Skip to main content

WAHAMIAJI HARAMU 83 WA KIETHIOPIA , DEREVA NA TINGO KUTUPWA JELA MIAKA 3 !

 


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Iringa imewahukumu kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya Sh Milioni 1.5 kila mmoja, dereva Hansi Mwakyoma (28) na tingo wake wake Alex Adam (32) baada ya kukamatwa na kukiri kusafirisha wahamiaji wasio na vibali 83 kutoka nchini Ethiopia ambao pia wamehukumiwa kwenda jela miaka 3 au kulipa faini ya Sh Milioni 1.

Kwa kutumia gari aina ya Scania lenye namba T478 DFE mali ya Frola Mwambenja wa Mbeya, Januari 16, mwaka huu; dereva huyo na tingo wake walikamatwa katika kijiji cha Ruaha Mbuyuni wilayani Kilolo mkoani Iringa, barabara kuu ya Iringa Mbeya wakiwasafirisha watu hao kuelekea Kyela ambako ni mpakani mwa Tanzania na Malawi.

Akitoa hukumu hiyo leo Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mkoa wa Iringa Endrew Scout alisema ameridhika na maelezo yaliyotolea na wakili wa serikali pamoja na vielelezo likiwamo gari lililotumiwa na watuhumiwa hao kusafirisha watu hao kutoka Kongowe Dar es Salaam kuelekea Kyela Mbeya.

Baada ya kusoma hukumu hiyo, baadhi ya raia hao wa Ethiopia waliangua kilio mahakamani hapo na kusababisha watu waliokuwa karibu na jengo hilo kusogea ili kujionea kulikoni.

Mkalimani wa wahamiaji hao ambao hawazungumzi Kingereza wala Kiswahili zaidi ya lugha ya kwao, Emanuel Yeb Mtaltisili ambaye ni mtangazaji wa kituo cha redio ya Ebony FM cha mjini Iringa alisema; “walichokitarajia wahamiaji hao ni kupewa hukumu ya kurudishwa kwao baada ya kukiri kosa hilo.”

Awali akisoma maelezo ya kosa la watuhumiwa hao baada ya watuhumiw a wote kukiri kosa mbele ya mahakama hiyo, Wakili wa Serikali kutoka Idara ya Uhamiaji Godfrey Ngwijo alisema ilikuwa Januri 16 mwaka huu katika eneo la Ruaha Mbuyuni watuhumiwa hao walipokamatwa wakiwa ndani ya gari hilo lenye bodi lililofunikwa wakisafiri kutoka Kongowe Jijini Dar es Salam kwenda Malawi kinyume na sheria ya uhamiaji ya mwaka 2002 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2015.

Alisema katika tarehe isiyojulikana, watuhumiwa 83 raia wa Ephiopia waliingia nchini kwa kutumia kwa njia zisizo halali na kuelekea jijini Dar es Salaam walikoanzia safari yao ya kuelekea Kyela mkoani Mbeya ili waingie nchini Malawi.

Alisema walipofika eneo la Ruaha Mbuyuni walikamatwa na Askari wa kikosi cha Usalama barabarani ambaye aliwataka wafungue mlango wa nyuma ya gari na kukuta kuna watu hao huku baadhi yao wakiwa hoi.

Alidai mara baadaya kukuta watu aliwaamuru kwenda kituo cha Polisi cha Ruaha Mbuyuni ambako dereva na msaidizi wake walikiri kosa wakidai walikubali kuwasafirisha kwa makubaliano ya kupata kiasi fulani cha fedha na kwamba walipoona mzigo mkubwa waliomba waongezwe na kukubaliana na mwenye mzigo kuwa wangeongezewa mara baada ya kufika walikokuwa wanakwenda.

Mara baada ya maelezo hayo ya wakili hakimu aliwataka watuhumiwa wote pamoja na kukiri kosa kuhojiwa kama wanayakubali maelezo hayo ili haki iweze kutendeka na walipoulizwa wakikiri kuwa maelezo yote yaliyotolewa na wakili wa serikali ni ya kweli

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...