Skip to main content

MADAM SOPHY CHARITY EVENTS YAZINDULIWA RASMI, JAMII YATAKIWA KUSAIDIA WENYE UHITAJI MAALUM



Baadhi ya wadau wakitoa zawadi na vitu mbalimbali kwa Madam Sophy ambavyo vitagawiwa kwa wanafunzi wa shule hiyo ya Jeshi la Wokovu na wale wa Makumbusho Sekondari.

Taasisi mpya ya Kijamii ijulikanayo Madam Sophy Charity Events yenye malengo ya kusaidia jamii hasa ile yenye uhitaji maalum ikiwemo watu wasiojiweza imezinduliwa rasmi mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam sambamba na kutoa misaada mbalimbali kwa watu na watoto wenye uhitaji huo maalum.

Tukio hilo la kipekee lililoandaliwa na kuratibiwa na Mwanadada, Sophia Mbeyela pia lilijumuisha wadau na marafiki mbalimbali walioungana na Madam Sophy katika kufanikisha tukio hilo lililofanyika katika ukumbi wa shule ya Msingi ya Jeshi la Wokovu ambayo ilishirikisha watoto wanafunzi wa kituo cha Matumaini wenye Ulemavu wa viungo na ngozi.

Madam Sophy na marafiki zake kwa pamoja waliweza kutoa misaada ya vitu mbalimbali kwa watoto hao ambapo pia walipata wasaha wa kuzindua taasisi hiyo huku mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni ambaye aliwakilishwa na Mbunge Kibaha Vijijini, Mh. Amoud Abduul Jumaa ambaye aliahidi kufikisha kilio cha walemavu na watu wenye mahitaji maalum Serikalini paamoja na kwenda kuwasilisha Bungeni ilikuona utekelezaji wake kwa ukaribu.

“Madam Sophy Charity. ni taasisi ambayo zaidi ni kuona wenzetu wenye uhitaji maalum hasa walemavu wanapata nafuu katika kuendana na majukumu ya nchi hii kwani sote tuna haki sawa kama wengine na ulemavu wetu usitutenganishe. Tunahitaji Serikali kuhakikisha inashusha bei vifaa vyote vya walemavu ikwemo viungo vya bandia ikiwemo mikono na miguu ambayo kwa kiungo mimoja pekee yake kinakaribia hadi milioni moja” alieleza Madam Sophy.

Madam Sophy aliongeza kuwa, Serikali inayo wajibu wa kujenga shule nyingi zaidi za watu wenye ulemavu kwani zilizopo sasa bado ni chache na watu wenye ulemavu wamehamasika kujitokeza kusoma hivyo jukumu lililopo ni kuhakikisha wanaongeza shule za watu hao pamoja na kutengeneza miundombinu ambayo inakuwa rafiki kwa walemavu kuanzia mashuleni na hata maeneo muhimu.

Aidha, Kwa upande wake, mgeni rasmi huyo aliweza kuchangia kiasi cha Sh Laki tano kwa ajili ya kuunga mkono juhudi na harakati za Madam Sophy ambapo alieleza kuwa, licha ya ulemvu wake ameweza kuonesha njia ya kujikwamua pamoja na kuwasaidia wenzake.

Madam Sophy ambaye kitaaluma ni Mwalimu, ni miongoni mwa wanafunzi waliopata kusoma katika shule hiyo na kumaliza hapo darasa la saba mwaka 2002 ambapo pia aliendelea na shule mbalimbali ikiwemo Sekondari ya Jangwani na baadae chuo, ameomba wadau kujitokeza kuungana naye katika kuhakikisha wanasaidia watu na jamii yenye uhitaji maalum kwani kutoa ni moyo.

Tazama MO tv, kuona tukio hilo hapa:




Mgeni rasmi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni ambaye aliwakilishwa na Mbunge Kibaha Vijijini, Mh. Amoud Abduul Jumaa akitoa nasaha zake kwa niaba ya Mh. Masauni. wakati wa uzinduzi rasmi wa taasisi hiyo ya Madam Sophy Charity Events. Upande wa kulia ni Madam Sophy. (Imeandaliwa na Andrew Chale, Modewjiblog)


Baadhi ya viongozi wa Jeshi la Wakovu wanaosimamia shule hiyo ya Msingi wakifuatilia tukio hilo..


Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika mkutano huo.


Wageni waalikwa.


Wanafunzi wenye ulemavu wa viungo na ngozi wakiwa katika tukio hilo.


Wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi wakitoa burudani kwa mgeni rasmi (hayupo pichani)


Mtoto Emmanuel Anthony 'Rais' akifurahia jambo katika tukio hilo. Emmanuel ameeleza kuwa, licha ya kuwa mlemavu, ndoto yake ni kuja kuwa Rais.


Meja wa Wilson Chacha wa Jeshi la Wokovu ambaye pia aliwahi kumfundisha Sophy miaka ya nyuma akitoa salamu zake katika tukio hilo


Mtoto akisoma risala maalum kwa mgeni rasmi


Mgeni rasmi Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mh. Amoud Abduul Jumaa akikata keki kwa pamoja na Madam Sophy kuashiria uzinduzi rasmi wa tukio hilo.


Mgeni rasmi Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mh. Amoud Abduul Jumaa akimlisha keki Madam Sophy.


Madam Sophy akimlisha keki mgeni rasmi Mbunge wa Kibaha Vijijini, Mh. Amoud Abduul Jumaa 


Madam Sophy akimlisha keki mama yake mzazi wakati wa tukio hilo..


Mama Mzazi wa Sophy akimkumbatia mwanae


Mwanadada, Hoyce Temu aliyejitoa kusaidia watanzania kupitia kipindi maalum cha 'MIMI NA TANZANIA' akilishwa keki na Madam Sophy katika tukio hilo


Hoyce Temu akimpongeza Madam Sophy kwa kuanzisha taasisi hiyo pamoja na kuandaa shughuli hiyo


Madam Sophy akitoa nasaha zake juu ya hatua aliyofikia hadi kuanzisha taasisi hiyo.


Baadhi ya watoto waliofika katika tukio hilo wakifanya maombi maalum kuwaombea wenzao wenye mahitaji maalum.


baadhi ya watoto hao wenye ulemavu wa viungo


Madam Sophy akitoa nasaha zake


Madam Sophy akikabidhi baadhi ya zawadi kwa wanafunzi wa shule ya Makumbusho ambayo anafundisha pamoja na watoto wa shule hiyo ya Jeshi la Wokovu. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...