Skip to main content

KAMPUNI YA MAWASILIANO YA TIGO YAHAMASISHA WATANZANIA KUJALI AFYA ZAO



Katika ni Robert Paul ambae ni Meneja Masoko ya Kampuni ya Mawasiliano ya TIGO Kanda ya Ziwa, akizungumza katika zoezi la Utoaji bure wa huduma mbalimbali za Afya ikiwemo upimaji wa Magonjwa ya Moyo, Utoaji wa Matibabu kwenye majeraha(Vidonda) pamoja na Uchangiaji damu lililofanyika juzi jumamosi katika Uwanja wa Furahisha Jijini Mwanza.




"Tigo tumeamua kushiriki zoezi hili ili kuonyesha mfano katika jamii namna tunavyojumuika na Watanzania katika shughuli za Kijamii, hivyo kupitia fursa hii ningependa kuwaasa Watanzania kuwa na desturi ya kupima afya zao mara kwa mara ikiwemo kupima shinikizo la damu, saratani lakini kubwa zaidi kuwa na moyo wa kujitolea kuchangia damu ili kuwasaidia wenye uhitaji wa damu. Alisema Paul.

Nae Cassim Aziz (Kushoto) ambae ni Meneja Masoko wa Tigo Mkoani Mwanza, alizishauri taasisi pamoja na makampuni mbalimbali nchini kuwa na desturi ya kushiriki katika shughuli za kijamii hususani kuhamasisha watanzania kupima afya zao mara kwa mara ili kuepuka athari za kiafya zinazoweza kuzuilika.

Zoezi hilo liliandaliwa na Umoja wa Wanafunzi waliosoma Chuo cha Udaktari Hubert Kairuki cha Jijini Dar es salaam wanaofanya kazi katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa ikiwa ni sehemu ya kuenzi Miaka 17 tangu mwasisi wa chuo hicho afariki dunia (Februa 06,1999) ikiwa ni miaka miwili baada ya kuanzisha chuo hicho.


Dkt.Emmanuel Chacha ambae ni Mkurugenzi wa Hospital ya CJ Jijini Mwanza akizungumza katika shughuli hiyo ya upimaji wa afya bure ambapo Hospital ya CF ilikuwa miongoni mwa wadau waliofanikisha shughulio hiyo.


Mwenye Kinasa Sauti ni Dkt.Francis Tegete ambae ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanafunzi waliosoma Chuo cha Hubert Kariuki wanaofanya kazi katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, akizungumza katika shughuli hiyo.


Profesa Paschalis Rugarabamu ambae ni Mlezi wa Umoja wa Wanafunzi waliosoma Chuo cha Hubert Kariuki wanaofanya kazi katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, akizungumza katika shughuli hiyo.


Picha ya Pamoja ya wa Umoja wa Wanafunzi waliosoma Chuo cha Hubert Kariuki wanaofanya kazi katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, akizungumza katika shughuli hiyo.


Wadau waliofanikisha zoezi la Upimaji afya bure wakiwa katika Picha ya Pamoja ya wa Umoja wa Wanafunzi waliosoma Chuo cha Hubert Kariuki wanaofanya kazi katika Mikoa ya Kanda ya Ziwa, akizungumza katika shughuli hiyo.


Kampuni ya Mawasiliano Tigo ikiendelea na Utoaji wa Huduma zake za Simu kwa wateja


Mmoja wa Wateja wa Kampuni ya Mawasiliano Tigo akipatiwa huduma na wahudumu wa Kampuni hiyo.


Wanafunzi na Wananchi mbalimbali walijitokeza kupima bure afya zao


Zoezi la Upimaji na utoaji huduma za afya bure likiwa linaendelea


Bank ya Damu salama Kanda ya Ziwa ikiendelea na zoezi la ukusanyaji damu kutoka kwa wananchi waliokuwa wanajitolea damu.


Katikati ni Alfredy Chibuae ambae ni Kaimu Mkurugenzi wa Taaisi ya Tanzania Rural Health Movement akifuatilia utoaji wa huduma unavyoendelea. Taasisi hiyo inashughulika na utoaji wa huduma za afya bure kwa watu wasiojiweza hususani watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi (mitaani) pamoja na utoaji wa huduma za dharura ikiwemo wale wanaopata ajali. Taasisi hiyo inapatikana Bugando Jijini Mwanza.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...