Skip to main content

WAKULIMA MBOZI WALIA NA MBEGU FEKI

Na Esther Macha,Tunduma

MAWAKALA wa forodha wanaotoa huduma kwa wateja katika mji wa Tunduma Mkoani Mbeya wameonywa kuacha lugha chafu mbazo zinaweza kukimbiza wageni toka nje ya nchi wanaofika katika mpaka huo kupata huduma .

Hayo yamesemwa jana na ofisa elimu kwa mlipa kodi wa mamlaka ya mapato (TRA)Mkoa wa Mbeya , Kissa Kyejo wakati wa semina ya uhamasishaji na sheria na taratibu katika shughuli za mawakala wa forodha na viongozi wa TRA.

Alisema kuwa mawakala wote wa forodha ni muhimu kuwa na lugha nzuri kwa wateja kwani mpaka huo umekuwa ukitoa huduma kwa wageni mbali mbali .

“Sehemu kama hii ambayo ina mchanganyiko wa watu na wanaotoka maeneo mbali mbali hapa nchini muhimu samba lugha nzuri ikatumika kwa wateja kwani vinginevyio tutapoteza wageni wengi wanaotoka nchi za jirani”alisema Ofisa huyo

Kwa upande wake Ofisa Mfawidhi wa forodha wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA)Mkoa wa Mbeya ,Cosmas Magori alisema katika utendaji ni vema kila wakala wa forodha kufuata misingi na taratibu za kazi ili kuweza kujiletea nidhamu ya kazi.

Alisema kuwa mambo muhimu yaliyokuwepo katika semina hiyo ni pamoja na huduma bora kwa wateja,uvaaji wa sare na vitambulisho lengo likiwa ni kuboresha huduma hasa wageni wa nje na ndani ya nchi .

Akizungumzia kuhusu rushwa ,Magori alisema hatapenda kuona kitengo cha forodha wanakuwa vinara wa kuombna rushwa kwa wageni na madereva wanaofika kwao kuomba huduma.

“Naombeni mbadilike katika hili sitapenda kusikia wageni wakilalamikia suala la rushwa kuanzia leo hili lianze utekelezaji mapema ,tufuate maadili ya kazi ili kulinda heshima “alisema Meneja Magori.


Na Esther Macha, Mbeya

SHIRIKA la Ugavi wa umeme Tanzania (Tanesco) mkoa wa Mbeya limesema kuwa katika mwaka ujao wa fedha litaanza mchakato wa kubadilisha na kuifanyia marekebisho miundombinu ya umeme ya zamani ili kuendana na mahitaji ya sasa.

Akizungumza juzi kwenye mkutano wa Tanesco na wateja wakubwa wa huduma ya umeme jijini hapa Meneja wa Tanesco mkoani Mbeya Mhandisi, Francis Maze alisema kuwa shirika hilo limedhamiria kutoa umeme wa uhakika katika kipindi kisichozidi miaka miwili kuanzia mwezi julai mwaka huu.

Alisema katika mwaka wa fedha 2016/2017 shirika hilo limetoa kipaumbele kubadilisha mifumo ya miundombinu ya zamani kwa sababu ina inashindwa kuhimili kiwango cha umeme kinachotumika sasa kutokana na kuongezeka kwa watumiaji wa huduma hiyo mkoani Mbeya.

“Mkoa wa Mbeya una mfumo wa zamani wa kusambaza umeme tunatakiwa kufanya marekebisho makubwa, nyaya zilizizopo ni ndogo haziendani na mahitaji ya umeme yanayohitajika kwa sasa, hivyo kuanzia julai baada ya kuanza mwaka wa fedha tutaanza zoezi hilo na inaweza kutuchukua miezi 24 kumaliza lakini tumeandaa mkakati angalau tutumie miezi 12 kumaliza” alisema.

Maze alisema Tanesco itatoa tenda kwa wakandarasi Binafsi kufanya kazi hiyo ili kuweza kumaliza kwa muda uliopangwa na kwamba watangaza tenda kubla ya mwezi Mei mwaka huu.

Akizungumzia hali ya umeme mkoani hapa alisema kuwa upo wa uhakika kwa sasa baada ya kufunga Transifoma mpya ya megawati 60 kwenye kituo kikubwa cha Mwakibete kilichopo Sae jijini Mbeya.

Alisema kabla ya mwezi Augusti mwaka huu wataboresha miundombinu inayopeleka umeme viwandani, ikiwa ni pamoja na kubadilisha nguzo ili wawe na hali bora ya umeme kwa kuwa wao ndio wateja wakubwa wa Tanesco.

Kwa upande wake Meneja wa umeme wa kiwanda cha Sementi cha Mbeya ambao kwa mujibu wa Tanesco ni walipaji wakubwa wa umeme mkoani Mbeya Daud Rwebangila alisema kuwa changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni kupata umeme ambao haujatulia hali inayowawia vigumu kwenye shughuli za uzalishaji kiwandani hapo.

Alisema kuwa changamoto hiyo imekuwa iksababisha kusimamisha kazi kwa muda wa masaa kadhaa na wakati mwingine baadjhi ya vifaa kuungua.

“Sisi kama wateja wakubwa chanagomoto kubwa tunayoipata ni umeme unaochreza wakati shuguli za kiwanda ikiendelea hali hii inasababisha vifaa vyetu kuungua na wakati mwingine tunalazimika kusitisha shuguli za uzalishaji kwa muda, tunaomba hili lirekebishwe” alisema.

MWISHO 

Na Esther Macha,Mbozi

WAKULIMA wa vijiji vya kata ya Isansa na Magamba Wilaya ya Mbozi Mkoani Mbeya, wamelalamikia wakala wa mbegu ya Kibo Seeds kuwauzia mbegu feki ambazo hazikuota, ambapo wamelazimika kuingia gharama ya kununua mbegu nyingine na hivyo kuwasababishia hasara ya mamilioni ya shilingi.

Wakizungumza na waandishi wa habari jana wakulima hao ,walisema kuwa waliuziwa mbegu aina ya Kitale Haibrid 614 ambayo inazalishwa na kampuni ya mbegu ya Kibo Seeds ya nchini Kenya.

Mmoja wa wakulima hao, Elia Shipelele alisema kuwa baada ya kugundua kuwa mbegu hizo ni feki walilaziika kutafuta begu zingine na mbolea ili kuendana na msimu wa kilimo.

Hata hivyo mkulima huyo aliiomba serikali kuangalia uwezekano wa kufanya ukaguzi wa mbegu kabla kupeleka kwa wakulima ili kuweza kuepuka hasara.

Kwa upande wake Ofisa kilimo na mifugo wa kata ya magamba ,clemence Mamuya alikiri kuwepo kwa tatizo hilo akidai kuwa na yeye ni miongoni kwa wakulima ambao wamepata hasara hiyo.

Alisema kuwa kutokana na tatizo hili ni vema serikali ikawa na mkakati wa kuyafuatilia makapuni na mawakala wanaosambaza mbegu kwa wakulima ili kuondoa sintofahamu kwa wakulima.

Akizungumzia malalamiko hayo Mkurugenzi wa Kampuni ya Meru green Care Victor Lema Kampuni ya Meru Green Care alisema suala hilo wamelisikia kutoka kwa wakulima .

Aidha Lema alisema kuwa baada ya kupata malalamiko hayo alichukua hatua kwa kwenda ofisi ya kilimo wilaya na kuamuliwa kuwasiliana na kampuni ya mbegu ya Kibo seeds ambao walitaka idadi ya majina ya wakulima waliopatwa na tatizo hilo.

Hata hivyo Lema alisema jumla ya wakulima 80 wameathirika na tatizo hilo la mbegu feki katika wilaya ya Mbozi.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...