Skip to main content

MBEYA CITY FC WAAGA MICHUANO YA KOMBE LA SHIRIKISHO




TIMU ya Mbeya City FC Jumamosi hii imeaga michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup 2015/16) inaendelea katika mzunguko wa nne katika hatua ya 16 bora.

Jumamosi Februari 27, kulikwa na michezo nane iliyochezwa katika viwanja mbalimbali nchini, ambapo, Mwadui FC ilicheza na maafande wa Rhino Rangers katika uwanja wa Mwadui Complex mjini Shinyanga, wakati jijini Mbeya Tanzania Prisons ilicheza na Mbeya City na kubamizwa bao 2-1 katika uwanja wa kumbukumbu wa Sokoine jijini hapa. 

Kwa mantiki hiyo Mbeya City FC imetolewa katika michuano hiyo baada ya kufungwa an Tanzania Prisons bao 2-1, na kufanya Tanzania Prison kusonga mbele katika hatua nyingi ya michuano hiyo katika uwanja sokoine uliyojaa maji baada ya mvua kubwa kunyesha.

Kutokana na hali hiyo wachezaji walicheza chini ya viwango kutokana na uwanja huo kuteleza na kufanya wachezaji wa timu zote mbili kushindwa kuonyesha kandanda safi.

Katika mchezo huo, Tanzania Prisons ilianza kupata goli baada ya kuchungulia katika nyavi ya Mbeya City FC kupitia kwa mshambuaji machachali Mohamed Mkopi katika kipindi cha kwanza.

Hadi mapumziko timu ya Tanzania Prisons ilikuwa inaongoza na kipindi cha pili kulipofika timu ya Mbeya City ilisawazisha kupitia winga wake wa kushoto, Joseph Mahundi baada ya kupata krosi safi kutoka kwa Haruna Moshi.

Timu zote ziliendelea kukamiana kipindi chote cha pili ndipo mshambuaji mahili Benjamin Asukile wa timu ya Tanzania Prisons alipopiga shuti kali kutoka katikati ya uwanja na kufunga goli la pili katika dakika 82.

Kosa alilofanya mlinda mlango wa Mbeya City, Beno Kakulanya ni kuacha mpira kudunda uliyomzidi urefu na kutumbukia nyavuni.

Mchezo huo ulichezeshwa na mwamuzi Selemani Kinugani toka Morogoro akisaidiana na John Kanyenye toka Mbeya na Milambo Tshikungu toka mkoani Tanga. 

Hata hivyo mzunguko huo wa nne utakamilika leo Jumapili ambapo Simba SC watakaribisha Singida United katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Panone FC dhidi ya Azam FC uwanja wa Ushirika mjini Moshi, huku Toto Africans wakicheza dhidi ya Geita Gold katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Bingwa wa michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) ataiwakilisha Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAF CC) mwaka 2017.



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...