Skip to main content

“WATANZANIA WAZINGATIE SHERIA ZA MTANDAO, KIFUNGO NI MIAKA 30 AU ZAIDI” – KITWANGA


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Charles Kitwanga (pichani) amewataka Watanzania kuzingatia sheria za mtandao ambazo zilitungwa mwaka jana kufuatia kuonekana kuwepo kwa baadhi ya watumiaji ambao wamekuwa hawafati sheria.

Mhe. Kitwanga alisema wanaotumia mtandao wanawajibu wa kutumia mtandao kwa matumizi ambayo hayatavunja sheria na ambao watakuwa wakikiuka sheria hiyo serikali haitawavumilia na watawachukulia hatua za kisheria.


Msemaji wa Jeshi la Polisi Advera John Bulimba.




“Adhabu ya kuvunja sheria hii ya makosa ya mtandao ni mbaya sana na ninataka kuwambia Watanzania wazingatie sheria za mtandao … kifungo ni miaka 30 au hata zaidi,” alisema Kitwanga.

Aidha aliwataka ambao wamekuwa wakitukanwa katika mitandao ya kijamii wapeleke malalamiko Polisi na serikali imejipanga kuwachukulia hatua watumiaji ambao wamekuwa hawafati sheria za mtandao.

Kwa upande wa Jeshi la Polisi kupitia kwa msemaji wa jeshi hilo, Advera Bulimba alisema kuwa jeshi hilo limekuwa likiwachukulia hatua watumiaji wote wa mitandao ambao wamekuwa wakikutwa na hatia ya kufanya matumizi mabaya.

Alisema tangu imetungwa sheria hiyo wameshafungwa baadhi ya watumiaji na kesi saba zikiwa mahakamani na bado wanaendelea kufatilia watumiaji wengine ili wawachukulie hatua.

“Polisi tunaendelea kuwachukulia hatua watumiaji ambao wanakuwa na makosa na kwasasa kuna kesi saba zipo mahakamani … tangu sheria imetungwa kesi tunazopokea zinazohusu mitandao zimepungua kutoka 25 hadi 30 kwa siku ila siku hizi zinakuwa 10 au chini ya hapo,” alisema Bulinda.

Nae mmoja wa watumiaji wa mtandao, Grace Mwanga aliwashauri Watanzania wenzake kudumisha maadili ya kitanzania na kuifanya mitandao kama njia ya mawasiliano kama jinsi lilivyo kusudiwa na waanzilishi wa mitandao hiyo.

“Watanzania tudumishe maadili yetu ya zamani, mitandao isitufanye tusahau asili yetu … tutumie mitandao kuwasiliana na hata kufanya matangazo ya biashara zetu,” alisema Grace.




Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...