Skip to main content

DUNIA YAAGIZWA KUMALIZA UKEKETAJI 2030



WATENDAJI wakuu wa mashirika mawili makubwa ya Umoja wa Mataifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA) na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia watoto (UNICEF) wametoa wito kwa dunia kujipanga vyema kumaliza kabisa tatizo la ukeketaji (FGM) ifikapo mwaka 2030.

Katika kauli zao walizotoa katika taarifa ya pamoja iliyotolewa na ofisi ya Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa mjini Dar es salaam watendaji hao Mkurugenzi Mtendaji wa UNFPA Dk. BabatundeOsotimehin, na Mkurugenzi Mtendaji wa UNCEF, Anthony Lake, wamesema ipo haja ya dunia kuadhimisha siku hiyo kwa kulenga kuwa na kiwango sifuri katika vitendo vya ukeketaji.

Mashirika hayo ya Umoja wa Mataifa yamesema kwamba ukeketaji ni vitendo vya kikatili vinavyowanyima wanawake haki yao ya msingi na kuwazuia kuchanua inavyostahili kama wanawake.

Viongozi hao wamesema kwamba vitendo vya ukeketaji vimesambaa duniani kote kuanzia Afrika, Mashariki ya Kati ambako imekuwa kama vitu vya kawaida vikiathiri pia familia katika nchi za Asia Australia, Ulaya, Amerika ya Kaskazini na Kusini.

Wamesema kwamba kama hatua zisipochukuliwa kutokomeza ukeketaji idadi ya mabinti na wanawake wanaoweza kuingizwa katika mkumbo huo itakuwa inaongezeka ikiwapeleka katika mzunguko ule ule wa kushamirisha ukeketaji na kurejesha nyuma maendeleo ya wanawake na binadamu kwa ujumla kama familia.

“ Ili kuhami utu wa mwanamke, tunahitaji kuchukua hatua sasa na kuwajibika kama dunia kutokomeza ukeketaji. “ ilisema sehemu ya taarifa ya viongozi hao kwa vyombo vya habari.

Septemba mwaka jana katika mkutano wa kutengeneza mpango wa kimataifa wa maendeleo endelevu, nchi 193 zilikubaliana kuhakikisha kwamba ukeketaji unakuw aumetokomezwa ifikapo mwaka 2030.

Taarifa hiyo imesema kwamba ili kufanikiwa wananchi wanatakiwa kushawishi familia nyingi duniani hapa kuachana na tabia ya ukeketaji.

“Tunahitaji kufanyakazi na idadi kubwa ya wataalamu wa tiba katika jamii zetu – wakiwemo waganga wa jadi na wataalamu wa kisasa wa matibabu, tukiwashawishi wakatae kutoa huduma ya ukeketaji.” Ilisema taarifa hiyo.

Aidha taarifa hiyo hiyo imetaka wanawake waliofanyiwa ukeketaji kusaidiwa huduma mbalimbali zikiwamo za kisaikolojia na nyingine zinazostahili ili kuwapunguzia maumivu waliyoyapata na wanayoendelea kuyapata kutokana na kukeketwa.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...