Skip to main content

DK. KIGWANGALLA ADHURU KAMBI YA WAGONJWA WA KIPINDUPINDU YA IRINGA


Eneo la vijiji vya Pawaga linavyoonekana kwa picha za angani wakati wa Naibu Waziri, Dk. Kigwangalla alipo dhuru kwa kutumia Chopa.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangallla amekuwa kiongozi wa kwanza wa ngazi za juu kufika katika eneo lililokumbwa na mafuriko katika vijiji vya Mbolimboli, Tarafa ya Pawaga iliyopo Iringa vijijini Mkoani hapa ambapo mbali na kutoa pole pia ameweza kutoa huduma za kitabibu kwa baadhi ya watu waliozidiwa waliokuwa bado hawajaokolewa.

Awali Dk. Kigwangalla alipodhuru kwa wananchi waliopo kwenye kambi ya muda baada ya kunusurika na mafuriko hayo, aliwaeleza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao bega kwa bega kwani Serikali ya "Hapa Kazi Tu" haina ngoja ngoja ndio maana yeye ameweza kufika haraka kuakikisha wananchi wapo salama na wanapatiwa huduma zote za msingi na za kijamii ikiwemo matibabu na elimu ya kijikinga na milipuko ya magonjwa ikiwemo magonjwa ya kipindupindu ambacho kimewakumba wananchi hao.

Dk. Kigwangalla ameweza kufanya hilo baada ya Chopa iliyokuwa ikimtembeza angani kufika katika maeneo yaliyozingirwa, alimuru rubani wake kushusha chini na kisha kutoa msaada wa haraka kwa akina mama na watoto waliokuwa wamezingirwa kwenye moja ya maeneo hayo zaidi ya siku tatu bila kuokolewa ambapo alitoa huduma na kisha Chopa hiyo iliwabeba hadi katika eneo maalum waliopo wahanga wengine waliookolewa.

Pia Dk. Kigwangalla aliweza kutoa elimu na maelekezo mbalimbali kwa wahanga hao kujiepusha na masuala ya kutumia mahitaji salama ilikuepukak kipindupindu kisienee zaidi kwani hadi sasa eneo hilo limeweza kupatikana wagonjwa wa ugonjwa huo zaidi ya 220 huku hadi wanatembelea katika kambi ya Mtakatifu Lucas iliyopo Pawaga, ilikuwa na wagonjwa zaidi ya 40.

Imeandaliwa na Magreth Kinabo–MAELEZO, Andrew Chale, modewjiblog-Iringa

Naibu Waziri, Dk. Kigwangalla alipo dhuru kwa kutumia Chopa katika eneo lililokumbwa na mafuriko hayo kijiji cha Mbolimboli

Baadhi ya wananchi waliookolewa baada ya Naibu Waziri, Dk.Kigwangalla kuamuru wawaishwe katika kambi waliopo wahanga wengine.


Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akipewa maelezo namna wanawake hao pamoja na watoto wao wadogo walivyoweza kuzingirwa na maji kwa muda wa siku tatu bila kuwa na huduma muhimu ambapo hata hivyo, Naibu Waziri aliweza kuwasaidia ikiwemoo kuamuru Chopa hiyo iwapeleke kwenye kambi maalum na kisha wao kubaki hapo kabla ya kurudiwa tena na kuendelea na safari ya Kambi ya watu wa Kipihdupindu.

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akipata maelezo ya mmoja wa waokoaji wanaotumia boti maalum namna walivyoweza kupata taabu jinsi ya uokoaji katika eneo hilo.

Baadhi ya wahanga wa mafuriko wa vijiji vya Mbolimboli katika Tarafa ya Pawaga wakipata maji maalum yenye dawa ilikujikinga na ugonjwa wa kipindupindu ambao hata hivyo umeenea katika eneo hilo kutokana na maji yake kuchafuliwa na vinyesi vya vyoo vilivyokumbwa na mafuriko.

Naibu Waziri, Dk.Kigwangalla akisisitiza wahanga hao wa mafuriko kuakikisha wanatumia vyakula na vitu vingine kwa hali ya usafi ilikueupuka ugonjwa huo wa kipindupindu.

Baadhi ya akina mama wakipanda Chopa baada ya Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla kuamuru wapelekwe kwenye kambi haraka kutokana na watoto waliokuwa nao kuzidiwa (wanawake hao wanaoonekana pichani ndani ya chopa).

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa wakiwa katika Chopa juu wakiangalia namna mafuriko hayo yalivyosababisha athari kubwa na kufanya kuwa kisiwa katika vijiji hivyo vya Mbolimboli.

eneo la chini linavyookena kutokana na mafuriko hayo.

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akioneshwa moja ya maeneo namna maji yake yalivyochafuliwa na kinyesi baada ya vyoo kuharibiwa na mafuriko hayo.

Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Naibu Waziri, Dk. Kigwangalla (hayupo pichani) wakati alipofika katika eneo lililokuwa akina mama hao na watoto ambao wamekaa siku tatu bila kupata huduma muhimu.

Pichani ni baadhi ya akina mama na watoto ambao walikwama kwa zaidi ya si tatu kwenye mafuriko hayo huku wakishindwa kupata mahitaji muhimu ambapo pia vifaa vya uokoaji na waokoaji kushindwa kuwafikia ambapo hata hivyo Naibu Waziri wa Afya. Dk. Kigwangalla alipoamuru Chopa iliyokuwa ikipita kuangalia athari hizo kushuka kisha kuwachunguza na kupelekwa kwenye kambi maalum.

uokoaji ukiendelea..


Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, wakielekea katika kambi ya wahanga hao wa mafurikoeneo la Itunundu..

Baadhi ya watoto wakiwa katika eneo la kambi ya wahanga ambao wengi wao wamekimbia kwenye maeneo hayo yaliyokumbwa na mafuriko.

Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akisaidiana na mmoja wa watoa huduma baada ya mtoto huyo kuzidiwa katika kambi hiyo maalum.

Kambi maalum inayohudumiwa wagonjwa wa kipindupindu lililo eneo la Mtakatifu Lucas

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...