Skip to main content

SERIKALI YAPONGEZA OPERESHENI SAFISHA YA TFDA, WAUZA DAWA ZA SERIKALI KUHUKUMIWA


Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla amepongeza juhudi za Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) nchini kwa hatua wanazochukua katika utendaji wake ikiwemo zoezi la kukagua madawa yasiyofaa kwa Jamii ikiwemo yale yaliyokwisha muda wake hasa katika zoezi la "Operesheni Safisha" iliyofanywa karibu mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara huku akitaka wale wote waliohusika kupandishwa Mahakamani kwa hatua za kushughulikiwa.

Kigwangalla ameyasema hayo mapema jana Machi 17 jijini Dar es Salaam baada ya kupewa matokeo ya Operesheni Safisha kwa maduka ya dawa muhimu na yasiokuwa na vibali iliyofanywa na Baraza la Wafamasia na TFDA pamoja na Jeshi la Polisi, amesema dawa zilizokamatwa zitaifishwe na kupeleka katika hospitali za serikali.

Amesema kuwa haiwezekani wananchi wakakosa dawa za serikali na kuonekana katika maduka ya dawa na watu hao wakaachwa bila kuchukuliwa hatua.

Kigwangalla amesema kuwa katika operesheni hiyo baadhi ya maduka yanauza dawa ambazo haziko kwenye orodha za dawa ikiwemo ni dawa ya usingizi ambayo inatakiwa kutumika wakati wa operesheni.

Aidha amesema kuwa baadhi ya maduka mengine yamefungwa lakini yanauza dawa nyakati za usiku na kuwataka wanaofanya operesheni kuendelea na wataokutwa wachukuliwe hatua mara moja.

Operesheni hiyo ilianza machi 1 hadi 3 mwaka huu ambapo walikagua maduka 685 katika mikoa tisa na kati hayo maduka 432 yamefungiwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo na kuwa na dawa za serikali pamoja na kuwa dawa za asili.

Aidha Kigwangalla amesema kuwa dawa ni sumu hivyo inatakiwa kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa na wanaouza dawa ambazo hawana orodha nazo wanazalisha matatizo ya kiafya kwa wananchi

Kigwangalla amesema hadi sasa ni dawa 65 tu ndiyo zenye nembo ya serikali na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano pale watakapopata dawa serikali katika duka la dawa.

Amesema kuwa jeshi la polisi lichukue hatua ya kuwabana wale wote waliokutwa na dawa za serikali kuwabana katika kuweza kuwapata waliokuwa wakiwapa dawa hizo.

Tazama MO tv, kuona tukio hilo hapa



Msajili wa Baraza la Famasi nchini, Bi. Elizabeth Shekalaghe akisoma ripoti ya Operesheni Safisha kwa Naibu Waziri pamoja na wanahabari na wakuu wa idara ya TFDA (hawapo pichani). 


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Hiiti Sillo akitoa taarifa yake juuu ya Operesheni Safisha


Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akisoma tamko la Serikali ikiwemo juu ya kuwachukulia sheria kali wahusika wanaohujumu sekta ya Afya hasa upande wa madawa tiba ikiwemo watumishi wanaoiba dawa za Serikali pamoja na wale wanaoendesha maduka ya dawa bila kuwa na vibari.


Baadhi ya maafisa kutoka TFDA na Famasia wakifuatilia tukio hilo.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa tamko hilo.


Mwanahabari wa mtandao wa Michuzi Blog, Bw. Chalila Chibuda akiuliza swali kwa Naibu Waziri Dk. Kigwangalla (hayupo pichani) wakati wa tukio hilo.


Meza kuu ikisikilia swali kwa umakini kutoka wa wanahabari (hawapo pichani).


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akijibu maswali ya wanahabari.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akiwaonesha wanahabari baadhi ya vitu vilivyokamatwa katika Opresheni Safisha. kifaa alichokishika Naibu Waziri ni miongoni mwa vifaa vilivyokutwa vinatumika kuchemshia vifaa vya kufanyia upasuaji/operesheni ikiwemo vifaa vya kutolea mimba.


Baadhi ya vifaa na madawa vilivyokutwa wakati wa operesheni hiyo.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla moja ya dawa ambayo ni ya usingizi hata hivyo ilikutwa katika maduka ya dawa ya kawaida


Madawa hayo.


Madawa hayo yaliyokamatwa.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa agizo la Kiserikali juu ya hatua zitakazochukuliwa dhidi ya wahusika waliokamatwa kwa kukutwa na dawa zilizokwisha muda wake, maduka yasiyokuwa na wafamasia waliosomea na yale yenye kuendeshwa kienyeji.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...