Skip to main content

MUNGY AWATAKA WATANZANIA KUZINGATIA MASHARTI NA KANUNI ZA MITANDAO (AUDIO + VIDEO)




Mungy


Mkuu wa Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy.

Ili kuhakikisha kunapungua kwa makosa ya uvunjifu wa sheria ya mtandao, Mkuu wa Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA), Innocent Mungy amewataka watumiaji wa mitandao kuzingatia kanuni na masharti ya mitandao.

Mungy aliyasema hayo katika mahojiano maalumu na Mo Blog na kueleza kuwa moja ya sababu zinazopelekea watumiaji wa mitandao kufanya makosa ni kutokusoma masharti na kanuni za mitandao wanaoingia wakati wanapojisajili.

“Wengine hawaelewi maana ya mitandao ya kijamii lakini kabla ya kuingia wanatakiwa kusoma masharti na vigezo wakati wanajisajili kuingiza kwenye mitandao hiyo,” alisema Mungy.

Alisema makosa ya mitandao yalianza kujitokeza zaidi mwaka 2012 katika mitandao ya Facebook na Instagram na yaliongezeka zaidi baada ya kukua kwa mtandao wa Whatsapp na kuwataja waathirika wakubwa kuwa vijana na zaidi wa kike kati ya miaka 18 hadi 24.

Mungy alieleza kuwa ili kupambana na makosa ya mtandao Watanzania wanatakiwa kubadilika na kutumia mitandao vizuri na kabla hawajaweka picha au kuandika maneno wahakikishe wanachokiweka mtandaoni hakina makosa.

Aliongeza kuwa sheria zipo na watumiaji ambao wamekuwa wakivunja sheria wamekuwa wakifungwa, wengine wakitozwa faini na wengine bado wanafatiliwa na Jeshi la Polisi ili kuwatia hatiani kwa makosa ya kuvunja sheria ya makosa ya mtandaoni.

“Watanzania wanatakiwa kufuata sheria kabla ya kuweka picha mtandaoni wanatakiwa kufikiria kwanza je kama nikiweka itakuwaje maana mtandaoni kila mtu anaona na hiyo taarifa itadumu milele,” alisema Mungy.

Pia alizungumzia tukio lililotokea mtandaoni linalomhusu Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu la kuandikwa vibaya na Mungy kueleza kuwa walipokea taarifa za Hoyce na tayari wameshalikabidhi kwa Jeshi la Polisi na hatua zaidi zinaendelea kuchukuliwa na Polisi ili kuishughulikia kesi hiyo.

Mungy alimaliza kwa kuwataka Watanzania kutumia mawasiliano kama njia ya kuleta maendeleo na sio kuvunja sheria ambayo serikali imeitunga kwa ajili ya kudhibiti makosa ya mtandaoni lakini pia kuutaja mtandao wa Mo Blog kama moja ya mtandao ambao umekuwa mstari wa mbele kukemea matumizi mabaya ya mtandao.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...