Skip to main content

SERIKALI YA KIJIJI YAKAMATA MBAO ZILIKATWA KATIKA MSITU WA GANGALAMTUMBA

NA DENIS MLOWE, IRINGA VIJIJINI

SERIKALI ya kijiji cha Mfyome, kata ya Kiwele katika Halmashauri ya wilaya ya Iringa vijijini mkoani Iringa imefanikiwa kukamata shehena ya mbao 298 zinazosadikiwa kukatwa kutoka kwenye msitu wa Gangalamtumba uliopo kijijini hapo na kusababisha uharibifu mkubwa wa kimazingira.

Wananchi hao kwa kwa kushirikiana na Chama Cha Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) kupitia mradi wake wa ushiriki wa wananchi katika kusimamia maliasili unaofadhiliwa na Watu wa Marekani (USAID)imefanikiwa kukamata shehena ya hizo zenye thamani ya shilingi miloni 8 baada ya kupatiwa mafunzo ya ufuatiliaji uwajibikaji katika jamii kwa wananchi.

Akizungumza mara baada ya kukamatwa kwa mbao hizo katika kijiji cha Mfyome, Afisa Mawasiliano wa LEAT, Miriam Mshana alisema elimu ya uwajibikaji katika jamii ni muhimu kwa vile inasaidia kuongeza hamasa miongoni mwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayozungukwa na rasilimali kuweza kuzilinda.

Alisema kuwa Leat kwa kushirikiana na USAID waliwapatiwa mafunzo wanakijiji ambapo mradi huo unawafikia katika kuwawezesha kutambua uwajibikaji katika jamii kwa wananchi katika uhifadhi wa mazingira ambapo juhudi kubwa inafanyika katika kuwadhibiti watu ambao wanaharibu mazingira na kuwachukulia hatua kali.

Mshana alisema kuwa katika miaka ya nyuma jukumu la kutunza misitu, wanyamapori na uvuvi lilikuwa linafanywa na Serikali lakini hivi sasa jukumu hilo limepelekwa katika ngazi ya vijiji na wilaya ambapo wananchi wanashiriki moja kwa moja katika utunzaji wa rasilimali husika na kupatiwa mafunzo sahihi ya utunzaji wa mazingira.

Kwa upande Chuki Mduda ambaye ni mjumbe wa kamati ufuatiliaji uwajibikaji katika jamii katika ngazi ya wilaya amesema baada ya kukamatwa kwa mbao hizo uongozi wa kijiji umeamua mbao hizo zitumike kutengenezea madawati ili kumaliza tatizo la uhaba wa madawati kijijini hapo.

Alisema mbao hizo zimetokana na miti ya asili iliyoko katika msitu wa msitu wa Gangalamtumba ulioko katika kijiji cha Mfyome walikutwa nazo waaribifu wa mazingira baada ya wananchi wengi kupatiwa elimu ya mazingira na kuanza kulinda msitu huo.
Alisema kuwa kwa sasa wananachi baada ya kupatiwa elimu wamekuwa wakiwakamata watu wanaoharibu mazingira na kuwapeleka katika uongozi wa Serikali ya mtaa ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi.

Mradi wa ushiriki wa wananchi katika kusimamia maliasili unaosimamiwa na LEAT kwa uadhili wa shirika la maendeleo la kimataifa la Marekeni (USAID) unatekelezwa katika vijiji 32 kutoka halmashauri mbili za Iringa vijijini na Mufindi mkoani Iringa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...