Skip to main content

JAMII IWE MAKINI NA MATANGAZO YA NAMNA HII

Na:George Binagi @BMG
Hili ni miongoni mwa Matangazo yanayosambaa kwa kasi katika mitandao ya kijamii. Awali matangazo kama haya ikiwemo lile la Kujiunga na Freemason pamoja na watalaamu wa tiba asili yalizagaa pia mitaani na hata katika mitandao ya kijamii.

Asilimia kubwa ya matangazo haya yanaonekana kuwa ya kuwalaghai wananchi kupitia shida na matatizo yao hususani katika magonjwa.

Nakumbuka mwaka jana Serikali ilipiga marufuku matangazo yote ya waganga wa kienyeji katika mabango ya mitaani, mitandao ya kijamii na hata katika vyombo muhimu vya habari kama vile redio, runinga na magazeti, kutokana na matangazo hayo kujaa upotoshaji kwa baadhi ya maeneo ikiwemo kutibu magonjwa sugu ikiwemo Ukimwi nk.

Hata hivyo katazo hilo halikuzaa matunda kama ilivyotarajiwa, kwani lilizua mvutano mkali baina ya serikali na waganga wa jadi (hupenda kuitwa watalaamu wa tiba asili), na sasa kasi ya matangazo hayo imeongezeka maradufu zaidi.

Ni kutokana na upotoshaji wa baadhi ya matangazo hayo, Binagi Blog inahoji; Ni nani mwenye jukumu la kufuatilia matangazo yanayobandikwa katika mitaa, kwenye runinga, magazeti pamoja na kwenye mitandao ya kijamii ili kuondoa athari za matangazo hayo katika jamii?.

Mfano mzuri ni tangazo hapo juu ambalo limeonekana kubandikwa katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Jijini Mwanza, na sasa linasambaa kwa kasi katika mitandao ya Kijamii, kwamba kuna biashara mpya ya ununuzi wa mkojo wa binadamu.

Kwa tangazo kama hili pamoja na mengineyo mengi, ni vyema viongozi wa serikali katika janja zote ikiwemo Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoo wakachukua hatua dhidi ya wahusika ili kuondoa upotoshaji unaojitokeza ama unaoweza kujitokeza kutokana na matangazo yenye upotoshaji katika jamii. Pia wanajamii wawe makini na matangazo ya aina hiyo.
Bonyeza HAPA Kusoma Tangazo Jingine la Upotoshaji.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...