Skip to main content

MO DEWJI FOUNDATION YAKABIDHI MILIONI 100 KWA WAFUGAJI WA KUKU, KIJIJI CHA MSOGA, CHALINZE



Afisa Mahusiano wa Mo Dewji Foundation, Zainul Mzige (wa pili kulia) akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 100 kwa Mwenyekiti wa mradi ufugaji kuku wa kienyeji katika kijiji cha Msoga, Michael Mkindo (wa tatu kushoto). Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Mh. Ridhiwani Kikwete (wa pili kushoto), Mkuu wa Wilaya ya ya Bagamoyo, Mh. Majid Mwanga (kushoto) na Diwani wa kata ya Msoga, Hassan Mwinyikondo (kulia).

Afisa Mahusiano wa MO Dewji Foundation, Zainul Mzige akisoma hotuba wakati wa makabidhiano ya mfano wa hundi kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji chotara kutoka kijiji cha Msoga, Chalince mkoa wa Pwani. Wa kwanza kushoto ni mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Chalinze, Majid Mwanga, wa kwanza kulia ni Diwani wa Kata ya Msoga, Hassan Mwinyikondo.

Mfuko wa MO Dewji umeupatia mradi wa ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara wa kijiji cha Msoga mkoani Pwani shilingi milioni 100 kufanikisha uendeshaji wa mradi huo awamu ya kwanza.

Mradi huo unaokisiwa kuwa na makisio ya uzalishaji ya sh 2,777,901,500 ulibuniwa mwaka 2013 kwa lengo la kukabiliana na umaskini kijijini hapo.

Kwa mujibu wa taarifa za mradi makisio ya mapato kutokana na mauzo ya mayai, vifaranga na kuku baada ya kukoma kutaga zinakadiriwa kuwa sh 4,913,708,000

Aidha mradi huu unasimamiwa na kufadhiliwa na rais Mstaafu Dk Jakaya Mrisho Kikwete.

Akikabidhi hundi hiyo ya sh milioni 100, Afisa Mahusiano wa Mo Dewji Foundation, Zainul Mzige alisema kwamba fedha hizo zitaumika kujenga mabanda 200, ununuzi wa vifaranga, ununuzi wa chakula cha kuku, chanjo na dawa na malipo kwa wataalamu.




Afisa Mahusiano wa MO Dewji Foundation, Zainul Mzige akisoma hotuba wakati wa makabidhiano ya mfano wa hundi kwa wafugaji wa kuku wa kienyeji chotara kutoka kijiji cha Msoga.

Mambo mengine ni utawala, mawasiliano, ununuzi wa chachu za mpunga na vifaa vya chakula na maji.

Mzige alisema pamoja na kutoa fedha hizo kuunga mkono juhudi za Msoga Poultry Farming Project (MPFP) kuendesha na kuuendeleza mradi kibiashara, aliwataka wahisaniwa kutambua kwamba maendeleo ya mradi wao yatategemea sana namna wanavyokuwa makini kutumia fursa mbalimbali kujiimarisha.

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita Mo Dewji Foundation imetumia zaidi ya dola za Marekani milioni 3 kwa ajili ya kusaidia miradi mbalimbali ya kijamii nchini.

Aidha hivi karibuni Mfuko wa MO Dewji kwa kushirikiana na kampuni ya Darecha Limited walizindua shindano la Mo Mjasiriamali lenye lengo la kusaidia kukuza ujasirimali miongoni mwa vijana.

Shindano ya Mo Mjasiriamali litatoa fursa ya ukuzaji wa mitaji, ulezi wa wajasiriamali na mitandao ya biashara kuongeza mwanga, ujasiri na kuzalisha wajasiriamali Tanzania.

Ili kufanikisha nia ya kuwa na wajasiriamali wengi, shindano hilo linatarajiwa kuwa daraja kwenda kwa Ofisa Mtendaji, Mohammed Dewji (MeTL Group na mwenyekiti wa Mo DewjiFoundation) ambapo vijana ambao wanaonekana wana kitu cha kufanya, lakini hawana msaada watashiriki kwa lengo la kupata msaada katika mfumo wa mtaji, mtandao na usimamizi wa ukuaji wa shughuli wanayofanya au kutaka kuifanya ili kuianzisha na kuikuza.

Kwa niaba ya wananchi wa Msoga, mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete alimshukuru Mwenyekiti wa Taasisi ya Mo Dewji, Mohammed Dewji kw ufadhili ambao ameufanya kwa wananchi wa kijiji cha Msogo na kumtaka kuwa na moyo wa kutoa zaidi ili azidi kusaidia wananchi walio na mahitaji.




Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete akitoa neno la shukrani kwa MO Dewji Foundation mara baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya shilingi 100 kwa ajili ya ufugaji wa kuku wa kienyeji Chotara.

Alisema kuwa kupitia mradi huo wa ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara, wananchi wa kijiji cha Msoga wataweza kujikwamua na janga la umasikini na wataendelea kuwa wakiandika maombi ya miradi mbalimbali ambayo wanataka kuifanya ili kuzidi kutengeza ajira zaidi kwa wananchi wa Mzoga.

“Tunamshukuru Mohammed Dewji kwa msaada huu tunaimani utasaidia wananchi wa Mzoga na namuomba asisite kutupokea muda mwingine tunapokuwa na miradi mingine,” alisema Kikwete.

Nae Mratibu wa Mradi wa ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara (Msoga Poultry Farming Project), Novatus Kailembo alisema wazo la kuanzisha mradi huo lilitolewa na Rais wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete mwaka 2013 ili kusaidia kuboresha maisha ya wananchi wa Msoga kama kiuchumi, kielimu na kiafya.

Alisema wanataraji kuanza na wanakijiji 300 ukiwa ni mradi wa mfano, awamu ya kwanza ambao wanataraji kuanza kufanyika katika vitongoji tisa ambavyo ni Hospital, Takalagame, Kota, Mnazi Mmoja, Tumbi Juu, Tumbi Chini, Kingugi, Mkundi na Mokela.


Mkuu wa Wilaya ya Chalinze, Majid Mwanga akimshukuru Mwenyekiti wa MO Dewji Foundation, Mohammed Dewji kwa ufadhili ambao ameutoa kwa wilaya yake kwa ajili ya ufugaji wa kuku wa kienyeji chotara ambapo ufugaji huo unataraji kufanyika katika kijiji cha Msoga.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...