMA KWA WENYE UPUNGUFU WA CHAKULA


Mkurugenzi wa Idara ya Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Brigedia Jenerali Mbazi Msuya amewataka wananchi waliokumbwa na uhaba wa chakula nchini kufuata ushauri wa wataalam kwa kupanda mimea inayostahimili ukame ikiwemo mtama na uwele ili kuondokana na adha hiyo kila mwaka. 

Akizungumza jana na wananchi wa vijiji vya Iguluba na Mkulula vilivyopo kata ya Malenga Makali, Tarafa ya Isimani ambayo imeathirika zaidi na upungufu wa chakula wilayani Iringa, Brigedia jenerali Msuya amesema serikali itawapatia wananchi hao mbegu za mtama za bure ili wapande msimu huu.

Mkurugenzi wa Idara ya Maafa amefuatana na ujumbe wake kutathmini hali ya upungufu wa chakula wilayani Iringa na kujiridhisha na ugawaji wa msaada uliotolewa na serikali na kujua ni maeneo gani yanahitaji msaada zaidi.

Brigedia Jenerali Msuya anawahakikishia wananchi kuwa hakuna mwananchi atakayekufa kwa njaa.

Wakielezea hali halisi ya upungufu wa chakula wananchi wameishukuru serikali kwa kupelekea chakula lakini wakaomba kujengewa mabwawa ya umwagiliaji, maghala ya kuhifadhi chakula pamoja na mbegu zinazostahimili ukame.

Brigedia Jenerali Msuya na timu yake pia, wameshuhudia zoezi la ugawaji wa chakula kwa kaya zilizokumbwa na upungufu ukiendelea katika kijiji cha Igingilanyi na kusema kuwa serikali inatambua chakula hicho hakitoshelezi mahitaji yote.

Zaidi ya watu elfu 76 wilayani Iringa wanakabiliwa na upungufu wa chakula uliosababishwa na mvua chache zilizonyesha msimu uliopita.


Wiki mbili iliyopita serikali ilitoa tani 200 kwa kaya zilizokubwa na njaa kutokana na ukame.
 #####################################

IRINGA: Director of the Department of Disaster from the Office of the Prime Minister, Brigadier General Mbazi Msuya has urged citizens affected by food shortages in following the advice of experts to plant drought resistant crops including sorghum and millet to overcome the persecution every year.

Speaking yesterday to citizens at Iguluba and Mkulula villages in Malengamakali Ward, Isimani Division which is most affected by food shortages in Iringa district, Brigadier General Msuya said the government will give the citizens sorghum seeds free to plant into this season.

Director of the Department of Disaster his delegation came to assess the state of food insecurity in Iringa district, Iringa Region and assurance and distribution of the support given by the government to know what areas need more support.

Brigadier General Msuya he assured the public that no citizen will die of hunger.

Explain the real situation of food insecurity, citizens have thanked the government for giving them food but asked the government to build up dams for irrigation, food storage facilities and provide them with drought-resistant seeds.

Brigadier General Msuya and his team have also witnessed the distribution relief food to the households affected by food shortage in the Igingilanyi village and said the government is aware that food was not enough to cover all needs.

Over 76 thousand people Iringa District faced with food shortages caused by low rainfall last season.


Two weeks ago the government brought 200 tons of relief food to affected households in the villages of Isimani Division, Iringa district.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...