Skip to main content

Mwenyekiti Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa Mhekwa Azindua Maadhimisho ya Miaka 39 ya CCM

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa, Ephram Mhekwa akihutubia wananchi wa Kijiji cha Lulanzi wilayani Kilolo, mkoani Iringa wakati sherehe za uzinduzi wa maadhimisho  kimkoa ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM. (Picha zote na Friday Simbaya)











MAADHIMISHO ya kumbukumbu ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimkoa yamezinduliwa Januari 31, mwaka huu, na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa, Ephraam Mhekwa katika Kijiji cha Lulanza wilayani Kilolo, Mkoa wa Iringa.

Aidha, kilele cha maadhimisho hayo kinatarajiwa kufanyika mkoani Singida, Februari 6, mwaka huu, na mgeni rasmi atakuwa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais mstaafu Jakaya Kikwete.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa, Ephraam Mhekwa alisema mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho kimkoa mgeni rasmi atakuwa mlezi wa mkoa ambaye ni waziri mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Tanzania Mzengo Pinda.

Alisema pia kuwa kilele cha maadhimisho hayo kimkoa yatafanyika katika Jimbo la Isimani wakati mwaka jana yalifanyika katika Jimbo la kalenga wilayani Iringa.

Alisema kuwa mambo yanayotakiwa kuzingatiwa katika wiki hiyo ni pamoja na kuingiza wanachama wapya wa CCM na jumuia zake na kufanya shughuli zingine za kuimarisha Chama. 

“Shughuli nyingine inayotakiwa katika wiki ya maadhimisho ni kufanya mikutano ya kuwashukuru wana-CCM na wananchi kwa kuiamini CCM na kuhamasisha wananchi kufanya kazi za maendeleo,” alisema Mhekwa.

Aliongeza kuwa katika maadhimisho hayo yaliyobeba kaulimbiu ya ‘sasa kazi, kujenga nchi na kukijenga Chama’ ni pamoja na kushiriki katika ujenzi wa madarasa, vituo vya afya, zahanati, upandaji miti, uchimbaji wa mitaro ya maji na kufanya usafi wa mazingira.

Alisema kilele cha sherehe hizo zitafanyika Februari 6, mwaka huu, kwa kuwa Februari 5, ambayo ndiyo siku CCM ilianzishwa, itakuwa ni siku ya kazi. 

Pia, alitumia fursa hiyo kuwaomba wana-CCM, wadau na wananchi wengine kwa ujumla, kushiriki kikamilifu maandalizi na wahudhurie kwa wingi sherehe hizo.

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Iringa, Ephraam Mhekwa amekabidhi jumla ya kadi 287 kwa wana chama wapya  wakiwemo UVCCM (60), kadi za wanachama (50), UWT (77) na wazazi (100).


Baadhi ya viongozi waliohudhuria maadhimisho ni pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jowike Kasunga, Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Selemani Mzee, Katibu wa CCM wilaya ya Mufindi Jimson Mhagama, Katibu wa CCM Wilaya ya Kilolo Clemence Mponzi, Katibu wa wazazi mkoa Geofrey Kavinga, Katibu Msaidizi Mkuu  CCM  Mkoa Agnes Kasela, Mchumi wa CCM Mkoa Lazaro Manila na wengine wengi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...