Skip to main content

HOYCE TEMU: MISS TANZANIA ALIYEJITOA KUSAIDIA WATANZANIA KUPITIA KIPINDI CHA MIMI NA TANZANIA




Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akimlisha chakula Narsa Ramadhan (2) akiwa na mama yake Tatu Saleh (kushoto) wakati wa hafla ya chakula kilichondaliwa kwa watoto na wazee wanaoishi katika makazi ya wazee na watu wenye ulemavu wasiojiweza yaliyopo Nunge, Kigamboni, jijini Dar es Salaam ikiwa ni mojawapo ya shughuli ya kijamii kuuaga mwaka 2015 na kukaribisha mwaka mpya 2016.(Imeandaliwa na Modewjiblog)

Licha ya kuvaa taji la ulimbwende, Miss Tanzania 1999, Hoyce Anderson Temu amekuwa mfano wa kuigwa kwa walimbwende waliopita wa taji hilo nchini kwa kujitoa kusaidia jamii ya Tanzania kwa kutumia nafasi aliyonayo nchini.

Hoyce ambaye ni mzaliwa wa Arusha amekuwa mstari wa mbele kusaidia Watanzania ambao wanamatatizo mbalimbali kama ya kiafya na elimu ambapo amekuwa akitoa misaada na muda mwingine kutafuta wadhamini ili kusaidia jamii ambayo ameifikia kwa muda huo.

Baadhi ya mafanikio ambayo yamepatikana kupitia kipindi cha Mimi na Tanzania ni pamoja na kupeleka wagonjwa nje ya nchi kwa ajili ya kupata matibabu akiwepo mtoto Hamisi ambaye alimsaidia kwenda kupata matibabu ya mguu wake.

Kupitia kipindi chake cha Mimi na Tanzania kinachorushwa upitia Channel Ten kila siku ya jumapili, saa 9:30 usiku, Hoyce amefanikiwa kuandaa vipindi zaidi ya 1,000 maeneo mbalimbali nchini na katika maeneo yote ambayo ametembelea amefanikiwa kutoa msaada kulingana na mahitaji yanayohitajika.

Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akisalimiana na mmoja wa wazee wenye ulemavu uliotokana na ugonjwa wa ukoma, Mganga Shija (66), wakati alipotembelea makazi ya wazee na watu wenye ulemavu wasiojiweza yaliyopo Nunge, Kigamboni, jijini Dar es Salaam ikiwa ni mojawapo ya shughuli ya kijamii kuuaga mwaka 2015 na kukaribisha mwaka mpya 2016.

Uamuzi wa Hoyce kuwa na moyo wa aina hiyo ulikuja baada ya kutambua nafasi aliyonayo kwa jamii na kuona wingi wa matatizo waliyonayo Watanzania wenzake na hivyo kufikia uamuzi wa kuanzisha kipindi ambacho kwa sasa kina zaidi ya miaka 5 na bado ameonyesha nia ya dhati kuendeleza kipindi hicho.

Kwa kutambua huduma yake kwa jamii, Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga aliwahi kunukuliwa akimtaja Hoyce Temu kama mlimbwende bora kuliko wote wakati alipotembelea kituo cha Nunge kilichopo Kigamboni, Dar Es Salaam kinachotumika kutunza wazee wasiojiweza na walemavu wasiokuwa na uwezo.

Pamoja ya kujitoa kusaidia Watanzania wenzake walio na uhitaji na kutumia muda wake mwingi katika huduma za kijamii, baadhi ya watu wasio na nia njema na Hoyce wamekuwa wakimwandika vibaya ilimradi tu kumchafulia jina katika jamii inayomzunguka.

Mtangazaji wa kipindi cha Mimi na Tanzania, Hoyce Temu akirekodi moja ya kipindi chake cha Mimi na Tanzania na mtoto ambaye aliaga dunia kabla ya matibabu.

Kama Watanzania ambao tunapenda kuona huduma za kijamii zinaboreshwa kupitia kwa Hoyce Temu na kipindi chake cha Mimi na Tanzania tuna wajibu wa kuhakikisha tunaungana kwa pamoja kumsaidia Hoyce kama mwanamke shujaa na mwenye moyo wa huruma kuwasaidia Watanzania ili kufikia malengo ambayo ameweka kuisaidia jamii..

Muungano wa Watanzania ndiyo pekee utakaozidi kumfanya Hoyce kuwa na moyo zaidi wa kusaidia Watanzania wenzake wenye uhitaji na amekuwa mtu ambaye anaonekana kuzingatia maoni ambayo anapewa na Watanzania wenye nia njema na yeye ili kuzidi kuwa mtu mwema katika jamii ya Tanzania na dunia kwa ujumla.

Hata hivyo licha ya watu wachache kumchafua amekuwa mtu ambaye hajishughulishi kuwajibu wenye nia mbaya na mipango yake kuwasaidia Watanzania na muda mwingi kuendelea kuitumia jamii na kufanya kazi kwenye kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano katika ofisi za Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini.

Pia licha ya kazi anazofanya Hoyce kwa sasa anatumia muda wake mwingine kuongeza elimu yake kwa kuchukua PHD ya mambo ya Mawasiliano.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...